Ezekieli 29 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 29:1-21

Unabii Dhidi Ya Misri

1Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema: 229:2 Yer 25:19; Isa 19:1-17; Yer 46:2; Eze 25:2; 30:1-26; 31:1-18“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote. 329:3 Yer 44:30; Za 68:30; Isa 27:1; Eze 32:2; Yer 46:8Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri,

joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako.

Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe;

niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”

429:4 2Fal 19:28; Ay 41:2; Eze 38:4Lakini nitatia ndoana katika mataya yako

nami nitawafanya samaki wa vijito vyako

washikamane na magamba yako.

Nitakutoa katikati ya vijito vyako,

pamoja na samaki wote

walioshikamana na magamba yako.

529:5 Yer 7:33; 34:20; 8:2; Eze 31:13; 32:4-6; 39:4Nitakutupa jangwani,

wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako.

Utaanguka uwanjani,

nawe hutakusanywa au kuchukuliwa.

Nitakutoa uwe chakula

kwa wanyama wa nchi

na ndege wa angani.

629:6 2Fal 18:21; Isa 36:6Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

“ ‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli. 729:7 Yer 17:5; Eze 17:15-17; 2Fal 18:21; Isa 36:6Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.

829:8 Eze 14:17; 25:13; 32:11-13“ ‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao. 929:9 Eze 30:7-8, 13-19; Mit 16:18; Yer 46:8Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

“ ‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,” 1029:10 Eze 30:6-12; Yer 21:13; Kut 3:22; Yer 46:19; Kut 14:2; Isa 18:1kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia. 1129:11 Eze 32:13Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini. 1229:12 Yer 46:19; Eze 30:7; 34:10Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.

1329:13 Isa 19:23; Yer 46:26“ ‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa. 1429:14 Isa 11:11; Eze 30:14; 17:14; Isa 19:22; Yer 46:26Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi,29:14 Pathrosi ni Misri ya Juu. nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu. 1529:15 Zek 10:11Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine. 1629:16 2Nya 32:10; Isa 20:5; Hos 8:13; Isa 30:2; Mao 4:17; Hes 5:15Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’ ”

1729:17 Eze 30:20; 24:1; 40:1Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema: 1829:18 Yer 27:6; Law 13:40; Ay 1:20; Yer 39:1“Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro. 1929:19 Yer 43:10-13; Eze 32:11; Yer 27:6; Isa 19:4; Eze 26:5; 30:4, 10Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake. 2029:20 Isa 45:1; Yer 25; 9; Isa 43:3; 10:6-7Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.

2129:21 Lk 1:69; 1Sam 2:10; Za 132:17; Eze 33:22; 3:27; 24:27“Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

New International Version

Ezekiel 29:1-21

A Prophecy Against Egypt

Judgment on Pharaoh

1In the tenth year, in the tenth month on the twelfth day, the word of the Lord came to me: 2“Son of man, set your face against Pharaoh king of Egypt and prophesy against him and against all Egypt. 3Speak to him and say: ‘This is what the Sovereign Lord says:

“ ‘I am against you, Pharaoh king of Egypt,

you great monster lying among your streams.

You say, “The Nile belongs to me;

I made it for myself.”

4But I will put hooks in your jaws

and make the fish of your streams stick to your scales.

I will pull you out from among your streams,

with all the fish sticking to your scales.

5I will leave you in the desert,

you and all the fish of your streams.

You will fall on the open field

and not be gathered or picked up.

I will give you as food

to the beasts of the earth and the birds of the sky.

6Then all who live in Egypt will know that I am the Lord.

“ ‘You have been a staff of reed for the people of Israel. 7When they grasped you with their hands, you splintered and you tore open their shoulders; when they leaned on you, you broke and their backs were wrenched.29:7 Syriac (see also Septuagint and Vulgate); Hebrew and you caused their backs to stand

8“ ‘Therefore this is what the Sovereign Lord says: I will bring a sword against you and kill both man and beast. 9Egypt will become a desolate wasteland. Then they will know that I am the Lord.

“ ‘Because you said, “The Nile is mine; I made it,” 10therefore I am against you and against your streams, and I will make the land of Egypt a ruin and a desolate waste from Migdol to Aswan, as far as the border of Cush.29:10 That is, the upper Nile region 11The foot of neither man nor beast will pass through it; no one will live there for forty years. 12I will make the land of Egypt desolate among devastated lands, and her cities will lie desolate forty years among ruined cities. And I will disperse the Egyptians among the nations and scatter them through the countries.

13“ ‘Yet this is what the Sovereign Lord says: At the end of forty years I will gather the Egyptians from the nations where they were scattered. 14I will bring them back from captivity and return them to Upper Egypt, the land of their ancestry. There they will be a lowly kingdom. 15It will be the lowliest of kingdoms and will never again exalt itself above the other nations. I will make it so weak that it will never again rule over the nations. 16Egypt will no longer be a source of confidence for the people of Israel but will be a reminder of their sin in turning to her for help. Then they will know that I am the Sovereign Lord.’ ”

Nebuchadnezzar’s Reward

17In the twenty-seventh year, in the first month on the first day, the word of the Lord came to me: 18“Son of man, Nebuchadnezzar king of Babylon drove his army in a hard campaign against Tyre; every head was rubbed bare and every shoulder made raw. Yet he and his army got no reward from the campaign he led against Tyre. 19Therefore this is what the Sovereign Lord says: I am going to give Egypt to Nebuchadnezzar king of Babylon, and he will carry off its wealth. He will loot and plunder the land as pay for his army. 20I have given him Egypt as a reward for his efforts because he and his army did it for me, declares the Sovereign Lord.

21“On that day I will make a horn29:21 Horn here symbolizes strength. grow for the Israelites, and I will open your mouth among them. Then they will know that I am the Lord.”