Ezekieli 28 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 28:1-26

Unabii Dhidi Ya Mfalme Wa Tiro

1Neno la Bwana likanijia kusema: 228:2 Isa 14:13; Mwa 3:4-5; 2The 2:4; Kum 8:14; Mit 16:18; Sef 2:15; Za 9:20“Mwanadamu, mwambie mfalme wa Tiro, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Kwa sababu moyo wako umejivuna

na umesema, “Mimi ni mungu;

nami ninaketi katika kiti cha enzi cha mungu

katika moyo wa bahari.”

Lakini wewe ni mwanadamu, wala si mungu,

ingawa unafikiri kuwa una hekima kama mungu.

328:3 Dan 1:20; 2:20-23, 28; Zek 9:2; Eze 14:14Je, wewe una hekima kuliko Danieli?

Je, hakuna siri iliyofichika kwako?

428:4 Zek 9:3; Isa 10:13Kwa hekima yako na ufahamu wako,

umejipatia utajiri,

nawe umejikusanyia dhahabu

na fedha katika hazina zako.

528:5 Ay 31:25; Hos 13:6; Kum 8:12-14; Isa 23:8; Yer 9:23; 9:23; Eze 27:33Kwa werevu wako mwingi katika biashara,

umeongeza utajiri wako

na kwa sababu ya utajiri wako

moyo wako umekuwa na kiburi.

6“ ‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Kwa sababu unafikiri una hekima,

mwenye hekima kama mungu,

728:7 Eze 32:12; 30:11; 31:12; Yer 9:23; Eze 7:24mimi nitawaleta wageni dhidi yako,

taifa katili kuliko yote;

watafuta panga zao dhidi ya uzuri wa hekima yako,

na kuchafua fahari yako inayongʼaa.

828:8 Za 55:23; Eze 32:30; 27:27; 26:12; Ufu 18:7Watakushusha chini shimoni,

nawe utakufa kifo cha kikatili

katika moyo wa bahari.

928:9 Isa 31:3; Eze 16:49Je, wakati huo utasema, “Mimi ni mungu,”

mbele ya wale wanaokuua?

Utakuwa mwanadamu tu, wala si mungu,

mikononi mwa hao wanaokuua.

1028:10 1Sam 14:6; Yer 9:26; Eze 32:18-19Utakufa kifo cha wasiotahiriwa

kwa mkono wa wageni.

Kwa kuwa mimi nimenena, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

11Neno la Bwana likanijia kusema: 1228:12 Eze 19:1; 27:2-4“Mwanadamu, mfanyie maombolezo mfalme wa Tiro, nawe umwambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ulikuwa kipeo cha ukamilifu,

ukiwa umejaa hekima

na mkamilifu katika uzuri.

1328:13 Mwa 2:8; Eze 31:8-9; 27:16; Ufu 17:4; Isa 14:11; Ufu 21:20Ulikuwa ndani ya Edeni,

bustani ya Mungu;

kila kito cha thamani kilikupamba:

akiki nyekundu, yakuti manjano na zumaridi,

krisolitho, shohamu na yaspi,

yakuti samawi, almasi na zabarajadi.

Kuwekwa kwa hayo mapambo na kushikizwa kwake

kulifanywa kwa dhahabu;

siku ile ulipoumbwa yaliandaliwa tayari.

1428:14 Kut 30:26; 40:9; 25:17-20Ulitiwa mafuta kuwa kerubi mlinzi,

kwa kuwa hivyo ndivyo nilivyokuweka wakfu.

Ulikuwa kwenye mlima mtakatifu wa Mungu;

ulitembea katikati ya vito vya moto.

15Ulikuwa mnyofu katika njia zako

tangu siku ile ya kuumbwa kwako,

hadi uovu ulipoonekana ndani yako.

1628:16 Mwa 6:11; Hab 2:17; Mwa 3:24Kutokana na biashara yako iliyoenea,

ulijazwa na dhuluma,

nawe ukatenda dhambi.

Hivyo nilikuondoa kwa aibu kutoka mlima wa Mungu,

nami nikakufukuza, ee kerubi mlinzi,

kutoka katikati ya vito vya moto.

1728:17 Isa 10:12; Eze 16:49; 31:10; 19:12Moyo wako ukawa na kiburi

kwa ajili ya uzuri wako,

nawe ukaiharibu hekima yako

kwa sababu ya fahari yako.

Kwa hiyo nikakutupa chini;

nimekufanya kioja mbele ya wafalme.

1828:18 Oba 1:18; Mal 4:3; Zek 9:2-4Kwa dhambi zako nyingi na biashara yako ya dhuluma,

umenajisi mahali pako patakatifu.

Kwa hiyo nilifanya moto utoke ndani yako,

nao ukakuteketeza,

nami nikakufanya majivu juu ya nchi,

machoni pa wote waliokuwa wakitazama.

1928:19 Yer 51:64; Eze 26:21; Law 26:21Mataifa yote yaliyokujua

yanakustajabia;

umefikia mwisho wa kutisha

na hutakuwepo tena milele.’ ”

Unabii Dhidi Ya Sidoni

20Neno la Bwana likanijia kusema: 2128:21 Eze 6:2; 13:17; Yer 25:2; Mwa 10:15“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Sidoni, ukatabiri dhidi yake, 2228:22 Kut 14:4; Za 9:16; Eze 30:19; 39:13; Law 10:3nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Mimi ni kinyume chako, ee Sidoni,

nami nitapata utukufu ndani yako.

Nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana,

nitakapotekeleza hukumu zangu

na kuonyesha utakatifu wangu ndani yake.

2328:23 Eze 5:17; 38:22Nitapeleka tauni ndani yake

na kufanya damu itiririke katika barabara zake.

Waliochinjwa wataanguka ndani yake,

kwa upanga dhidi yake kila upande.

Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.

2428:24 Hes 33:55; Yos 23:13; Isa 5:6; Eze 2:6“ ‘Nyumba ya Israeli hawatakuwa tena na majirani wenye nia ya kuwadhuru wanaoumiza kama michongoma na miiba mikali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.

2528:25 Za 106:47; Yer 32:37; Isa 11:12; Eze 20:41; Yer 12:15; 12:15; 23:8; Eze 11:17“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapoikusanya nyumba ya Israeli kutoka mataifa ambako wametawanyika, nitajionyesha kuwa mtakatifu miongoni mwao machoni pa mataifa. Ndipo watakapoishi katika nchi yao wenyewe, niliyompa mtumishi wangu Yakobo. 2628:26 Law 25:18; Yer 23:6; Hos 2:15; Amo 9:14-15; 1Fal 4:25; Yer 17:25; Kum 20:6; Eze 38:8; 39:26-27; Isa 65:21Wataishi humo kwa salama na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu, wataishi kwa salama nitakapowaadhibu majirani zao wote ambao waliwafanyia uovu. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.’ ”

King James Version

Ezekiel 28:1-26

1The word of the LORD came again unto me, saying, 2Son of man, say unto the prince of Tyrus, Thus saith the Lord GOD; Because thine heart is lifted up, and thou hast said, I am a God, I sit in the seat of God, in the midst of the seas; yet thou art a man, and not God, though thou set thine heart as the heart of God:28.2 midst: Heb. heart 3Behold, thou art wiser than Daniel; there is no secret that they can hide from thee: 4With thy wisdom and with thine understanding thou hast gotten thee riches, and hast gotten gold and silver into thy treasures: 5By thy great wisdom and by thy traffick hast thou increased thy riches, and thine heart is lifted up because of thy riches:28.5 thy great…: Heb. the greatness of thy wisdom 6Therefore thus saith the Lord GOD; Because thou hast set thine heart as the heart of God; 7Behold, therefore I will bring strangers upon thee, the terrible of the nations: and they shall draw their swords against the beauty of thy wisdom, and they shall defile thy brightness. 8They shall bring thee down to the pit, and thou shalt die the deaths of them that are slain in the midst of the seas. 9Wilt thou yet say before him that slayeth thee, I am God? but thou shalt be a man, and no God, in the hand of him that slayeth thee.28.9 of him that slayeth: or, of him that woundeth 10Thou shalt die the deaths of the uncircumcised by the hand of strangers: for I have spoken it, saith the Lord GOD.

11¶ Moreover the word of the LORD came unto me, saying, 12Son of man, take up a lamentation upon the king of Tyrus, and say unto him, Thus saith the Lord GOD; Thou sealest up the sum, full of wisdom, and perfect in beauty. 13Thou hast been in Eden the garden of God; every precious stone was thy covering, the sardius, topaz, and the diamond, the beryl, the onyx, and the jasper, the sapphire, the emerald, and the carbuncle, and gold: the workmanship of thy tabrets and of thy pipes was prepared in thee in the day that thou wast created.28.13 sardius: or, ruby28.13 beryl: or, chrysolite28.13 emerald: or, chrysoprase 14Thou art the anointed cherub that covereth; and I have set thee so: thou wast upon the holy mountain of God; thou hast walked up and down in the midst of the stones of fire. 15Thou wast perfect in thy ways from the day that thou wast created, till iniquity was found in thee. 16By the multitude of thy merchandise they have filled the midst of thee with violence, and thou hast sinned: therefore I will cast thee as profane out of the mountain of God: and I will destroy thee, O covering cherub, from the midst of the stones of fire. 17Thine heart was lifted up because of thy beauty, thou hast corrupted thy wisdom by reason of thy brightness: I will cast thee to the ground, I will lay thee before kings, that they may behold thee. 18Thou hast defiled thy sanctuaries by the multitude of thine iniquities, by the iniquity of thy traffick; therefore will I bring forth a fire from the midst of thee, it shall devour thee, and I will bring thee to ashes upon the earth in the sight of all them that behold thee. 19All they that know thee among the people shall be astonished at thee: thou shalt be a terror, and never shalt thou be any more.28.19 a terror: Heb. terrors

20¶ Again the word of the LORD came unto me, saying, 21Son of man, set thy face against Zidon, and prophesy against it, 22And say, Thus saith the Lord GOD; Behold, I am against thee, O Zidon; and I will be glorified in the midst of thee: and they shall know that I am the LORD, when I shall have executed judgments in her, and shall be sanctified in her. 23For I will send into her pestilence, and blood into her streets; and the wounded shall be judged in the midst of her by the sword upon her on every side; and they shall know that I am the LORD.

24¶ And there shall be no more a pricking brier unto the house of Israel, nor any grieving thorn of all that are round about them, that despised them; and they shall know that I am the Lord GOD. 25Thus saith the Lord GOD; When I shall have gathered the house of Israel from the people among whom they are scattered, and shall be sanctified in them in the sight of the heathen, then shall they dwell in their land that I have given to my servant Jacob. 26And they shall dwell safely therein, and shall build houses, and plant vineyards; yea, they shall dwell with confidence, when I have executed judgments upon all those that despise them round about them; and they shall know that I am the LORD their God.28.26 safely: or, with confidence28.26 despise: or, spoil