Ezekieli 27 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 27:1-36

Maombolezo Kwa Ajili Ya Tiro

1Neno la Bwana likanijia kusema: 227:2 Eze 19:1; 26:17; 28:12; 32:2“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro. 327:3 Hos 9:13; Isa 23:9; Eze 28:2; Za 83:16Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ee Tiro, wewe umesema,

“Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”

427:4 Eze 28:12Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari,

wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.

527:5 Kum 3:9; Isa 2:13Walizifanya mbao zako zote

kwa misunobari itokayo Seniri;27:5 Yaani Hermoni.

walichukua mierezi kutoka Lebanoni

kukutengenezea mlingoti.

627:6 Za 29:9; Zek 11:2; Mwa 10:4; Isa 23:12; Yer 22:20; Hes 21:33Walichukua mialoni toka Bashani

wakakutengenezea makasia yako;

kwa miti ya msanduku

kutoka pwani ya Kitimu

wakatengeneza sitaha27:6 Yaani sakafu ya merikebu au mashua. yako

na kuipamba kwa pembe za ndovu.

727:7 Kut 25:4; Yer 10:9; Isa 19:9; Mwa 10:4; Kut 26:36Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako,

nacho kilikuwa bendera yako;

chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau

kutoka visiwa vya Elisha.

827:8 Mwa 10:18; 1Fal 9:23-27Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako;

watu wako wenye ustadi, ee Tiro,

walikuwa ndio mabaharia wako.

927:9 Yos 13:5; 1Fal 5:18; Za 104:26Wazee wa Gebali27:9 Yaani Bubilo, mji wa zamani sana wa Ufoinike (kama kilomita 80 kaskazini mwa Beiruti). pamoja na mafundi stadi

walikuwa mafundi wako melini.

Meli zote za baharini na mabaharia wao

walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.

1027:10 Dan 8:20; Mwa 10:6; Nah 3:9; Yer 46:9; Eze 38:5; 2Nya 36:20; Isa 66:19; Wim 4:4“ ‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu

walikuwa askari katika jeshi lako.

Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako,

wakileta fahari yako.

1127:11 Eze 27:27Watu wa Arvadi na wa Heleki

walikuwa juu ya kuta zako pande zote;

watu wa Gamadi

walikuwa kwenye minara yako.

Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako;

wakaukamilisha uzuri wako.

1227:12 Mwa 10:4; 2Nya 20:36“ ‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.

1327:13 Isa 66:19; Ufu 18:13; Yoe 3:6; Mwa 10:2; Eze 32:26; 38:2“ ‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.

1427:14 Mwa 10:3; Eze 38:6“ ‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.

1527:15 Mwa 10:7; Yer 25:22; 1Fal 10:22; Ufu 18:12“ ‘Watu wa Dedani27:15 Yaani Rhodes. walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.

1627:16 Amu 10:6; Isa 7:1-8; Kut 28:18; 39:11; Eze 28:13; 16:10; Ay 28:18“ ‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe27:16 Yaani marijani, jiwe laini la pwani au baharini, kama mawe ya chokaa. na akiki nyekundu.

1727:17 Amu 11:33; Mdo 12:20; Mwa 43:11“ ‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.

1827:18 Mwa 14:15; Eze 47:16-18“ ‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.

1927:19 Kut 30:24; Mwa 10:2, 27“ ‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.

2027:20 Mwa 10:7“ ‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.

2127:21 Mwa 25:13; Isa 60:7; 2Nya 9:14; Isa 21:17“ ‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.

2227:22 1Fal 10:1-2; Isa 60:8; Mwa 43:11; Za 72:10; Ufu 18:12“ ‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.

2327:23 Mwa 11:26; 2Fal 19:12; Isa 37:12; Mwa 10:22; Hes 24:24“ ‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe. 24Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.

2527:25 Mwa 10:4; Isa 2:16; Ufu 18:3“ ‘Merikebu za Tarshishi ndizo

zinazokusafirishia bidhaa zako.

Umejazwa shehena kubwa

katika moyo wa bahari.

2627:26 Mwa 41:6; Za 48:7; Yer 18:7Wapiga makasia wako wanakupeleka

mpaka kwenye maji makavu.

Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande

katika moyo wa bahari.

2727:27 Mit 11:4; Eze 28:8Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako,

mabaharia wako, manahodha wako,

mafundi wako wa meli,

wafanyabiashara wako na askari wako wote,

na kila mmoja aliyeko melini

atazama kwenye moyo wa bahari

siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.

2827:28 Yer 49:21; Eze 26:15Nchi za pwani zitatetemeka

wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.

2927:29 Ufu 18:17Wote wapigao makasia

wataacha meli zao,

mabaharia wote na wanamaji wote

watasimama pwani.

3027:30 Yos 7:6; Yer 6:26; Ufu 18:17-19; Mao 2:10Watapaza sauti zao

na kulia sana kwa ajili yako;

watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao

na kujivingirisha kwenye majivu.

3127:31 Isa 16:9; Ay 3:20; Es 4:1; Law 13:40; Ay 1:20; Isa 3:17; Yer 48:37; Isa 22:12; Mao 2:10; Eze 7:16Watanyoa nywele zao kwa ajili yako,

nao watavaa nguo za magunia.

Watakulilia kwa uchungu wa moyo

na kwa maombolezo makuu.

3227:32 Eze 19:1; 26:17; Isa 23:1-6Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako,

watafanya maombolezo kukuhusu wakisema:

“Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro,

katika moyo wa bahari?”

3327:33 Eze 28:4-5Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini,

ulitosheleza mataifa mengi;

kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako

ulitajirisha wafalme wa dunia.

3427:34 Za 9:4Sasa umevunjavunjwa na bahari,

katika vilindi vya maji,

bidhaa zako na kundi lako lote

vimezama pamoja nawe.

3527:35 Eze 26:15; Law 26:32; Ay 18:20; Eze 32:10Wote waishio katika nchi za pwani

wanakustaajabia;

wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu,

nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.

3627:36 Yer 18:16; Sef 2:15; Eze 26:21; Za 37:10; Yer 19:8; 49:17; 50:13Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka;

umefikia mwisho wa kutisha

nawe hutakuwepo tena.’ ”

King James Version

Ezekiel 27:1-36

1The word of the LORD came again unto me, saying, 2Now, thou son of man, take up a lamentation for Tyrus; 3And say unto Tyrus, O thou that art situate at the entry of the sea, which art a merchant of the people for many isles, Thus saith the Lord GOD; O Tyrus, thou hast said, I am of perfect beauty.27.3 of perfect…: Heb. perfect of beauty 4Thy borders are in the midst of the seas, thy builders have perfected thy beauty.27.4 midst: Heb. heart 5They have made all thy ship boards of fir trees of Senir: they have taken cedars from Lebanon to make masts for thee.27.5 made: Heb. built 6Of the oaks of Bashan have they made thine oars; the company of the Ashurites have made thy benches of ivory, brought out of the isles of Chittim.27.6 the company…: or, they have made thy hatches of ivory well trodden27.6 company: Heb. daughter 7Fine linen with broidered work from Egypt was that which thou spreadest forth to be thy sail; blue and purple from the isles of Elishah was that which covered thee.27.7 blue…: or, purple and scarlet 8The inhabitants of Zidon and Arvad were thy mariners: thy wise men, O Tyrus, that were in thee, were thy pilots. 9The ancients of Gebal and the wise men thereof were in thee thy calkers: all the ships of the sea with their mariners were in thee to occupy thy merchandise.27.9 calkers: or, stoppers of chinks: Heb. strengtheners, etc 10They of Persia and of Lud and of Phut were in thine army, thy men of war: they hanged the shield and helmet in thee; they set forth thy comeliness. 11The men of Arvad with thine army were upon thy walls round about, and the Gammadims were in thy towers: they hanged their shields upon thy walls round about; they have made thy beauty perfect. 12Tarshish was thy merchant by reason of the multitude of all kind of riches; with silver, iron, tin, and lead, they traded in thy fairs. 13Javan, Tubal, and Meshech, they were thy merchants: they traded the persons of men and vessels of brass in thy market.27.13 market: or, merchandise 14They of the house of Togarmah traded in thy fairs with horses and horsemen and mules. 15The men of Dedan were thy merchants; many isles were the merchandise of thine hand: they brought thee for a present horns of ivory and ebony. 16Syria was thy merchant by reason of the multitude of the wares of thy making: they occupied in thy fairs with emeralds, purple, and broidered work, and fine linen, and coral, and agate.27.16 the wares…: Heb. thy works27.16 agate: or, chrysoprase 17Judah, and the land of Israel, they were thy merchants: they traded in thy market wheat of Minnith, and Pannag, and honey, and oil, and balm.27.17 balm: or, rosin 18Damascus was thy merchant in the multitude of the wares of thy making, for the multitude of all riches; in the wine of Helbon, and white wool. 19Dan also and Javan going to and fro occupied in thy fairs: bright iron, cassia, and calamus, were in thy market.27.19 going…: or, Meuzal 20Dedan was thy merchant in precious clothes for chariots.27.20 precious…: Heb. clothes of freedom 21Arabia, and all the princes of Kedar, they occupied with thee in lambs, and rams, and goats: in these were they thy merchants.27.21 they occupied…: Heb. they were the merchants of thy hand 22The merchants of Sheba and Raamah, they were thy merchants: they occupied in thy fairs with chief of all spices, and with all precious stones, and gold. 23Haran, and Canneh, and Eden, the merchants of Sheba, Asshur, and Chilmad, were thy merchants. 24These were thy merchants in all sorts of things, in blue clothes, and broidered work, and in chests of rich apparel, bound with cords, and made of cedar, among thy merchandise.27.24 all…: or, excellent things27.24 clothes: Heb. foldings 25The ships of Tarshish did sing of thee in thy market: and thou wast replenished, and made very glorious in the midst of the seas.

26¶ Thy rowers have brought thee into great waters: the east wind hath broken thee in the midst of the seas.27.26 midst: Heb. heart 27Thy riches, and thy fairs, thy merchandise, thy mariners, and thy pilots, thy calkers, and the occupiers of thy merchandise, and all thy men of war, that are in thee, and in all thy company which is in the midst of thee, shall fall into the midst of the seas in the day of thy ruin.27.27 and in…: or, even with all27.27 midst of the seas: Heb. heart, etc 28The suburbs shall shake at the sound of the cry of thy pilots.27.28 suburbs: or, waves 29And all that handle the oar, the mariners, and all the pilots of the sea, shall come down from their ships, they shall stand upon the land; 30And shall cause their voice to be heard against thee, and shall cry bitterly, and shall cast up dust upon their heads, they shall wallow themselves in the ashes: 31And they shall make themselves utterly bald for thee, and gird them with sackcloth, and they shall weep for thee with bitterness of heart and bitter wailing. 32And in their wailing they shall take up a lamentation for thee, and lament over thee, saying, What city is like Tyrus, like the destroyed in the midst of the sea? 33When thy wares went forth out of the seas, thou filledst many people; thou didst enrich the kings of the earth with the multitude of thy riches and of thy merchandise. 34In the time when thou shalt be broken by the seas in the depths of the waters thy merchandise and all thy company in the midst of thee shall fall. 35All the inhabitants of the isles shall be astonished at thee, and their kings shall be sore afraid, they shall be troubled in their countenance. 36The merchants among the people shall hiss at thee; thou shalt be a terror, and never shalt be any more.27.36 a terror: Heb. terrors27.36 never…: Heb. shalt not be for ever