Ezekieli 23 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 23:1-49

Dada Wawili Makahaba

1Neno la Bwana likanijia kusema: 223:2 Eze 16:45-46; Yer 3:7“Mwanadamu, walikuwepo wanawake wawili, binti wa mama mmoja. 323:3 Yos 24:14; Law 17:7; Isa 1:21; Za 25:7; Eze 16:15Wakawa makahaba huko Misri, wakajitia kwenye ukahaba tangu ujana wao. Katika nchi ile vifua vyao vya ubikira vikakumbatiwa huko na wakapoteza ubikira wao. 423:4 Eze 16:8, 20; 16:46Mkubwa aliitwa Ohola na mdogo wake Oholiba. Walikuwa wangu nao wakazaa wavulana na msichana. Ohola ni Samaria, Oholiba ni Yerusalemu.

523:5 2Fal 16:7; 15:19; Hos 5:13; 8:9“Ohola akajitia kwenye ukahaba alipokuwa bado ni wangu, akatamani sana wapenzi wake, mashujaa Waashuru, 6waliovaa nguo za buluu, watawala na majemadari, wote walikuwa wanaume vijana wa kuvutia, wapandao farasi. 723:7 Isa 57:8; Hos 6:10; 5:3Akafanya ukahaba na wasomi wote wa Ashuru, na kujinajisi kwa sanamu zote za kila mwanaume aliyemtamani. 823:8 Kut 32:4; Eze 16:15Hakuacha ukahaba wake aliouanza huko Misri, wakati ambapo tangu ujana wake wanaume walilala naye, wakikumbatia kifua cha ubikira wake na kumwaga tamaa zao juu yake.

923:9 2Fal 18:11; Hos 11:5; 2Fal 17:3-6; Yer 4:30“Kwa hiyo nilimtia mikononi mwa wapenzi wake, Waashuru, kwa kuwa ndio aliowatamani. 1023:10 Hos 2:10; Eze 16:36, 41; Yer 42:10Wakamvua nguo zake wakamwacha uchi, wakawachukua wanawe na binti zake, naye wakamuua kwa upanga. Akawa kitu cha kudharauliwa miongoni mwa wanawake na adhabu ikatolewa dhidi yake.

1123:11 Yer 3:8-11; Eze 16:51“Oholiba dada yake aliliona jambo hili, lakini kwa tamaa zake na ukahaba wake, akaharibu tabia zake kuliko Ohola dada yake. 1223:12 2Fal 16:7-15; 2Nya 28:16; Eze 16:15; 28Yeye naye aliwatamani Waashuru, watawala na majemadari, mashujaa waliovalia sare, wapandao farasi, wanaume vijana wote waliovutia. 1323:13 Hos 12:2; 2Fal 17:19Nikaona kuwa yeye pia alijinajisi, wote wawili wakaelekea njia moja.

1423:14 Eze 8:10; Nah 2:3; Yer 22:14“Lakini yeye akazidisha ukahaba wake. Akaona wanaume waliochorwa ukutani, picha za Wakaldayo23:14 Wakaldayo yaani Wababeli. waliovalia nguo nyekundu, 1523:15 Isa 5:27wakiwa na mikanda viunoni mwao na vilemba vichwani mwao, wote walifanana na maafisa wa Babeli wapandao magari ya vita, wenyeji wa Ukaldayo.23:15 Ukaldayo yaani Babeli. 1623:16 Isa 57:9; Eze 6:9Mara tu alipowaona, aliwatamani, akatuma wajumbe kwao huko Ukaldayo. 1723:17 Yer 40:9; Eze 16:29Ndipo hao Wababeli wakaja kwake kwenye kitanda cha mapenzi, nao katika tamaa zao wakamtia unajisi. Baada ya kutiwa unajisi, akawaacha kwa kuwachukia. 1823:18 Za 106:40; Yer 6:8; 12:8; Amo 5:21; Zek 11:8; Isa 57:8; Za 78:59Alipofanya ukahaba wake waziwazi na kuonyesha hadharani uchi wake, nilimwacha kwa kumchukia, kama vile nilivyokuwa nimemwacha dada yake. 1923:19 Eze 23:3Lakini akazidisha zaidi ukahaba wake alipozikumbuka siku zake za ujana, alipokuwa kahaba huko Misri. 2023:20 Eze 16:26Huko aliwatamani wapenzi wake, ambao viungo vyao vya uzazi ni kama vya punda, na kile kiwatokacho ni kama kiwatokacho farasi. 2123:21 Eze 16:26Hivyo ulitamani uasherati wa ujana wako wakati ulipokuwa Misri, kifua chako kilipokumbatiwa, na walipokutomasa kwa sababu ya matiti yako machanga.

2223:22 Yer 4:30; Eze 16:37“Kwa hiyo, Oholiba, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawachochea wapenzi wako wawe kinyume na wewe, wale uliowaacha kwa kuchukia, nitawaleta dhidi yako kutoka kila upande: 2323:23 2Fal 20:14-15; Yer 40:9; 50:21; 2Fal 24:2; Mwa 11:28Wababeli na Wakaldayo wote, watu kutoka Pekodi, na Shoa na Koa, wakiwa pamoja na Waashuru wote, vijana wazuri, wote wakiwa watawala na majemadari, maafisa wa magari ya vita na watu wa vyeo vya juu, wote wakiwa wamepanda farasi. 2423:24 Yer 47:3; Nah 2:4; Yer 39:5-6; Eze 26:7-10Watakuja dhidi yako wakiwa na silaha, magari ya vita, magari ya kukokota, pamoja na umati mkubwa wa watu. Watakuzingira pande zote kwa ngao na vigao na kofia za chuma. Nitakutia mikononi mwao ili wakuadhibu, nao watakuadhibu sawasawa na sheria zao. 2523:25 Eze 24:21; Yer 12:9; Eze 16:38; 20:47-48; Kum 29:20Nitaelekeza wivu wa hasira yangu dhidi yako, nao watakushughulikia kwa hasira kali. Watakatilia mbali pua yako na masikio yako, na wale watakaosalia miongoni mwako watauawa kwa upanga. Watachukua wana wako na binti zako, na wale watakaosalia miongoni mwenu watateketezwa kwa moto. 2623:26 Yer 13:22; Isa 3:18-23; Eze 16:39; Ufu 17:16Watakuvua pia nguo zako na kuchukua mapambo yako yaliyotengenezwa kwa vito na dhahabu. 2723:27 Eze 16:41; 22:15Hivyo ndivyo nitakavyokomesha uasherati wako na ukahaba wako uliouanza huko Misri. Hutatazama vitu hivi kwa kuvitamani tena, wala kukumbuka Misri tena.

2823:28 Eze 34:20; Yer 21:7“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kukutia mikononi mwa wale unaowachukia, kwa wale uliojitenga nao kwa kuwachukia. 2923:29 Kum 28:48; Eze 16:36-39; 22:9; Yer 13:27; Mik 1:11Watakushughulikia kwa chuki na kukunyangʼanya kila kitu ulichokifanyia kazi. Watakuacha uchi na mtupu na aibu ya ukahaba wako itafunuliwa. Uasherati wako na uzinzi wako 3023:30 Za 106:37-38; Eze 6:9; Sef 3:1umekuletea haya yote, kwa sababu ulitamani mataifa na kujinajisi kwa sanamu zao. 3123:31 Yer 25:15; 2Fal 21:13Umeiendea njia ya dada yako, hivyo nitakitia kikombe chake mkononi mwako.

3223:32 Za 60:3; Isa 51:17; Eze 22:4-5; Yer 25:15; Hos 7:16; Za 44:13“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“Utakinywea kikombe cha dada yako,

kikombe kikubwa na chenye kina kirefu;

nitaletea juu yako dharau na dhihaka,

kwa kuwa kimejaa sana.

3323:33 Yer 25:15; Eze 12:19Utalewa ulevi na kujawa huzuni,

kikombe cha maangamizo na ukiwa,

kikombe cha dada yako Samaria.

3423:34 Isa 51:17; Za 16:5; Yer 25:27Utakinywa chote na kukimaliza;

utakivunja vipande vipande

na kuyararua matiti yako.

Nimenena haya, asema Bwana Mwenyezi.

3523:35 Yer 2:23; 3:21; Eze 22:12; 1Fal 14:9; Neh 9:26“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa kuwa tangu uliponisahau mimi na kunitupa nyuma yako, lazima ubebe matokeo ya uasherati wako na ukahaba wako.”

3623:36 Eze 16:2; Isa 58:1; Mik 3:8; Eze 22:2Bwana akaniambia, “Mwanadamu, Je, utawahukumu Ohola na Oholiba? Basi wakabili kwa ajili ya matendo yao ya machukizo, 3723:37 Eze 16:36kwa kuwa wamefanya uzinzi na damu imo mikononi mwao. Wamefanya uzinzi na sanamu zao, hata wamewatoa watoto wao walionizalia kuwa kafara, kuwa chakula kwao. 3823:38 Law 15:31; Neh 10:31Pia wamenifanyia hili: wakati huo huo wamenajisi patakatifu pangu na kuzitangua Sabato zangu. 3923:39 2Fal 21:4; Yer 7:10; Eze 22:8Siku ile ile walitoa watoto wao kuwa kafara kwa sanamu zao, waliingia patakatifu pangu na kupatia unajisi. Hilo ndilo walilolifanya katika nyumba yangu.

4023:40 Yer 4:30; Isa 57:9; 2Fal 9:30; Hos 2:13; Eze 16:13-19“Walituma hata wajumbe kuwaita watu kutoka mbali, nao walipowasili ulioga kwa ajili yao, ukapaka macho yako rangi na ukavaa mapambo yako yaliyotengenezwa kwa vito vya dhahabu. 4123:41 Mit 7:17; Amo 6:4; Isa 65:11; Eze 16:18-19; 41:22; 16:38; Hos 6:5Ukaketi kwenye kiti cha anasa, kukiwa na meza iliyoandaliwa mbele yake ambayo juu yake ulikuwa umeweka uvumba na mafuta ambayo yalikuwa yangu.

4223:42 Za 73:5; 2Nya 9:1; Mwa 24:30; Eze 16:11-12“Kelele za umati wa watu wasiojali zilikuwa zimemzunguka, wakaleta watu wengi waliokuwa wakifanya makelele na walevi kutoka nyikani, ambao walitia bangili kwenye mikono ya yule mwanamke na dada yake na pia taji nzuri za kupendeza kwenye vichwa vyao. 4323:43 Eze 23:3Ndipo nikasema kuhusu yule aliyechakazwa na uzinzi, ‘Basi wamtumie kama kahaba, kwa kuwa ndivyo alivyo.’ 44Nao wakazini naye. Kama vile watu wazinivyo na kahaba, ndiyo hivyo walivyozini na hao wanawake waasherati, Ohola na Oholiba. 4523:45 Eze 16:38Lakini watu wenye haki, watawahukumia adhabu wanawake wafanyao uzinzi na kumwaga damu, kwa kuwa ni wazinzi na damu iko mikononi mwao.

4623:46 Eze 16:40“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Leteni watu wengi wenye makelele dhidi yao na uwaache wapate hofu na watekwe nyara. 4723:47 Yer 34:22; Eze 16:40-41; 2Nya 36:17-19Hao watu wengi watawapiga kwa mawe na kuwaua kwa panga zao, watawaua wana wao na binti zao na kuzichoma nyumba zao.

4823:48 Eze 22:15; Kum 13:11; 2Pet 2:6“Hivyo nitaukomesha uasherati katika nchi, ili wanawake wote wapate onyo nao wasije wakafanya uasherati kama ninyi mlivyofanya. 4923:49 Isa 9:10; Eze 16:58; 24:13; 20:38Utapata adhabu kwa ajili ya uasherati wako na kuchukua matokeo ya dhambi zako za uasherati. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.”

Bibelen på hverdagsdansk

Ezekiels Bog 23:1-49

Billedtale om Samarias og Jerusalems utroskab

1Herren sagde til mig: 2-3„Du menneske, der var engang to søstre, der fra deres tidligste ungdom levede som prostituerede i Egypten. Dér krammede og knugede man deres jomfruelige bryster. 4Storesøsteren hed Ohola og lillesøsteren Oholiba. De symboliserer Samaria og Jerusalem.23,4 De to navne, der betyder „hendes telt” og „mit telt er i hende”, hentyder til, at Jerusalem havde Herrens helligdom/telt, mens Samaria havde sin egen helligdom. Hovedstæderne står symbolsk for Nordriget og Sydriget.

Jeg giftede mig med dem begge, og de fødte mig sønner og døtre. 5Men Ohola var mig utro og blev forgabt i assyrerne, 6for deres officerer og stormænd var utrolig flotte med purpurfarvede klæder og prægtige heste. 7Hun horede med Assyriens fornemste mænd og dyrkede uhæmmet deres afguder. 8Allerede da hun var i Egypten, var hun utro imod mig og gav sig hen til afguderne der. Desværre holdt hun fast ved sin utroskab, selv efter at hun havde forladt Egypten.

9Derfor lagde jeg hendes skæbne i assyrernes hænder. Hendes elskere kunne nu gøre med hende, hvad de ville. 10Som straf ydmygede de hende ved at rive tøjet af hende og gøre hendes børn til slaver. Derpå blev hun slået ned med sværdet, og de andre kvinder hånede hende for den skændsel, hun blev udsat for.

11Men selv om hendes søster Oholiba så, hvad der skete med hende, tog hun ikke ved lære. Hendes afgudsliderlighed var forfærdelig, og hun syndede endnu mere end søsteren. 12Hun flirtede med de assyriske officerer og stormænd, der havde så flotte uniformer og prægtige heste. 13Hun var lige så troløs som sin søster, 14-15ja, hun var faktisk værre end søsteren, for hun forelskede sig endog i de babyloniske officerer, hun havde set malerier af på murene med røde uniformer, bælte om livet og turban på hovedet. 16Hun blev så forelsket i dem, at hun sendte bud til Babylon om, at de skulle komme til hende. 17De kom så og horede med hende, men bagefter følte hun afsky for dem.

18Fordi hun blottede sig for dem og gav sig selv hen til dem, blev jeg led ved hende, som jeg var blevet led ved hendes storesøster. 19-20Men det generede hende ikke. Hun huskede sin fortid som prostitueret i Egypten og gav sig nu hen til de liderlige egyptere, der var brunstige som æsler og gejle som hingste. 21Hun gik tilbage til sin ungdoms lyster, dengang man krammede hendes bryster i Egypten.

22Men hør nu Herrens ord, Oholiba: Alle dine elskere, som du vendte dig fra i afsky, hidser jeg op imod dig. 23Babylonierne kommer imod dig sammen med alle kaldæerne fra Pekod, Shoa og Koa. Også assyrerne sender jeg mod dig, alle de flotte officerer og stormænd, klædt i purpur og ridende på prægtige heste. 24Fra nord kommer stridsvogne og forsyningsvogne rumlende imod dig, og deres fodfolk kommer vrimlende fra alle kanter, bevæbnet til tænderne. Fjenden omringer dig fra alle sider, og jeg overlader det til dem at udføre straffen over dig. 25I jalousi vil jeg hævne mig på dig. Jeg lader dem skære næsen og ørerne af dig og bortføre dine børn som slaver. De, der overlever, vil falde for sværdet eller brændes i ilden. 26De vil flå tøjet af dig og rive dine juveler til sig. 27Sådan vil jeg gøre en ende på dine uhæmmede lidenskaber, den skamløse livsstil du tog med dig fra Egypten. Du skal ikke mere tilbede falske guder eller tænke på Egypten. 28Jeg giver dig i dine fjenders vold, dem du afskyr og har taget afstand fra. 29I deres raseri vil de frarøve dig alt, hvad du har, og slænge dig bort, nøgen og forladt, så din skandaløse livsstil afsløres. 30Al den elendighed er du selv skyld i, fordi du dyrkede fremmede folkeslags guder og gjorde dig selv uren ved at tilbede deres afgudsbilleder. 31Du fulgte i din søsters fodspor, og derfor skal du få en straf, der svarer til hendes. 32Det er en hård straf, og du bliver genstand for alverdens hån. Du må tømme straffens fyldte bæger til bunds. 33Du vil blive fuldstændig omtåget og stønne af gru og rædsel. 34Men du skal tømme det til sidste dråbe og derefter smadre det i tusind stykker og rive dig selv til blods i fortvivlelse. Jeg, Herren, har talt. 35Fordi du glemte mig og vendte mig ryggen, må du tage konsekvensen af din forfærdelige utroskab.”

36Herren fortsatte: „Du menneske, udtal min dom over Ohola og Oholiba. Fortæl om deres frygtelige synder. 37De var mig utro og har blod på hænderne, for de dyrkede afguderne og myrdede de børn, som de fødte mig, ved at brænde dem på afgudsaltrene. 38Desuden vanærede de mit tempel og overholdt ikke sabbatsbudet. 39Tænk, lige efter at have slagtet og brændt deres børn til ære for afguderne kom de til mit tempel for at tilbede mig! Hvilken afskyelig handlemåde!

40I to søstre sendte bud til fjerne lande efter flotte mænd. I badede jer, lagde sminke på øjnene og tog jeres fineste smykker på. 41I satte jer til bords på elegante puder og stillede min hellige røgelse og olie frem på bordet. 42Der var fest og ballade. De mange indbudte mænd fra ørkenen drak sig fulde og satte armringe på jeres arme og en fornem krone på jeres hoved. 43Jeg sagde til mig selv: De utro gamle skøger! 44Derpå gik mændene ind til Ohola og Oholiba som til prostituerede. Åh, de skamløse kvinder. 45Men retskafne mænd skal efter lovens ord idømme dem straffen for ægteskabsbrud og mord, for de har været utro imod mig, og de har blod på hænderne.

46Gud Herren siger: Før en hær imod dem, så de bliver terroriseret og udplyndret. 47Lad fjenden kaste sten imod dem og hugge dem ned med sværdet, slagte deres børn og brænde deres huse ned til grunden. 48For jeg vil sætte en stopper for den afgudsliderlighed, der hersker i landet. I skal være et eksempel til skræk og advarsel for andre til alle tider. 49I vil blive straffet hårdt for jeres uanstændige afguderi, og I skal forstå, at jeg er Herren.”