Ezekieli 18 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 18:1-32

Roho Itendayo Dhambi Itakufa

1Neno la Bwana likanijia kusema: 218:2 Isa 3:15; Mao 5:7; Ay 21:19; Yer 31:29“Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli:

“ ‘Baba wamekula zabibu zenye chachu,

nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?

318:3 Za 49:4“Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli. 418:4 Mwa 18:32; Rum 6:23; Ebr 12:9; 2Fal 14:6; Mit 13:21; Kut 17:14; Ay 21:20; Isa 42:5; Eze 33:8Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.

5“Mtu aweza kuwa ni mwenye haki

atendaye yaliyo haki na sawa.

618:6 Eze 6:2; 22:9; Kum 4:19; Amo 5:26; Ebr 13:4; Eze 6:13; Law 15:24Hakula katika mahali pa ibada za miungu

kwenye milima

wala hakuziinulia macho sanamu

za nyumba ya Israeli.

Hakumtia unajisi mke wa jirani yake,

wala hakukutana kimwili na mwanamke

wakati wa siku zake za hedhi.

718:7 Yak 5:4; Kut 22:26; Kum 24:12; 24:12; 15:11; Lk 3:11; Kut 20:15; Ay 22:7Hamwonei mtu yeyote,

bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake.

Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake

na huwapa nguo walio uchi.

818:8 Zek 8:16; Kut 18:21; Kum 23:19-20; Yer 22:3; Kut 22:25; Law 25:35-37Hakopeshi kwa riba

wala hajipatii faida ya ziada.

Huuzuia mkono wake usifanye mabaya,

naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.

918:9 Hab 2:4; Law 18:5; Amo 5:4; Law 19:37; Eze 11:12; 20:11Huzifuata amri zangu

na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu.

Huyo mtu ni mwenye haki;

hakika ataishi,

asema Bwana Mwenyezi.

1018:10 Kut 21:12; Eze 22:6“Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya 1118:11 Kut 22:22; Ay 24:9; Isa 54:9; 59:6-7; Hab 2:6; Kut 22:17; Eze 16:49(ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya):

“Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima.

Humtia unajisi mke wa jirani yake.

1218:12 Kut 22:22; 22:27; Ay 24:9; Amo 4:1; 2Fal 21:11Huwaonea maskini na wahitaji.

Hunyangʼanyana.

Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake.

Huziinulia sanamu macho.

Hufanya mambo ya machukizo.

1318:13 Kut 22:25; Law 20:9; Hos 12:14; Eze 33:4-5Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada.

Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.

1418:14 2Nya 34:21; Mit 23:24“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:

1518:15 Eze 22:9; Za 24:4“Hakula katika mahali pa ibada za miungu

kwenye milima,

wala hainulii macho sanamu

za nyumba ya Israeli.

Hakumtia unajisi

mke wa jirani yake.

1618:16 Kut 22:27; Ay 22:7; Mit 22:9; Za 41:1; Eze 16:49; Isa 7:10Hakumwonea mtu yeyote

wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo.

Hanyangʼanyi,

bali huwapa wenye njaa chakula chake

na huwapa nguo walio uchi.

1718:17 Za 1:2Huuzuia mkono wake usitende dhambi,

hakopeshi kwa riba

wala hajipatii faida ya ziada.

Huzishika amri zangu

na kuzifuata sheria zangu.

Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi. 1818:18 Eze 3:18Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.

1918:19 Kut 20:5; Kum 5:9; Yer 15:4; Zek 1:3-6“Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi. 2018:20 Kum 24:16; Rum 2:9; Isa 3:10; Hes 15:31; 1Fal 8:32; 2Fal 14:6; Eze 7:27; Mt 16:27Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.

2118:21 Eze 13:22; 33:12-19; Yer 18:8; Mwa 26:5“Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa. 2218:22 Dan 4:27; Mik 7:19; Mit 18:20-24; Isa 43:25Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi. 2318:23 Mao 3:33; 2Pet 3:9; 1Tim 2:4; Za 147:11; Ay 37:23; Eze 16:6; Mik 7:18Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?

2418:24 Ay 35:8; 2Pet 2:20-22; Ebr 10:38; Yer 34:6; Eze 15:8; 1Sam 15:11; 2Nya 24:17-20“Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.

2518:25 Sef 3:5; Mal 3:1-17; Mwa 18:25; Yer 2:29; Eze 33:17; Mal 2:17“Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki? 2618:26 Eze 18:24Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa. 2718:27 Isa 1:18; Eze 13:22Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake. 2818:28 Eze 18:14; Isa 55:7Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa. 29Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”

3018:30 Yer 35:15; Eze 7:13; Mt 3:2; Hos 12:6; 1Pet 1:17; Isa 27“Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu. 3118:31 Za 51:10; Isa 1:16-17; Eze 36:26; Efe 4:22; Amu 6:8; Yer 27:13; Eze 11:19Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli? 3218:32 2Nya 7:14; Ay 37:23; Eze 33:11; Ay 22:23; Isa 55:7; Mal 3:7; Eze 16:6Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以西結書 18:1-32

犯罪者必滅亡

1耶和華對我說: 2「你們以色列人為什麼說『父親吃了酸葡萄,兒子的牙酸倒了』這句俗語呢? 3主耶和華說,我憑我的永恆起誓,你們在以色列必不再用這句話。 4因為所有的生命都屬於我,父和子都屬於我。誰犯罪,誰死亡。

5「倘若有義人秉公行義, 6不在山上的廟宇裡吃祭物,不拜以色列的偶像,不玷污別人的妻子,不親近經期中的婦女; 7不欺壓人,反而退還債戶的抵押品;不搶奪財物,反而給饑餓的人食物吃,給赤身露體的人衣服穿; 8不放債取利,不犯罪作惡,反而公平待人, 9遵守我的律例,順從我的典章——這樣的義人必能活著。這是主耶和華說的。

10「倘若這人生了一個不肖子,兇殘暴戾,殺人搶劫,無惡不作, 11常在廟宇吃祭偶像之物,玷污別人的妻子, 12欺壓貧窮困苦的人,搶奪財物,扣留債戶的抵押品,祭拜偶像,犯罪作惡, 13放債取利,這樣的人還能活著嗎?他必不能活。他作惡多端,必自取滅亡,抵償自己的血債。

14「倘若這不肖子有一個好兒子,他看見父親的所作所為,不願步父親的後塵。 15他不肯在山上吃祭偶像之物,不拜以色列人的偶像,不玷污別人的妻子, 16不欺壓他人,不扣留抵押品,不搶奪財物,反而給饑餓的人食物吃,給赤身露體的人衣服穿, 17不壓榨貧窮的人,不放債取利,反而遵守我的典章,順從我的律例,這人必不因父親的罪惡而死亡,他必活著。 18他父親因肆意欺詐,掠奪同胞,多行不義,必自招滅亡。

19「你們會問,『兒子為什麼不用承擔父親的罪惡呢?』這是因為兒子秉公行義,謹遵我的律例,所以他必活著。 20誰犯罪,誰死亡,兒子不用承擔父親的罪惡,父親也不用承擔兒子的罪惡。義人必有善報,惡人必有惡報。

21「惡人若肯痛改前非,遵守我的律例,秉公行義,就必活著,不致死亡。 22我必不追究他以前所犯的一切罪行,他必因行事正直而活著。 23主耶和華說,我難道喜歡惡人死亡嗎?我豈不是更願他們痛改前非並活著嗎? 24義人若棄善行惡,與惡人同流合污,這人豈能活著?他從前的義行不會被記念,他必因自己的背信和罪惡而滅亡。

25「你們說,主這樣做不公平。以色列人啊,你們聽著,是我的做法不公平呢?還是你們的做法不公平呢? 26倘若義人離義行惡,他必因犯罪而死。 27倘若惡人離惡行義,他必救回自己的性命。 28因為他醒悟過來,痛改前非,必能活著,不致死亡。 29以色列人卻說,『主這樣做不公平!』以色列人啊,是我的做法不公平呢?還是你們的做法不公平呢?

30「所以主耶和華說,『以色列人啊,我必按你們各人的行為審判你們。你們要悔改,痛改前非,使你們不致死在罪惡中。 31你們要離棄從前所有的罪惡,洗心革面。以色列人啊!你們何必走向滅亡呢?』 32主耶和華說,『我斷不喜歡任何人死亡,你們要悔改,以便存活。』」