Ezekieli 17 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 17:1-24

Tai Wawili Na Mizabibu

117:1 Amu 14:12; Eze 20:49Neno la Bwana likanijia kusema: 217:2 Amu 14:12; Eze 20:49“Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo. 317:3 Kum 28:49; Dan 7:4; Yer 22:23; 49:22; Hos 8:1Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi, 417:4 Isa 10:33akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.

517:5 Kum 8:7-9; Isa 15:7; Eze 31:5; Isa 44:5“ ‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi, 617:6 Isa 18:5; Ay 5:3nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.

717:7 Eze 31:4“ ‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji. 817:8 Ay 18:19; Mal 4:1Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’

917:9 Yer 42:10; Amo 2:9“Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake. 1017:10 Ay 1:19; Hos 12:1; Yud 12; Eze 15:4; Hos 13:15Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’ ”

11Ndipo neno la Bwana likanijia kusema: 1217:12 Eze 12:9; 2Fal 24:15; Kum 21:10; 2Nya 36:10; Eze 24:19“Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli. 1317:13 2Nya 36:13; 2Fal 24:17; Kut 23:32; Isa 3:2Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi, 1417:14 Eze 29:14ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake. 1517:15 Yer 52:3; Kum 17:16; Isa 30:2; Za 56:7; Kum 17:16; Yer 34:3; Eze 29:16Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?

1617:16 Yer 52:11; Eze 12:13; Yer 32:5; 2Fal 24:17“ ‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake. 1717:17 Yer 37:7; Eze 4:2; Isa 36:6; Mao 4:17; Eze 29:6-7Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi. 1817:18 2Fal 10:15; 1Nya 29:24Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.

1917:19 Yer 7:9; Hos 10:4; Eze 16:59; 21:23“ ‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja. 2017:20 Yos 10:16-18; Mhu 9:12; Eze 12:13; 32:3; 20:36; 15:8; Yer 2:35Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu. 2117:21 Eze 12:14; 2Fal 25:11; Law 26:33; Zek 2:5-6; 2Fal 25:5Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.

Hatimaye Israeli Kutukuzwa

2217:22 Isa 2:2; 53:2; Yer 23:5; 2Fal 19:30; Isa 4:2; Eze 20:40; 40:2; 43:12“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana. 2317:23 Dan 4:12; Mt 13:32; Mik 4:1; Yer 31:12; Isa 27:6; 2:2; Za 92:12; Hos 14:5-7Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake. 2417:24 Za 96:12; Isa 2:13; Eze 19:12; 21:26; 22:14; Amo 9:11; Za 52:5; Hes 17:8; Dan 5:21; 1Sam 2:7-8; Eze 37:13Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi.

“ ‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 17:1-24

鹰和葡萄树的比喻

1耶和华对我说: 2“人子啊,你要向以色列人出谜语,讲比喻, 3告诉他们,主耶和华说,‘有一只大鹰翅膀宽大,羽毛丰满,色彩缤纷。这只鹰飞到黎巴嫩的香柏树上,折去树梢, 4叼到一个商贾云集的城市,栽在那里。 5它又把以色列的树苗像柳树一样栽在水源丰沛的沃土里。 6树苗很快发了芽,成了向四面蔓延的矮小葡萄树,根深叶茂,枝子向着鹰伸展开去。

7“‘又有一只大鹰飞来,翅膀宽大,羽毛丰满。这葡萄树把根和枝子转向这只鹰,渴望得到它的浇灌。 8但这树已栽在水源丰沛的沃土里,可以长得枝繁叶茂,成为结实累累的好葡萄树。’

9“你要告诉他们,主耶和华这样说,‘这树能长得枝繁叶茂吗?难道那鹰不把它连根拔起,摘掉它的果子,使树和嫩叶全部枯萎吗?不必费多大力气,也不需要多少人就可以把它连根拔起。 10这树虽然被栽种了,又岂能长得茂盛呢?东风一吹,它岂不完全枯萎在园圃中了吗?’”

11耶和华对我说: 12“你要对这些悖逆的人说,‘你们不明白这比喻的意思吗?’要告诉他们,巴比伦王攻取了耶路撒冷,把其中的君王和大臣掳到巴比伦13并从犹大王室中选出一人与他立约,要他效忠。巴比伦王掳去犹大国的重臣, 14使犹大国臣服于他,无法图强,只能遵守盟约,以求生存。 15后来,犹大王背叛了巴比伦王,派使者到埃及请求支援军队马匹。他能成功吗?他这样做怎能逃脱惩罚呢?他这样背约怎能逃脱惩罚呢?

16“我凭我的永恒起誓,巴比伦王立他做王,他却弃约背誓,他必死在巴比伦17敌人筑起围攻的土垒和高台大肆杀戮的时候,法老虽然兵强马壮,人多势众,仍无法帮他抗敌。 18他起誓降服,却弃约背誓,所以绝不能逃避后果。 19因此,主耶和华说,‘我凭我的永恒起誓,他既藐视与我所立的誓言,背弃与我所定的约,我必惩罚他。 20我要撒开网罗抓住他,把他带到巴比伦,审判他对我不忠的罪。 21他所有的精兵都要丧身刀下,余下的也要四散逃窜。这样,你们就知道这是我耶和华说的。

22“主耶和华说,‘我要从高大的香柏树梢折下一根嫩枝,种植在以色列巍峨的高山上。 23它会生枝结果,成为一棵美丽的香柏树,各类飞鸟都要栖息在它的树枝上。 24田野所有的树都会知道我耶和华使高树倒下、矮树长高、青树枯萎、枯树发荣。我耶和华言出必行。’”