Ezekieli 15 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 15:1-8

Yerusalemu Mzabibu Usiofaa

1Neno la Bwana likanijia kusema: 215:2 Za 80:8-16; Yn 15:2; Yer 2:21; Isa 27:2-6; 5:1-7; Hos 10:1“Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu? 315:3 Yer 13:10; Isa 22:23Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake? 415:4 Eze 17:3-10; Yn 15:6; Eze 19:14Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote? 5Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?

6“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu. 715:7 Yer 21:10; Law 26:17; Za 34:16; Isa 24:18; Amo 9:1-4; Eze 14:8; 5:2-4Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana. 815:8 Eze 14:13; 17:20; Amo 5:19; Eze 18:24Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”

Korean Living Bible

에스겔 15:1-8

포도나무 가지에 대한 비유

1여호와께서 나에게 말씀하셨다.

2“사람의 아들아, 포도나무를 어떻 게 다른 나무에 비할 수 있겠느냐? 포도나무 가지를 숲속의 나무에 비교할 때 나은 것이 무엇이냐?

3포도나무 가지에서 무슨 쓸모있는 나무가 나오겠느냐? 그것을 가지고 물건을 걸어 둘 못이라도 만들 수 있겠느냐?

4그것은 불에 던질 땔감밖에 되지 않는다. 불이 그 두 끝을 사르고 그 가운데를 새까맣게 태우면 그것을 어디에 쓰겠느냐?

5그것이 타기 전에도 아무 쓸모가 없는데 그것이 불에 타서 새까맣게 된 다음에야 무슨 쓸모가 있겠느냐?

6“그러므로 나 주 여호와가 말한다. 내가 숲속의 나무 중에서 포도나무를 땔감으로 불에 던진 것처럼 예루살렘에 사는 사람들도 불에 던질 것이다.

7내가 그들을 대적할 것이니 그들이 불에서 나와도 불이 그들을 삼킬 것이다. 내가 그들을 벌할 때에 너희가 나를 여호와인 줄 알 것이다.

8그들이 나에게 신실하지 못하였으므로 내가 그 땅을 황폐하게 하겠다. 이것은 나 주 여호와의 말이다.”