Ezekieli 13 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 13:1-23

Manabii Wa Uongo Walaumiwa

1Neno la Bwana likanijia kusema: 213:2 Yer 23:16; 37:19; 14:14; Isa 9:15; Yer 28:15; Eze 22:28“Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana! 313:3 Mao 2:14; Hos 9:7; Yer 23:25-32Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote! 413:4 Mik 3:5; Wim 2:15; 2Kor 11:13Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu. 513:5 Isa 58:12; Eze 22:30; 7:19; 30:3Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana. 613:6 Yer 28:15; 29:9; 23:16; 14:14; Eze 12:24-25; 22:28Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa. 713:7 Yer 30:10Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?

813:8 Yer 21:13“ ‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi. 913:9 Kum 32:32; Yer 17:13; Kut 6:2; Ebr 12:23; Yer 20:3-6; Eze 20:38Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.

1013:10 2Tim 3:13; Yer 50:6; 23:13; Eze 7:25; 22:28; Yer 4:10“ ‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa, 1113:11 Eze 38:22; Za 11:6; Yos 10:11; Ay 38:23kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake. 12Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”

1313:13 Yos 10:11; Ufu 11:19; Kut 9:25; Ay 38:23; Ufu 16:21; Isa 30:30“ ‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza. 1413:14 Mik 1:6; Yer 6:15; Eze 14:8; Isa 22:5Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana. 15Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa, 1613:16 Isa 57:21; Yer 6:14; 8:11; Eze 7:25wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.” ’

1713:17 Kut 15:20; Ufu 2:20; Isa 3:16; Eze 4:7; 25:2; 28:21“Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao 1813:18 2Pet 2:14na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu? 1913:19 Yer 44:26; Eze 22:26; 20:39; Mit 28:21; Mik 3:11; Rum 14:15Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.

2013:20 Za 124:7“ ‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege. 2113:21 Za 91:3Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. 2213:22 Yer 23:14; Eze 18:21; Mit 19:27; Isa 9:21; Eze 33:14-16Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao, 2313:23 Eze 12:24; Mik 3:6; Eze 14:8; Neh 6:12; Za 72:14kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以西結書 13:1-23

斥責假先知

1耶和華對我說: 2「人子啊,你要說預言斥責以色列那些說預言的先知,告訴那些私自發預言的人,『你們要聽耶和華的話。 3主耶和華說,愚頑的先知有禍了!他們沒有看到異象,卻私自發預言。 4以色列人啊,你們的先知像廢墟中的狐狸, 5沒有上去堵住缺口,也沒有重建以色列的圍牆,使以色列在耶和華的日子來臨時的爭戰中堅立。 6他們的異象虛假不實,他們的預言謊話連篇。他們口口聲聲說是傳達耶和華的話,其實耶和華並沒有差遣他們。他們竟然指望自己的謊言能夠應驗。 7難道你們不是見了虛假的異象,說了虛謊的預言嗎?你們說這是耶和華說的,其實我並沒有說。』」

8所以主耶和華說:「因為你們的假異象和謊言,我要攻擊你們。這是主耶和華說的。 9我必動手攻擊那些見假異象、說假預言的先知。他們必從我的子民當中被剔除,不被收錄在以色列人的名冊上,也不能進入以色列的土地。這樣,你們就知道我是主耶和華。 10因為他們欺騙我的子民說,『平安!』其實並沒有平安,就像有人築了一道薄牆,用白灰加以粉飾。 11所以,你要警告那些粉刷白灰的人,說,『牆必倒塌,暴雨要來臨,冰雹勢必降下,狂風也必大作。』 12牆倒塌之後,一定會有人問,『你們粉飾的白灰在哪裡呢?』 13主耶和華說,『我必在烈怒中用狂風暴雨和冰雹來摧毀這牆, 14我必把你們粉飾的牆夷為平地,使其露出根基。牆倒塌的時候,你們必葬身其中。這樣,你們就知道我是耶和華。 15我要向這牆和粉飾這牆的人發怒,懲罰他們。我告訴你們,這牆完了!粉飾這牆的人也完了!』 16他們就是那些向耶路撒冷說假預言,在沒有平安的時候宣稱看到了平安異象的以色列先知。這是主耶和華說的。」

17「人子啊,你要說預言斥責你同胞中私自發預言的女子, 18告訴她們主耶和華這樣說,『你們這些婦女有禍了!你們為了獵取人命,給人縫製戴在手腕上的符咒和各種尺寸的頭巾。你們獵取我子民的性命,還想保住自己的性命嗎? 19你們為了幾把大麥和幾塊餅,在我的子民中褻瀆我,向那些肯聽謊言的說謊,殺死那些不該死的,救活那些不該活的。』

20「所以主耶和華說,『你們用符咒獵取人命如同捕鳥,我要除去你們的符咒,從你們手臂上扯掉它們,釋放你們所獵取的人。 21我還要撕去你們的頭巾,把我的子民從你們手中拯救出來,使他們不再做你們手中的獵物。這樣,你們就知道我是耶和華。 22我沒有使義人憂傷,你們卻以謊言叫他們灰心。你們慫恿惡人不要改邪歸正,以致他們喪命。 23因此,你們必不再見假異象,也不再占卜。我必從你們手中拯救我的子民。這樣,你們就知道我是耶和華。』」