Ezekieli 10 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 10:1-22

Utukufu Unaondoka Hekaluni

110:1 Kut 23:10; Eze 1:22; Ufu 4:2-3; Mwa 3:24Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. 210:2 Eze 1:15; 9:2; Ufu 8:5; 2Sam 22:9Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.

3Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani. 410:4 Kut 24:16; Eze 44:4; 1:28Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana. 510:5 Ay 40:9; Eze 1:24; 3:15Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi10:5 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). wakati anapoongea.

610:6 Dan 7:9Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu. 710:7 Eze 5:4Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje. 810:8 Eze 1:8(Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)

910:9 Kut 28:20; Eze 1:15-21; 24:6Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi. 10Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine. 1110:11 Eze 1:17Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda. 1210:12 Ufu 4:6-8; Eze 1:15-21; 24:6Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne. 13Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.” 1410:14 1Fal 7:36; Eze 41:19; Dan 9:21; Ufu 4:7Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.

1510:15 Isa 6:2; Eze 1:3-5; Za 137:1Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari. 1610:16 Eze 1:19Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao. 1710:17 Eze 1:20-21; 3:13Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.

1810:18 Za 78:60; 18:10; Eze 7:20-22; 1Sam 4:21Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi. 1910:19 Eze 11:1-22; 43:4Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.

2010:20 Eze 1:1-8Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi. 2110:21 Eze 1:6, 8Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu. 2210:22 Eze 1:10, 12Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.

Bibelen på hverdagsdansk

Ezekiels Bog 10:1-22

Herrens herlighed forlader templet

1Derefter så jeg i mit syn noget, der lignede en trone af safir, som stod på den lysende hvælving over kerubernes hoveder. 2Jeg hørte Herren sige til manden, der var klædt i linned: „Gå ind mellem hjulene under keruberne og tag en håndfuld af de glødende kul og strø dem ud over byen.”

3Da manden fik besked på at gå hen til keruberne, stod de ved templets sydside, og den strålende sky af Herrens herlighed fyldte den indre forgård. 4Herrens stråleglans havde løftet sig fra keruberne og flyttet sig hen over templets indgang, så hele templet fyldtes af skyen, og hele forgården fyldtes af skæret fra Herrens herlighed. 5Lyden af kerubernes vingeslag kunne høres helt ud i den ydre forgård, og det lød, som når Gud, den Almægtige, taler.

6Da Herren befalede manden at gå ind mellem hjulene under keruberne og tage en håndfuld glødende kul, gik han hen og stillede sig ved et af hjulene. 7Derefter rakte en af keruberne hånden ud, tog nogle af de glødende kul fra ilden og gav dem til ham. Han tog imod kullene og gik tilbage, hvor han kom fra.

8Under kerubernes vinger var der nemlig noget, der lignede menneskehænder. 9Under hver af de fire keruber var der et hjul, der funklede som ædelsten. 10Alle hjulene var ens og inden i hvert hjul sad der et andet hjul på tværs. 11Keruberne og hjulene kunne bevæge sig i alle fire retninger uden at vende sig. De fulgte efter den ledende kerub uden at vende sig. 12Kerubernes krop, ryg, hænder og vinger var fulde af øjne, og det samme gjaldt hjulene. 13Jeg hørte, at hjulene blev kaldt „hvirvelhjul”.

14Hver af keruberne havde fire ansigter: et kerubansigt, et menneskeansigt, et løveansigt og et ørneansigt.

15Derpå bevægede de sig op i luften. De var ligesom de levende væsener, jeg tidligere havde set ved Kebarfloden. 16Når keruberne flyttede sig, gjorde hjulene det også. Når keruberne hævede sig i vejret, fulgte hjulene med dem og blev hos dem, mens de fløj. 17Hvor som helst de bevægede sig hen, fulgte hjulene med, for deres ånd var i hjulene.

18Derefter flyttede Herrens herlighed sig fra templets indgang til tronen over keruberne, 19og jeg så keruberne sprede vingerne ud og løfte sig fra jorden sammen med hjulene. De fløj væk fra templet, men gjorde ophold ved den østlige port, og Israels Guds herlighed hvilede hele tiden over dem.

20Jeg var klar over, at disse keruber var de samme som de levende væsener, jeg tidligere havde set under Israels Guds trone ved Kebarfloden. 21Hver af dem havde fire ansigter og fire vinger, og under deres vinger var der noget, som lignede menneskehænder. 22Deres ansigter var som dem, jeg havde set ved Kebarfloden, og de bevægede sig også på samme måde.