Ezekieli 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 1:1-28

Viumbe Hai Na Utukufu Wa Bwana

11:1 Kum 21:10; Mt 3:16; Eze 11:24-25; Mdo 7:56; Kut 24:10Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.

21:2 2Fal 24:15; 24:15; 24:12Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini, 31:3 2Fal 3:15; Isa 8:11; 2Pet 1:21; Eze 24:24; 3:14, 22; 33:22neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.

41:4 Yer 1:14; 23:19; Eze 8:2; Ay 38:1Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto. 51:5 Isa 6:2; Ufu 4:6; Dan 7:13Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu, 61:6 Eze 10:14lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne. 71:7 Dan 10:6; Ufu 1:15; Eze 40:3Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa. 81:8 Eze 10:8; 10:18, 21Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa, 91:9 Eze 10:22; 10:11; 1:11nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.

101:10 Eze 10:4; Ufu 4:7; Hes 2:10Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai. 111:11 Isa 6:2Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake. 121:12 Eze 10:16-19; 10:22Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka. 131:13 Ufu 4:5; Mt 28:3; 2Sam 22:9Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi. 141:14 Zek 4:10; Za 29:7; Amu 13:20Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.

151:15 Eze 3:13; 10:2; Dan 7:9Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne. 161:16 Dan 10:6; Kut 28:20Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake. 171:17 Eze 1:12; 1:19Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda. 181:18 Mit 15:3; Eze 10:12; Ufu 4:6Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.

191:19 Eze 1:16, 17Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka. 201:20 Eze 1:12; 10:17Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu. 211:21 Eze 10:9, 12, 17Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.

221:22 Eze 10:1, 5Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha. 23Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake. 241:24 2Fal 7:6; Ufu 14:2; Dan 10:6; Za 18:13; 46:3; Eze 10:5; 43:2; Ufu 19:6Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi,1:24 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.

25Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa. 261:26 Kut 24:10; Eze 10:1; Ufu 1:13; Isa 6:1; 1Fal 22:19; Yer 3:17Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu. 271:27 Eze 8:2Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka. 281:28 Mwa 9:13; Ufu 10:1; 4:2; 1:17; Hes 12:8; Kut 24:16; Dan 8:17; Hes 14:5; Lk 2:9; Kut 16:7Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka.

Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

King James Version

Ezekiel 1:1-28

1Now it came to pass in the thirtieth year, in the fourth month, in the fifth day of the month, as I was among the captives by the river of Chebar, that the heavens were opened, and I saw visions of God.1.1 captives: Heb. captivity 2In the fifth day of the month, which was the fifth year of king Jehoiachin’s captivity, 3The word of the LORD came expressly unto Ezekiel the priest, the son of Buzi, in the land of the Chaldeans by the river Chebar; and the hand of the LORD was there upon him.1.3 Ezekiel: Heb. Jehezkel

4¶ And I looked, and, behold, a whirlwind came out of the north, a great cloud, and a fire infolding itself, and a brightness was about it, and out of the midst thereof as the colour of amber, out of the midst of the fire.1.4 infolding…: Heb. catching itself 5Also out of the midst thereof came the likeness of four living creatures. And this was their appearance; they had the likeness of a man. 6And every one had four faces, and every one had four wings. 7And their feet were straight feet; and the sole of their feet was like the sole of a calf’s foot: and they sparkled like the colour of burnished brass.1.7 straight…: Heb. a straight foot 8And they had the hands of a man under their wings on their four sides; and they four had their faces and their wings. 9Their wings were joined one to another; they turned not when they went; they went every one straight forward. 10As for the likeness of their faces, they four had the face of a man, and the face of a lion, on the right side: and they four had the face of an ox on the left side; they four also had the face of an eagle. 11Thus were their faces: and their wings were stretched upward; two wings of every one were joined one to another, and two covered their bodies.1.11 stretched…: or, divided above 12And they went every one straight forward: whither the spirit was to go, they went; and they turned not when they went. 13As for the likeness of the living creatures, their appearance was like burning coals of fire, and like the appearance of lamps: it went up and down among the living creatures; and the fire was bright, and out of the fire went forth lightning. 14And the living creatures ran and returned as the appearance of a flash of lightning.

15¶ Now as I beheld the living creatures, behold one wheel upon the earth by the living creatures, with his four faces. 16The appearance of the wheels and their work was like unto the colour of a beryl: and they four had one likeness: and their appearance and their work was as it were a wheel in the middle of a wheel. 17When they went, they went upon their four sides: and they turned not when they went. 18As for their rings, they were so high that they were dreadful; and their rings were full of eyes round about them four.1.18 and their rings: or, and their strakes 19And when the living creatures went, the wheels went by them: and when the living creatures were lifted up from the earth, the wheels were lifted up. 20Whithersoever the spirit was to go, they went, thither was their spirit to go; and the wheels were lifted up over against them: for the spirit of the living creature was in the wheels.1.20 of…: or, of life 21When those went, these went; and when those stood, these stood; and when those were lifted up from the earth, the wheels were lifted up over against them: for the spirit of the living creature was in the wheels.1.21 of…: or, of life 22And the likeness of the firmament upon the heads of the living creature was as the colour of the terrible crystal, stretched forth over their heads above. 23And under the firmament were their wings straight, the one toward the other: every one had two, which covered on this side, and every one had two, which covered on that side, their bodies. 24And when they went, I heard the noise of their wings, like the noise of great waters, as the voice of the Almighty, the voice of speech, as the noise of an host: when they stood, they let down their wings. 25And there was a voice from the firmament that was over their heads, when they stood, and had let down their wings.

26¶ And above the firmament that was over their heads was the likeness of a throne, as the appearance of a sapphire stone: and upon the likeness of the throne was the likeness as the appearance of a man above upon it. 27And I saw as the colour of amber, as the appearance of fire round about within it, from the appearance of his loins even upward, and from the appearance of his loins even downward, I saw as it were the appearance of fire, and it had brightness round about. 28As the appearance of the bow that is in the cloud in the day of rain, so was the appearance of the brightness round about. This was the appearance of the likeness of the glory of the LORD. And when I saw it, I fell upon my face, and I heard a voice of one that spake.