Ezekieli 1 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 1:1-28

Viumbe Hai Na Utukufu Wa Bwana

11:1 Kum 21:10; Mt 3:16; Eze 11:24-25; Mdo 7:56; Kut 24:10Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.

21:2 2Fal 24:15; 24:15; 24:12Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini, 31:3 2Fal 3:15; Isa 8:11; 2Pet 1:21; Eze 24:24; 3:14, 22; 33:22neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.

41:4 Yer 1:14; 23:19; Eze 8:2; Ay 38:1Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto. 51:5 Isa 6:2; Ufu 4:6; Dan 7:13Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu, 61:6 Eze 10:14lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne. 71:7 Dan 10:6; Ufu 1:15; Eze 40:3Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa. 81:8 Eze 10:8; 10:18, 21Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa, 91:9 Eze 10:22; 10:11; 1:11nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.

101:10 Eze 10:4; Ufu 4:7; Hes 2:10Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai. 111:11 Isa 6:2Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake. 121:12 Eze 10:16-19; 10:22Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka. 131:13 Ufu 4:5; Mt 28:3; 2Sam 22:9Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi. 141:14 Zek 4:10; Za 29:7; Amu 13:20Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.

151:15 Eze 3:13; 10:2; Dan 7:9Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne. 161:16 Dan 10:6; Kut 28:20Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake. 171:17 Eze 1:12; 1:19Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda. 181:18 Mit 15:3; Eze 10:12; Ufu 4:6Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.

191:19 Eze 1:16, 17Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka. 201:20 Eze 1:12; 10:17Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu. 211:21 Eze 10:9, 12, 17Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.

221:22 Eze 10:1, 5Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha. 23Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake. 241:24 2Fal 7:6; Ufu 14:2; Dan 10:6; Za 18:13; 46:3; Eze 10:5; 43:2; Ufu 19:6Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi,1:24 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.

25Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa. 261:26 Kut 24:10; Eze 10:1; Ufu 1:13; Isa 6:1; 1Fal 22:19; Yer 3:17Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu. 271:27 Eze 8:2Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka. 281:28 Mwa 9:13; Ufu 10:1; 4:2; 1:17; Hes 12:8; Kut 24:16; Dan 8:17; Hes 14:5; Lk 2:9; Kut 16:7Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka.

Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

Священное Писание

Езекиил 1:1-28

Видение славы Вечного

1На тридцатом году моей жизни, в пятый день четвёртого месяца, когда я жил среди пленников у реки Кевар в Вавилоне, небеса раскрылись, и мне было видение от Всевышнего. 2В тот день (шёл пятый год плена царя Иехонии)1:2 Иехония правил Иудеей всего лишь три месяца и был уведён в плен в Вавилонию в 597 г. до н. э. (см. 4 Цар. 24:8-17; 2 Лет. 36:9-10). (31 июля 593 г. до н. э.) 3слово Вечного1:3 Вечный – на языке оригинала: «Яхве». Под этим именем Всевышний открылся Мусе и народу Исраила (см. Исх. 3:13-15). См. пояснительный словарь. было ко мне, священнослужителю Езекиилу, сыну Бузи1:3 Или: «ко мне, Езекиилу, сыну священнослужителя Бузи»., у реки Кевар в стране вавилонян, и там на мне была рука Вечного.

4Я смотрел и видел смерч, который надвигался с севера: огромное облако со сверкающими молниями, окружённое сиянием. Посреди огня было нечто, подобное сияющему металлу. 5В огне были подобия четырёх живых существ. Обличием они походили на людей, 6но у каждого из них было по четыре лица и четыре крыла. 7Ноги у них были прямыми, а ступни ног походили на копыта телёнка и сверкали, как блестящая латунь. 8Под крыльями на четырёх их сторонах у них были человеческие руки. 9Все они имели лица и крылья, и крылья их соприкасались одно с другим. Каждое из них двигалось лицом вперёд; при движении они не оборачивались. 10Лица у них были такими: у каждого из четырёх спереди было человеческое лицо, с правой стороны у каждого было лицо льва, с левой стороны – лицо вола, а сзади у каждого из них было лицо орла. 11Такими были их лица. Крылья у них были простёрты вверх; у каждого существа было по две пары крыльев: одна пара касалась крыльев других существ по обеим сторонам, а другая пара закрывала тело. 12Каждое из них шло лицом вперёд. Куда бы ни шёл Дух, шли и они, не оборачиваясь на ходу. 13Облик живых существ был подобен горящим углям, подобен факелам. Огонь непрестанно перемещался посреди существ; он пламенел, и из него вырывалась молния. 14Существа быстро передвигались вперёд и назад, подобно тому, как сверкает молния.

15Я смотрел на живых существ и видел на земле возле них колёса, по одному на каждого из четырёх. 16Колёса выглядели следующим образом: они искрились, подобно хризолиту, и все четыре колеса были одинаковыми на вид. Они выглядели так, словно колесо находилось в колесе. 17Двигаясь, они могли направляться в любую из четырёх сторон, куда были обращены существа; когда существа передвигались, колёса не поворачивались. 18Их ободья были высокими и устрашающими; по всему кругу ободьев всех четырёх колёс располагались глаза.

19Когда живые существа двигались, двигались и колёса, располагавшиеся возле них; когда существа поднимались с земли, поднимались и колёса. 20Куда бы ни шёл дух, шли и они; колёса поднимались с ними, потому что дух живых существ был в колёсах. 21Когда существа двигались, они тоже двигались; когда существа стояли, они тоже стояли, а когда существа поднимались с земли, колёса поднимались вместе с ними, потому что дух живых существ был в колёсах.

22Над головами живых существ было нечто, подобное своду, оно изумительно искрилось, подобно кристаллу; и этот свод был распростёрт над их головами. 23Под сводом крылья существ были простёрты одно к другому, и каждый из них имел по два крыла, закрывавших тело. 24Когда существа двигались, я слышал шум от их крыльев, который был подобен рёву могучих вод, подобен голосу Всемогущего или боевому кличу в воинском стане. Останавливаясь, существа опускали крылья.

25И из-за свода над их головами раздавался голос; останавливаясь, они опускали крылья. 26Над сводом, который был над их головами, было нечто, подобное престолу из сапфира, а над подобием престола, сверху, восседал Некто, похожий на человека. 27Я видел, что от пояса и выше Он был похож на сияющий металл, словно бы исполненный пламени, а ниже пояса Он был похож на огонь; Его окружало сияние. 28Сияние вокруг Него было подобно радуге в облаках в дождливый день.