Esta 9 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 9:1-32

Ushindi Wa Wayahudi

19:1 Yer 29:4-7; Mit 22:22-23Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, yaani mwezi wa Adari, amri iliyoagizwa na mfalme ilikuwa itekelezwe. Siku hii adui wa Wayahudi walikuwa wametumaini kuwashinda, lakini sasa mambo yaliwageukia na Wayahudi wakawashinda wale waliokuwa wanawachukia. 29:2 Mwa 22:17; Za 35:26Wayahudi walikusanyika katika miji yao, katika majimbo ya Mfalme Ahasuero kuwashambulia wale waliokuwa wanatafuta kuwaangamiza. Hakuna yeyote aliyeweza kushindana nao, kwa sababu watu wa mataifa mengine yote waliwaogopa. 3Nao wakuu wote wa majimbo, majemadari, watawala na maafisa wa mfalme wakawasaidia Wayahudi, kwa sababu walimhofu Mordekai. 49:4 Kum 25:17-19; Ezr 4:6Mordekai alikuwa mtu mashuhuri katika jumba la mfalme; sifa zake zilienea katika majimbo yote naye alipata uwezo zaidi na zaidi.

59:5 Kum 25:17-19; Ezr 4:6Wayahudi waliwaangusha adui zao wote kwa upanga wakiwaua na kuwaangamiza, nao walifanya kile walichotaka kwa wale waliowachukia. 6Katika ngome ya Shushani Wayahudi waliua na kuangamiza wanaume 500. 7Pia waliwaua Parshendatha, Dalfoni, Aspatha, 8Poratha, Adalia, Ardatha, 9Parmashta, Arisai, Aridai na Waizatha, 109:10 Es 5:11; Mwa 14:23wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchukua nyara.

11Mfalme aliarifiwa siku iyo hiyo hesabu ya waliouawa katika ngome ya Shushani. 129:12 Es 5:6; 7:2Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wamewaua wanaume 500 na wana kumi wa Hamani ndani ya ngome ya Shushani. Wamefanyaje katika majimbo mengine ya mfalme yaliyobaki? Je, sasa haja yako ni nini? Nayo pia utapewa. Nalo ombi lako ni nini? Nalo utafanyiwa.”

13Esta akajibu, “Ikimpendeza mfalme, uwape ruhusa Wayahudi walioko Shushani warudie amri ya leo kesho pia, na wana wa Hamani kumi wanyongwe mahali pa kunyongea watu.”

149:14 Ezr 6:11Basi mfalme akaamuru kwamba hili litendeke. Amri ilitolewa huko Shushani, nao wakawanyonga wana kumi wa Hamani. 159:15 Mwa 14:23Wayahudi huko Shushani wakakusanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, nao wakawaua wanaume 300 huko Shushani, lakini hawakuchukua nyara zao.

169:16 Kum 25:19; 1Nya 4:43Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao 75,000 lakini hawakugusa nyara zao. 179:17 1Fal 3:15Hili lilitendeka siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari na siku ya kumi na nne walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.

Kusherehekea Purimu

18Wayahudi huko Shushani, hata hivyo, walikuwa wamekusanyika siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne, pia siku ya kumi na tano walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.

199:19 Ufu 11:10Ndiyo sababu Wayahudi wanaokaa vijijini na katika miji midogo huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu, siku ambayo wao hupeana zawadi mmoja kwa mwingine.

20Mordekai aliandika matukio haya, naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote walioko katika majimbo ya Mfalme Ahasuero, majimbo yaliyo mbali na karibu, 21akiwataka kila mwaka washerehekee siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ya mwezi wa Adari 229:22 Neh 8:12; Za 30:11-12kama wakati ambao Wayahudi walipata nafuu kutoka kwa adui zao na kama mwezi ambao huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha na kuomboleza kwao kuwa siku ya kusherehekea. Aliwaandikia kushika siku hizo kama siku za karamu na za furaha na kupeana zawadi za vyakula wao kwa wao na zawadi kwa maskini.

23Hivyo Wayahudi walikubali kuendeleza sherehe walizokuwa wamezianza, wakifanya lile Mordekai alilokuwa amewaandikia. 249:24 Kut 17:8-16; Law 16:8Kwa maana Hamani mwana wa Hamedatha Mwagagi, adui wa Wayahudi wote, alikuwa amepanga hila dhidi ya Wayahudi ili kuwaangamiza, na alikuwa amepiga puri (yaani kura) kwa ajili ya maangamizi na uharibifu wao. 259:25 Za 7:16; Es 7:10Lakini wakati shauri hilo baya lilipoarifiwa kwa mfalme, alitoa amri iliyoandikwa kwamba mipango mibaya ambayo Hamani ameipanga dhidi ya Wayahudi inapasa imrudie juu ya kichwa chake mwenyewe, na kwamba yeye na wanawe waangikwe mahali pa kunyongea watu. 26(Kwa hiyo siku hizi ziliitwa Purimu, kutokana na neno puri.) Kwa sababu ya kila kitu kilichoandikwa kwenye barua hii na kwa sababu ya yale waliyoyaona na yale yaliyowatokea, 27Wayahudi wakachukua na kuifanya desturi kwamba wao na wazao wao na wote ambao walijiunga nao wangefanya bila kuacha kushika siku hizi mbili kila mwaka, kwa njia ilivyoelekezwa na kwa wakati wake. 28Siku hizi zinapasa zikumbukwe na kuadhimishwa katika kila kizazi, kila jamaa na katika kila jimbo na kila jiji. Nazo siku hizi za Purimu kamwe zisikome kusherehekewa na Wayahudi, wala kumbukumbu zake zisipotee miongoni mwa wazao wake.

29Basi Malkia Esta binti Abihaili, pamoja na Mordekai, Myahudi, waliandika kwa mamlaka yote kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu. 309:30 Es 1:1Naye Mordekai akatuma barua kwa Wayahudi wote katika majimbo 127 ya ufalme wa Ahasuero, barua zenye maneno ya amani na matumaini, 319:31 Es 4:1-3ili kuimarisha siku hizi za Purimu katika majira yake yaliyowekwa, kama Mordekai, Myahudi na Malkia Esta walivyowaamuru, na walivyojiimarisha wenyewe na wazao wao kuhusu nyakati za kufunga na kuomboleza. 32Amri ya Esta ilithibitisha taratibu hizi kuhusu Purimu, nayo ikaandikwa katika kumbukumbu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以斯帖記 9:1-32

猶太人的反擊

1十二月,即亞達月十三日,是執行王諭旨的日子。那天,猶太人的仇敵原本想轄制他們,卻反而被他們轄制。 2猶太人在亞哈隨魯王的各省各城聚集起來,攻擊那些要害他們的人,無人能抵擋他們,因為各族都懼怕他們。 3各省的官員、總督、省長和為王辦事的人因懼怕末底改,就都幫助猶太人。 4因為末底改已是王宮要員,他的名聲傳遍各省,權勢日盛。 5猶太人用刀擊殺所有敵人,任意消滅恨他們的人。 6猶太人單在書珊城就殺了五百人。 7他們還殺了巴珊大他達分亞斯帕他8坡拉他亞大利雅亞利大他9帕瑪斯他亞利賽亞利代瓦耶撒他10這十人是猶太人的仇敵哈曼的兒子、哈米大他的孫子。但猶太人沒有動他們的財物。

11當天,王獲悉在書珊城被殺的人數, 12便對以斯帖王后說:「猶太人在書珊城殺了五百人,還殺了哈曼的十個兒子,在其餘各省就更不知怎樣了!現在你要什麼?必賜給你。你還有何要求?必為你成就。」 13以斯帖回答說:「王若願意,就請恩准書珊城的猶太人明天仍執行今天的諭旨,並把哈曼十個兒子的屍體吊在木架上。」 14王允准了,便在書珊城頒佈諭旨,哈曼十個兒子的屍體便被吊了起來。 15亞達月十四日,書珊城的猶太人再次聚集起來,在城中殺了三百人,但沒有動他們的財物。

16王其他各省的猶太人也都聚集起來自衛,得以脫離仇敵。他們殺了七萬五千個仇敵,但沒有動他們的財物。 17這事發生在亞達月十三日。十四日,猶太人休息,並以此日為設宴歡慶的日子。 18書珊城的猶太人在十三、十四日聚集殺敵,十五日才休息,並以此日為設宴歡慶的日子。 19因此,住在鄉村的猶太人都以亞達月十四日為設宴歡慶的節日,並互贈禮物。

普珥節

20末底改把這些事記錄下來,寫信給亞哈隨魯王國內遠近各省的猶太人, 21吩咐他們每年在亞達月十四、十五日守節期, 22設宴歡慶,互贈禮物,賙濟窮人,以紀念猶太人在此月此日得以脫離仇敵,化憂為樂,轉悲為喜。

23猶太人接受了末底改寫給他們的信,同意每年慶祝這個節日。 24因為猶太人的仇敵亞甲哈米大他的兒子哈曼曾經陰謀毀滅猶太人,曾經抽普珥,即抽籤,要殺戮、滅絕他們。 25但王知道這陰謀後,便降旨使哈曼謀害猶太人的惡計落到他自己頭上,將他及其眾子吊在木架上。 26他們借用普珥這個詞,稱這兩天為普珥節。猶太人因這信上的一切話,又因所看見、所經歷的事, 27就為自己、自己的後代和歸屬他們的人定下規矩:每年必按時守這兩天為節日,永不廢棄。 28各省各城、家家戶戶、世世代代都要紀念、遵守這節日,使猶太人永不中斷過普珥節,他們的後代也不可忘記。

29亞比孩的女兒以斯帖王后和猶太末底改以全權寫第二封信,囑咐猶太人守這普珥節, 30用和善、真誠的話寫信給亞哈隨魯王國一百二十七省的所有猶太人, 31囑咐他們照猶太末底改以斯帖王后的指示,按他們為自己及其後代所規定的,按時守普珥節,禁食哀哭。 32以斯帖的命令確定了普珥節,這命令被記載下來。