Esta 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 7:1-10

Hamani Aangikwa

17:1 Mwa 40:20-21; Mt 22:1-14Basi mfalme na Hamani wakaenda kula chakula pamoja na Malkia Esta. 27:2 Es 5:3Walipokuwa wakinywa mvinyo katika siku ya pili, mfalme akauliza tena, “Malkia Esta, ni nini haja yako? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.”

3Kisha Malkia Esta akajibu, “Kama nimepata kibali kwako, ee mfalme, tena kama inapendeza utukufu wako, nijalie maisha yangu, hii ndiyo haja yangu. Pia uokoe watu wangu, hili ndilo ombi langu. 47:4 Es 3:9Kwa kuwa mimi na watu wangu tumeuzwa kwa kuangamizwa, kuchinjwa na kuharibiwa. Kama tungalikuwa tumeuzwa tu kuwa watumwa wa kiume na wa kike, ningalinyamaza kimya, kwa sababu shida kama hii isingalitosha kumsumbua mfalme.”

5Mfalme Ahasuero akamuuliza Malkia Esta, “Ni nani huyu? Yuko wapi mtu huyu aliyethubutu kufanya jambo kama hili?”

6Esta akasema, “Mtesi na adui ni huyu mwovu Hamani.”

Hamani alifadhaika mbele ya mfalme na malkia. 77:7 Mwa 34:7; 2Fal 21:18Mfalme akainuka kwa ghadhabu, akaacha mvinyo wake, akaenda kwenye bustani ya jumba la kifalme. Lakini Hamani, akitambua kwamba mfalme ameshaamua hatima yake, alibaki nyuma kumsihi Malkia Esta aokoe maisha yake.

8Mara mfalme aliporudi kutoka bustani ya jumba la kifalme na kuja kwenye ukumbi wa karamu, Hamani alikuwa akijitupa juu ya kiti mahali ambapo Esta alikuwa akiegemea.

Mfalme akasema kwa nguvu, “Je, atamdhalilisha malkia hata huku nyumbani akiwa pamoja nami!”

Mara neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, walifunika uso wa Hamani. 97:9 Za 7:14-16; Mit 11:5-6Kisha Harbona, mmoja wa matowashi wanaomtumikia mfalme, akasema, “Mahali pa kuangika watu penye urefu wa mita ishirini na mbili pako nyumbani mwa Hamani. Alikuwa amepatengeneza kwa ajili ya Mordekai, ambaye alizungumza ili kumsaidia mfalme.”

Mfalme akasema, “Mwangikeni juu yake!” 107:10 Mwa 40:22; Mit 10:28Kwa hiyo wakamtundika Hamani mahali alipokuwa ameandaa kwa ajili ya Mordekai. Ndipo ghadhabu ya mfalme ikatulia.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以斯帖記 7:1-10

哈曼被處死

1王帶著哈曼去赴以斯帖王后的宴席。 2在這第二次宴會中,王在席間又問以斯帖:「以斯帖王后啊,你要什麼?我必賜給你。你有何要求?就是半壁江山,也必為你成就。」 3以斯帖回答說:「我若得到王的恩寵,王若願意,就請王把我的性命和我本族人的性命賜給我——這是我所求的。 4因為我和我本族的人都被賣了,我們將被剷除、殺光、滅盡。如果只是賣我們為奴為婢,我會閉口不語,因為那樣的痛苦不值得來打擾王7·4 因為那樣的痛苦不值得來打擾王」或譯「但王的損失,敵人無法補償」。。」 5亞哈隨魯王問以斯帖王后:「誰敢這樣做?他在哪裡?」 6以斯帖回答說:「敵人和仇家就是這惡人哈曼!」哈曼在王和王后面前十分驚恐。

7王大怒,離席去了御花園。哈曼見王定意要懲罰他,便留下來求以斯帖王后饒命。 8王從御花園回到席上,見哈曼伏在以斯帖所靠的榻上,便說:「他竟敢在宮中當著我的面侮辱王后嗎?」王這話一出口,便有人蒙了哈曼的臉。 9服侍王的太監哈波拿說:「哈曼為那救駕有功的末底改做了一個二十三米高的木架,如今正立在哈曼家裡。」王說:「把哈曼吊在上面!」 10於是,哈曼被吊在他為末底改預備的木架上,王的怒氣這才平息。