Danieli 9 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 9:1-27

Maombi Ya Danieli

19:1 Dan 5:31; Ezr 4:6Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli, 29:2 Yer 29:10; Zek 7:5; Yer 25:11-12; 2Nya 36:21katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini. 39:3 2Sam 13:19; Neh 1:4; 2Nya 20:3; Yer 29:12; Dan 10:12; Yon 3:6Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.

49:4 Kum 7:9, 21; 1Fal 8:23, 30Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu:

“Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake, 59:5 Isa 53:6; Mao 1:20; Za 106:6; Mao 3:42; Ezr 9:6; Yer 8:14tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako. 69:6 Yer 44:5; Yak 5:10; 2Fal 18:12; Ufu 10:7; 2Nya 36:16Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.

79:7 Ezr 9:7; Za 44:15; Kum 4:27; Amo 9:9; Eze 39:23-24; Yer 24:9; Isa 42:6“Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako. 89:8 Neh 9:33; Yer 14; 20; Eze 16:63Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako. 99:9 Kut 34:7; Hes 14:18; Neh 9:17; Yer 14:7; Za 130:4; Yer 42:12; 2Sam 24:14Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake. 109:10 2Fal 18:12; Ufu 10:7; 2Fal 17:13-15Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii. 119:11 Isa 1:4-7; Yer 8:5-10; Kum 27:15-26; Yer 2:29; 2Fal 22:16; Kum 11:26; 28:15; 2Fal 17:23Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii.

“Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako. 129:12 Isa 44:26; Yoe 2:2; Zek 1:6; 7:12; Mao 2:17; Yer 30:7; 4:23; Dan 12:1Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu. 139:13 Isa 9:13; Yer 2:30; Isa 31:1; Kum 4:29Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake. 149:14 Yer 18:8; 44:27; Neh 9:33; Yer 32:23; Mwa 18:25; 2Nya 12:6; Yer 40:3Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.

159:15 Kut 3:20; Yer 32:21; Neh 9:10“Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya. 169:16 Amu 5:11; Kut 15:17; Zek 8:2; Za 39:8; Eze 5:14; Isa 5:25Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.

179:17 Hes 6:24-26; Za 80:19“Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu. 189:18 Za 80:14; Kum 28:10; Isa 37:17; Yer 7:10-12; 25:29; Lk 18:13Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi. 199:19 Za 44:23; 1Sam 12:22Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”

Majuma Sabini

209:20 Za 145:18; Isa 58:9; Ezr 10:1Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu, 219:21 Dan 8:16; Lk 1:19; Kut 29:39wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni. 229:22 Dan 7:16; 10:14; Amu 3:7Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu. 239:23 Dan 10:19; Lk 1:24; Dan 10:11-12; Mt 24:15; Isa 65:24Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:

249:24 Isa 53:10; 56:1; Ebr 9:12; Isa 1:26“Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.

259:25 Ezr 4:24; 6:15; Yn 4:25; 1Sam 13:14; Ezr 3:3“Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu. 269:26 Isa 53:8; Mt 16:21; Isa 28:2; Nah 1:8; Dan 1:8; 11:10; Za 46:8; Zek 4:14; Hag 2:23Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa. 279:27 Isa 10:22Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”

King James Version

Daniel 9:1-27

1In the first year of Darius the son of Ahasuerus, of the seed of the Medes, which was made king over the realm of the Chaldeans;9.1 which: or, in which he 2In the first year of his reign I Daniel understood by books the number of the years, whereof the word of the LORD came to Jeremiah the prophet, that he would accomplish seventy years in the desolations of Jerusalem.

3¶ And I set my face unto the Lord God, to seek by prayer and supplications, with fasting, and sackcloth, and ashes:

4And I prayed unto the LORD my God, and made my confession, and said, O Lord, the great and dreadful God, keeping the covenant and mercy to them that love him, and to them that keep his commandments; 5We have sinned, and have committed iniquity, and have done wickedly, and have rebelled, even by departing from thy precepts and from thy judgments: 6Neither have we hearkened unto thy servants the prophets, which spake in thy name to our kings, our princes, and our fathers, and to all the people of the land. 7O Lord, righteousness belongeth unto thee, but unto us confusion of faces, as at this day; to the men of Judah, and to the inhabitants of Jerusalem, and unto all Israel, that are near, and that are far off, through all the countries whither thou hast driven them, because of their trespass that they have trespassed against thee.9.7 belongeth…: or, thou hast 8O Lord, to us belongeth confusion of face, to our kings, to our princes, and to our fathers, because we have sinned against thee. 9To the Lord our God belong mercies and forgivenesses, though we have rebelled against him; 10Neither have we obeyed the voice of the LORD our God, to walk in his laws, which he set before us by his servants the prophets. 11Yea, all Israel have transgressed thy law, even by departing, that they might not obey thy voice; therefore the curse is poured upon us, and the oath that is written in the law of Moses the servant of God, because we have sinned against him. 12And he hath confirmed his words, which he spake against us, and against our judges that judged us, by bringing upon us a great evil: for under the whole heaven hath not been done as hath been done upon Jerusalem. 13As it is written in the law of Moses, all this evil is come upon us: yet made we not our prayer before the LORD our God, that we might turn from our iniquities, and understand thy truth.9.13 made…: Heb. intreated we not the face of the, etc 14Therefore hath the LORD watched upon the evil, and brought it upon us: for the LORD our God is righteous in all his works which he doeth: for we obeyed not his voice. 15And now, O Lord our God, that hast brought thy people forth out of the land of Egypt with a mighty hand, and hast gotten thee renown, as at this day; we have sinned, we have done wickedly.9.15 gotten…: Heb. made thee a name

16¶ O Lord, according to all thy righteousness, I beseech thee, let thine anger and thy fury be turned away from thy city Jerusalem, thy holy mountain: because for our sins, and for the iniquities of our fathers, Jerusalem and thy people are become a reproach to all that are about us. 17Now therefore, O our God, hear the prayer of thy servant, and his supplications, and cause thy face to shine upon thy sanctuary that is desolate, for the Lord’s sake. 18O my God, incline thine ear, and hear; open thine eyes, and behold our desolations, and the city which is called by thy name: for we do not present our supplications before thee for our righteousnesses, but for thy great mercies.9.18 which…: Heb. whereupon thy name is called9.18 present: Heb. cause to fall 19O Lord, hear; O Lord, forgive; O Lord, hearken and do; defer not, for thine own sake, O my God: for thy city and thy people are called by thy name.

20¶ And whiles I was speaking, and praying, and confessing my sin and the sin of my people Israel, and presenting my supplication before the LORD my God for the holy mountain of my God; 21Yea, whiles I was speaking in prayer, even the man Gabriel, whom I had seen in the vision at the beginning, being caused to fly swiftly, touched me about the time of the evening oblation.9.21 swiftly: Heb. with weariness, or, flight 22And he informed me, and talked with me, and said, O Daniel, I am now come forth to give thee skill and understanding.9.22 to…: Heb. to make thee skilful of 23At the beginning of thy supplications the commandment came forth, and I am come to shew thee; for thou art greatly beloved: therefore understand the matter, and consider the vision.9.23 commandment: Heb. word9.23 greatly…: Heb. a man of desires 24Seventy weeks are determined upon thy people and upon thy holy city, to finish the transgression, and to make an end of sins, and to make reconciliation for iniquity, and to bring in everlasting righteousness, and to seal up the vision and prophecy, and to anoint the most Holy.9.24 finish: or, restrain9.24 make an…: or, seal up9.24 prophecy: Heb. prophet 25Know therefore and understand, that from the going forth of the commandment to restore and to build Jerusalem unto the Messiah the Prince shall be seven weeks, and threescore and two weeks: the street shall be built again, and the wall, even in troublous times.9.25 be built…: Heb. return and be built9.25 wall: or, breach, or, ditch9.25 troublous: Heb. strait of 26And after threescore and two weeks shall Messiah be cut off, but not for himself: and the people of the prince that shall come shall destroy the city and the sanctuary; and the end thereof shall be with a flood, and unto the end of the war desolations are determined.9.26 but…: or, and shall have nothing9.26 desolations…: or, it shall be cut off by desolations 27And he shall confirm the covenant with many for one week: and in the midst of the week he shall cause the sacrifice and the oblation to cease, and for the overspreading of abominations he shall make it desolate, even until the consummation, and that determined shall be poured upon the desolate.9.27 the covenant: or, a covenant9.27 for the…: or, with the abominable armies9.27 the desolate: or, the desolator