Danieli 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 6:1-28

Danieli Katika Tundu La Simba

16:1 Dan 5:31; Es 1:1Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote, 26:2 Dan 2:48-49; Mit 3:35; Dan 5:12-14; 1:20pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara. 36:3 Es 10:3; Mwa 41:41; Mit 3:35; Dan 5:12-14; 1:20Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote. 46:4 Yer 20:10Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe. 56:5 Mdo 24:13-16Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”

66:6 Neh 2:3; Dan 2:4Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele! 76:7 Dan 3:2; Za 59:3; 64:2-6; Dan 3:6Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba. 86:8 Es 1:19Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.” 96:9 Dan 9:23; Eze 2:1; Dan 9:23Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.

106:10 1Fal 8:29; Mdo 5:29; Za 95:6; Mt 6:6Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni. 116:11 1Fal 8:48-50; Za 55:17; 1The 5:17-18Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada. 126:12 Es 1:19; Dan 3:8-12Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?”

Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”

136:13 Eze 14:14; Dan 2:25; Es 3:8; Dan 3:12Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.” 146:14 Dan 3:13; Mk 6:26Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.

156:15 Es 8:8Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”

166:16 Ay 5:19; 2Kor 1:10; Za 97:10; 37:39-40Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”

176:17 Mt 27:66; Mao 3:536:17 Dan 4:3; 3:29Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa. 186:18 2Sam 12:17; Dan 3:10; Es 6:1; Dan 2:1Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.

19Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba. 206:20 Dan 3:17; Yer 32:17; Mwa 18:14Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”

216:21 Neh 2:3; Dan 2:4; 3:9Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele! 226:22 Dan 3:23-28; Mwa 32:1; Za 91:11-13; Ebr 11:33; Mdo 12:11; 2Tim 4:17Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”

236:23 Dan 3:27; Mk 16:18; Isa 12:2; 1Nya 5:20Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.

246:24 Kum 19:18-19; Es 7:9-10; 2Fal 14:6; Isa 38:13; Kum 24:16; 2Fal 14:6Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.

256:25 Dan 3:4; 4:1Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote:

“Ninyi na mstawi sana!

266:26 Dan 4:34; Es 8:17; Dan 2:44; Za 99:1-3; Yos 2:11; 3:10; Dan 12:7; Za 5:7; Dan 3:26; Yer 10:10; Ufu 1:18“Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli.

“Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai,

naye hudumu milele,

ufalme wake hautaangamizwa,

nao utawala wake hauna mwisho.

27Huponya na kuokoa;

hufanya ishara na maajabu

mbinguni na duniani.

Amemwokoa Danieli

kutoka nguvu za simba.”

286:28 2Nya 36:22; Dan 1:21; 5:1, 28Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

但以理書 6:1-28

但以理在獅子坑

1大流士決定設立一百二十個總督治理全國。 2總督之上,設三個總長,以維護王的統治,但以理是其中之一。 3因為但以理有非凡的心智,遠超過其他總長和總督,王便考慮讓他治理全國。 4於是,其他總長和總督想在但以理的政務中找把柄控告他,卻找不到任何把柄或過失,因為他誠實可靠,毫無過失。 5最後他們說:「除非我們從但以理上帝的律法下手,否則找不到指控他的把柄。」

6於是,這些總長和總督齊來見王,說:「願大流士王萬歲! 7所有總長、行政官、總督、謀士和省長都認為王應該下一道禁令,三十天內,任何人不得向王以外的神明或人禱告,違者必被扔進獅子坑。 8王啊,求你頒佈、簽署這道禁令,使之不可更改,正如瑪代人和波斯人的律令是不可更改的。」 9於是大流士王簽署了這道禁令。

10但以理知道王簽署禁令後,就回到家裡。他樓上的窗戶朝向耶路撒冷,他像往常一樣每日三次跪下向上帝禱告、感恩。 11那些官員一同來了,發現但以理向他的上帝禱告、祈求, 12便去見王,提及王的禁令,說:「王啊,你不是簽署禁令,三十天內,任何人不得向王以外的神明或人禱告,違者必被扔進獅子坑嗎?」王說:「確有此事,按照瑪代人和波斯人的律,這禁令不可更改。」 13他們對王說:「王啊,被擄來的猶大但以理不理會你和你的禁令,仍一日三次向他的上帝祈禱。」 14王聽了這些話,十分愁煩,一心想救但以理,直到日落都在籌畫解救之道。 15那些人齊來見王,說:「王啊,按照瑪代人和波斯人的律,王頒佈的禁令和律例是不可更改的。」

16王便下令把但以理帶來扔進獅子坑。他對但以理說:「願你忠心事奉的上帝拯救你!」 17坑口用大石封住,並加上王和大臣的封印,使懲辦但以理的事不可更改。 18王回宮後,整夜禁食,拒絕娛樂,無法入睡。

19次日黎明,王起來匆忙趕往獅子坑, 20到了坑邊,淒聲呼喊但以理:「永活上帝的僕人但以理啊,你忠心事奉的上帝有沒有救你脫離獅子的口?」 21但以理對王說:「願王萬歲! 22我的上帝差遣天使封住了獅子的口,不讓牠們傷害我,因為我在上帝面前是清白的。王啊,我在你面前也沒有過錯。」 23王非常高興,便命人把但以理從坑中拉上來。於是,但以理從坑中被拉了上來,他因為信靠他的上帝,身上毫無損傷。 24王下令把那些惡意控告但以理的人及其兒女妻子都帶來,扔進獅子坑。他們還沒到坑底,獅子便撲上去,咬碎了他們的骨頭。

25後來,大流士王傳諭境內的各族、各邦、各語種的人,說:「願你們大享平安! 26我下令,我統治的國民都要敬畏但以理的上帝,

「因為祂是永活長存的上帝,

祂的國度永不滅亡,

祂的統治直到永遠。

27祂庇護、拯救,

在天上地下行神蹟奇事,

但以理脫離獅子的口。」

28因此,在大流士波斯塞魯士執政期間,但以理凡事亨通。