Danieli 4 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 4:1-37

Ndoto Ya Nebukadneza Ya Mti

14:1 Dan 3:4; 6:25Mfalme Nebukadneza,

Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote:

Mafanikio yawe kwenu sana!

24:2 Dan 3:26; Za 74:9Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.

34:3 Za 105:27; Dan 6:25-27; 2:44Ishara zake ni kuu aje,

na maajabu yake yana nguvu aje!

Ufalme wake ni ufalme wa milele;

enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.

44:4 Za 30:6; Isa 32:9Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa. 54:5 Dan 2:1, 28; Za 4:4; Mwa 41:8; Ay 3:26; Dan 5:6; 2:3Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha. 64:6 Dan 2:2Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu. 74:7 Mwa 41:8; Isa 44:25; Dan 2:2, 10Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria. 84:8 Mwa 41:38; Dan 5:11-14; 1:7Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)

94:9 Dan 2:48; 5:11-12Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie. 104:10 Za 4:4; Eze 31:3-4Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana. 114:11 Eze 19:11; 31:5Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia. 124:12 Eze 17:23; Mt 13:32; Mao 4:20Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.

134:13 Dan 8:13; Kum 33:2; Dan 7:1“Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni. 144:14 Mt 3:10; Dan 5:20; Ay 24:20; Eze 31:2Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake. 15Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni.

“ ‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia. 16Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.

174:17 Za 83:18; Rum 13:1; Mt 23:12; Dan 11:21; Za 83:18; Yer 27:5-7; Za 103:19“ ‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’

184:18 Mwa 41:8; Dan 5:8, 15; 1:20; Mwa 41:38; Dan 1:20“Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”

Danieli Anafasiri Ndoto

194:19 Mwa 41:15; Dan 10:16-17; 2Sam 18:32; Mwa 41:8; 40:12; Dan 7:15, 28; 8:27Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.”

Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako! 20Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote, 214:21 Eze 31:6ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani. 224:22 2Sam 12:7; Yer 27:7; Dan 2:37-38; Ay 20:5; Dan 5:18-19Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.

234:23 Dan 8:13; 5:21; Eze 31:3-4“Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’

244:24 Ay 40:12; Yer 40:2; Ay 34:19; Isa 46:10-11; Za 107:40“Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme: 254:25 Za 83:18; Yer 27:5; Dan 2:47; Ay 24:8; Dan 5:21; Za 83:18Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye. 264:26 Dan 2:37; Lk 15:18Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo. 274:27 Isa 55:6-7; Kum 24:13; 1Fal 21:29; Mdo 8:22; Za 41:3; Mit 28:13; Yer 29:7; Eze 18:22Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”

Ndoto Inatimia

284:28 Hes 23:19; 2Sam 22:28; Dan 5:20Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza. 29Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli, 304:30 Mit 16:18; Isa 37:24-25; Hab 1:11; Isa 13:19; 10:13; Dan 5:20alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”

314:31 2Sam 22:28; Dan 5:20Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako. 324:32 Ay 9:12Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”

334:33 Ay 20:5; Dan 5:20-21; Ay 24:8Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.

344:34 Dan 12:7; Ufu 4:10; Lk 1:33; Ay 12:20; Isa 37:16; Dan 6:26; Za 145:13; Dan 2:44; 5:21Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele.

Utawala wake ni utawala wa milele;

ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.

354:35 Isa 40:17; Kum 21:8; Yon 1:14; Ay 9:4; Rum 9:20; Isa 14:24; 45:9; Za 115:3; 136:6; Kum 32:39; Dan 5:21Mataifa yote ya dunia

yanahesabiwa kuwa si kitu.

Hufanya kama atakavyo

kwa majeshi ya mbinguni,

na kwa mataifa ya dunia.

Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake

au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”

364:36 Mit 22:4; Dan 5:18; Ay 42:12Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni. 374:37 Kum 32:4; Za 33:4-5; Kut 18:11; Mt 23:12; Kut 15:2; Za 18:27; 34:3; Ay 31:4; 40:11-12; Isa 13:11; Dan 5:23; Za 119:21Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.

New International Reader’s Version

Daniel 4:1-37

Nebuchadnezzar Dreams About a Tree

1I, King Nebuchadnezzar, am writing this letter.

I am sending it to people who live all over the world. I’m sending it to people of every nation no matter what language they speak.

May you have great success!

2I am pleased to tell you what has happened. The Most High God has done miraculous signs and wonders for me.

3His signs are great.

His wonders are mighty.

His kingdom will last forever.

His rule will never end.

4I was at home in my palace. I was content and very successful. 5But I had a dream that made me afraid. I was lying in bed. Then dreams and visions passed through my mind. They terrified me. 6So I commanded that all the wise men in Babylon be brought to me. I wanted them to tell me what my dream meant. 7Those who try to figure things out by using magic came. So did those who study the heavens. I told all of them what I had dreamed. But they couldn’t tell me what it meant. 8Finally, Daniel came to me. He is called Belteshazzar, after the name of my god. The spirit of the holy gods is in him. I told him my dream.

9I said, “Belteshazzar, you are chief of the magicians. I know that the spirit of the holy gods is in you. No mystery is too hard for you to figure out. Here is my dream. Tell me what it means. 10Here are the visions I saw while I was lying in bed. I looked up and saw a tree standing in the middle of the land. It was very tall. 11It had grown to be large and strong. Its top touched the sky. It could be seen anywhere on earth. 12Its leaves were beautiful. It had a lot of fruit on it. It provided enough food for people and animals. Under the tree, the wild animals found safety. The birds lived in its branches. Every creature was fed from that tree.

13“While I was still lying in bed, I looked up. In my visions, I saw a holy one. He was a messenger. He was coming down from heaven. 14He called out in a loud voice. He said, ‘Cut down the tree. Break off its branches. Strip off its leaves. Scatter its fruit. Let the animals under it run away. Let the birds in its branches fly off. 15But leave the stump with its roots in the ground. Let it stay in the field. Put a band of iron and bronze around it.

“ ‘Let King Nebuchadnezzar become wet with the dew of heaven. Let him live with the animals among the plants of the earth. 16Let him no longer have the mind of a man. Instead, let him be given the mind of an animal. Let him stay that way until seven periods of time pass by.

17“ ‘The decision is announced by holy messengers. So all who are alive will know that the Most High God is King. He rules over all kingdoms on earth. He gives them to anyone he wants. Sometimes he puts the least important people in charge of them.’

18“This is the dream I, King Nebuchadnezzar, had. Now tell me what it means, Belteshazzar. None of the wise men in my kingdom can explain it to me. But you can. After all, the spirit of the holy gods is in you.”

Daniel Explains Nebuchadnezzar’s Dream

19Daniel, who was also called Belteshazzar, was very bewildered for a while. His thoughts terrified him. So the king said, “Belteshazzar, don’t let the dream or its meaning make you afraid.”

Belteshazzar answered, “My master, I wish the dream were about your enemies! I wish its meaning had to do with them! 20You saw a tree. It grew to be large and strong. Its top touched the sky. It could be seen from anywhere on earth. 21Its leaves were beautiful. It had a lot of fruit on it. It provided enough food for people and animals. Under the tree, the wild animals found safety. The birds lived in its branches. 22Your Majesty, you are that tree! You have become great and strong. Your greatness has grown until it reaches the sky. Your rule has spread to all parts of the earth.

23“Your Majesty, you saw a holy one. He was a messenger. He came down from heaven. He said, ‘Cut down the tree. Destroy it. But leave the stump with its roots in the ground. Let it stay in the field. Put an iron and bronze band around it. Let King Nebuchadnezzar become wet with the dew of heaven. Let him live with the wild animals. Let him stay that way until seven periods of time pass by.’

24“Your Majesty, here is what your dream means. The Most High God has given an order against you. 25You will be driven away from people. You will live with the wild animals. You will eat grass just as an ox does. You will become wet with the dew of heaven. Seven periods of time will pass by for you. Then you will recognize that the Most High God rules over all kingdoms on earth. He gives them to anyone he wants. 26But he gave a command to leave the stump of the tree along with its roots. That means your kingdom will be given back to you. It will happen when you recognize that the God of heaven rules. 27So, Your Majesty, I hope you will accept my advice. Stop being sinful. Do what is right. Give up your evil practices. Show kindness to those who are being treated badly. Then perhaps things will continue to go well with you.”

Nebuchadnezzar’s Dream Comes True

28All this happened to King Nebuchadnezzar. 29It took place twelve months later. He was walking on the roof of his palace in Babylon. 30He said, “Isn’t this the great Babylon I have built as a place for my royal palace? I used my mighty power to build it. It shows how glorious my majesty is.”

31He was still speaking when he heard a voice from heaven. It said, “King Nebuchadnezzar, here is what has been ordered concerning you. Your royal authority has been taken from you. 32You will be driven away from people. You will live with the wild animals. You will eat grass just as an ox does. Seven periods of time will pass by for you. Then you will recognize that the Most High God rules over all kingdoms on earth. He gives them to anyone he wants.”

33What had been said about King Nebuchadnezzar came true at once. He was driven away from people. He ate grass just as an ox does. His body became wet with the dew of heaven. He stayed that way until his hair grew like the feathers of an eagle. His nails became like the claws of a bird.

34At the end of that time I, Nebuchadnezzar, looked up toward heaven. My mind became clear again. Then I praised the Most High God. I gave honor and glory to the God who lives forever.

His rule will last forever.

His kingdom will never end.

35He considers all the nations on earth

to be nothing.

He does as he pleases

with the powers of heaven.

He does what he wants

with the nations of the earth.

No one can hold back his hand.

No one can say to him,

“What have you done?”

36My honor and glory were returned to me when my mind became clear again. The glory of my kingdom was given back to me. My advisers and nobles came to me. And I was put back on my throne. I became even greater than I had been before. 37Now I, Nebuchadnezzar, give praise and honor and glory to the King of heaven. Everything he does is right. All his ways are fair. He is able to bring down those who live proudly.