Danieli 12 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 12:1-13

Nyakati Za Mwisho

112:1 Dan 10:13; Yud 9; Dan 9:12; Lk 10:20; Yer 17:13; Mt 24:21; Mk 13:19; Yer 30:7; Za 56:8; Kut 32:32“Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa. 212:2 Isa 26:19; Yn 5:28-29; Mt 25:46; Yn 11:24Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele. 312:3 Dan 11:33; Yn 5:35; Flp 2:15; Mit 4:18; 1Kor 15:42; Mt 13:43Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele. 412:4 Isa 8:16; Ufu 22:10; Yer 5:1Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”

512:5 Dan 10:4Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto. 612:6 Eze 9:2; Dan 8:13; Za 74:9Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”

712:7 Dan 6:26; Ufu 10:5-7; Lk 21:24; Dan 8:24; 8:24; Ufu 11:2; Mwa 14:22Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.12:7 Wakati, nyakati mbili na nusu wakati maana yake mwaka mmoja, miaka miwili, na nusu mwaka, yaani miaka mitatu na nusu. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”

8Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”

912:9 Isa 29:11Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho. 1012:10 Isa 1:25; Zek 13:9; Hos 14:9; Isa 32:7; Ufu 22:11; Dan 11:35Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.

1112:11 Mk 13:14; Dan 8:11; 9:27; Mt 24:15; Kut 29:38; Ufu 11:2“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290. 1212:12 Isa 30:18; Eze 4:5-6; Dan 8:14Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.

1312:13 Isa 57:2“Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”

New Russian Translation

Даниил 12:1-13

О конце времен

1В то время поднимется Михаил, великий князь, защитник твоего народа. Тогда будет такое бедственное время, какого не было с тех пор, как появились народы, до того времени. Но в то время твой народ – все, чьи имена будут найдены записанными в книгу – будет избавлен. 2Многие из спящих в прахе земли проснутся: одни для вечной жизни, другие – на позор и вечное отвращение. 3Мудрые12:3 Или: «Учащие мудрости». воссияют подобно сиянью небес12:3 Или: «небесной тверди»., и те, кто ведет многих к праведности, – подобно звездам, – во веки и веки! 4Но ты, Даниил, скрой эти слова и запечатай свиток, пока не придут последние времена. Многие будут метаться из стороны в сторону, а знание будет умножаться.

5Я, Даниил, увидел, как появились двое других – один на одном берегу реки, а другой на другом берегу. 6Один из них сказал одетому в льняные одежды, который стоял над водами реки:

– Сколько времени пройдет до конца этих непостижимых событий?

7Одетый в льняные одежды, который стоял над водами реки, поднял правую и левую руки к небу, и я услышал, как он клянется Живущим вечно, говоря:

– Год, два года и полгода12:7 То есть 3,5 года.. Когда не станет того, кто сломил силы святого народа12:7 Или: «Когда силы святого народа будут сломлены»., все это совершится.

8Я услышал, но не понял. Тогда я спросил:

– Мой господин, каким будет исход всего этого?

9Он ответил:

– Иди, Даниил. Эти слова скрыты и запечатаны до последних времен. 10Многие очистятся, убелятся и будут испытаны, но нечестивые будут продолжать поступать нечестиво. Никто из нечестивых не поймет, но те, кто мудр, поймут.

11Со времени, когда будет отменена ежедневная жертва и будет поставлена опустошающая мерзость, пройдет тысяча двести девяносто дней. 12Блажен тот, кто ждет и достигнет завершения тысячи трехсот тридцати пяти дней.

13А ты иди своим путем до конца. Ты упокоишься и в конце дней встанешь, чтобы получить свою долю.