Ayubu 42 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 42:1-17

Sehemu Ya Tano

(Ayubu 42)

Ayubu Anamjibu Bwana

1Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:

242:2 Mwa 18:14; Yer 32:17; Mt 19:26; 2Nya 20:6; Efe 1:11“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote,

wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.

342:3 Ay 34:35; 38:2; Za 40:5Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’

Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi,

mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.

442:4 Ay 38:3; 40:7“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena;

nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’

542:5 Ay 26:14; Rum 10:17; Amu 13:22; Mt 5:8Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako,

lakini sasa macho yangu yamekuona.

642:6 Eze 6:9; Rum 12:3; Kut 10:3; Ezr 9:6Kwa hiyo najidharau mwenyewe,

na kutubu katika mavumbi na majivu.”

Mwisho: Marafiki Wa Ayubu Wanafedheheshwa

742:7 Yos 1:7; Ay 32:3, 8; 9:15Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu. 842:8 Hes 23:29; Eze 45:23; Mwa 20:17; Yak 5:15-17; Ay 22:30Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.” 942:9 Ay 2:11; Mwa 19:21; 20:17; Eze 14:14Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.

1042:10 Kum 30:3; Za 14:7; 126:5-6; Yak 5:11Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni. 1142:11 Ay 19:13Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.

1242:12 Yak 5:11Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja. 13Tena alikuwa na wana saba na binti watatu. 14Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki. 15Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.

16Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne. 1742:17 Mwa 15:15; 25:8Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.

Nova Versão Internacional

Jó 42:1-17

1Então Jó respondeu ao Senhor:

2“Sei que podes fazer todas as coisas;

nenhum dos teus planos pode ser frustrado.

3Tu perguntaste:

‘Quem é esse que obscurece o meu conselho sem conhecimento?’

Certo é que falei de coisas que eu não entendia,

coisas tão maravilhosas que eu não poderia saber.

4“Tu disseste: ‘Agora escute, e eu falarei;

vou fazer perguntas,

e você me responderá’.

5Meus ouvidos já tinham ouvido a teu respeito,

mas agora os meus olhos te viram.

6Por isso menosprezo a mim mesmo

e me arrependo no pó e na cinza”.

Epílogo

7Depois que o Senhor disse essas palavras a Jó, disse também a Elifaz, de Temã: “Estou indignado com você e com os seus dois amigos, pois vocês não falaram o que é certo a meu respeito, como fez meu servo Jó. 8Vão agora até meu servo Jó, levem sete novilhos e sete carneiros, e com eles apresentem holocaustos42.8 Isto é, sacrifícios totalmente queimados. em favor de vocês mesmos. Meu servo Jó orará por vocês; eu aceitarei a oração dele e não farei a vocês o que merecem pela loucura que cometeram. Vocês não falaram o que é certo a meu respeito, como fez meu servo Jó”. 9Então Elifaz, de Temã, Bildade, de Suá, e Zofar, de Naamate, fizeram o que o Senhor lhes ordenara; e o Senhor aceitou a oração de Jó.

10Depois que Jó orou por seus amigos, o Senhor o tornou novamente próspero e lhe deu em dobro tudo o que tinha antes. 11Todos os seus irmãos e irmãs e todos os que o haviam conhecido anteriormente vieram comer com ele em sua casa. Eles o consolaram e o confortaram por todas as tribulações que o Senhor tinha trazido sobre ele, e cada um lhe deu uma peça de prata42.11 Hebraico: 1 quesita. Uma quesita era uma unidade monetária de peso e valor desconhecidos. e um anel de ouro.

12O Senhor abençoou o final da vida de Jó mais do que o início. Ele teve catorze mil ovelhas, seis mil camelos, mil juntas de boi e mil jumentos. 13Também teve ainda sete filhos e três filhas. 14À primeira filha deu o nome de Jemima, à segunda o de Quézia e à terceira o de Quéren-Hapuque. 15Em parte alguma daquela terra havia mulheres tão bonitas como as filhas de Jó, e seu pai lhes deu herança junto com os seus irmãos.

16Depois disso Jó viveu cento e quarenta anos; viu seus filhos e os descendentes deles até a quarta geração. 17E então morreu, em idade muito avançada.