Ayubu 42 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 42:1-17

Sehemu Ya Tano

(Ayubu 42)

Ayubu Anamjibu Bwana

1Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:

242:2 Mwa 18:14; Yer 32:17; Mt 19:26; 2Nya 20:6; Efe 1:11“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote,

wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.

342:3 Ay 34:35; 38:2; Za 40:5Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’

Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi,

mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.

442:4 Ay 38:3; 40:7“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena;

nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’

542:5 Ay 26:14; Rum 10:17; Amu 13:22; Mt 5:8Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako,

lakini sasa macho yangu yamekuona.

642:6 Eze 6:9; Rum 12:3; Kut 10:3; Ezr 9:6Kwa hiyo najidharau mwenyewe,

na kutubu katika mavumbi na majivu.”

Mwisho: Marafiki Wa Ayubu Wanafedheheshwa

742:7 Yos 1:7; Ay 32:3, 8; 9:15Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu. 842:8 Hes 23:29; Eze 45:23; Mwa 20:17; Yak 5:15-17; Ay 22:30Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.” 942:9 Ay 2:11; Mwa 19:21; 20:17; Eze 14:14Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.

1042:10 Kum 30:3; Za 14:7; 126:5-6; Yak 5:11Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni. 1142:11 Ay 19:13Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.

1242:12 Yak 5:11Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja. 13Tena alikuwa na wana saba na binti watatu. 14Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki. 15Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.

16Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne. 1742:17 Mwa 15:15; 25:8Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.

Hoffnung für Alle

Hiob 42:1-17

Gott wendet Hiobs Schicksal zum Guten

(Kapitel 42)

Hiobs letztes Wort

1Da antwortete Hiob:

2»Herr, ich erkenne, dass du alles zu tun vermagst;

nichts und niemand kann deinen Plan vereiteln.

3Du hast gefragt:

›Wer bist du, dass du meine Weisheit anzweifelst

mit Worten ohne Verstand?‹

Ja, es ist wahr:

Ich habe von Dingen geredet, die ich nicht begreife,

sie sind zu hoch für mich und übersteigen meinen Verstand.

4Du hast gesagt:

›Hör mir zu, jetzt rede ich, ich will dich fragen,

und du sollst mir antworten!‹

5Herr, ich kannte dich nur vom Hörensagen,

jetzt aber habe ich dich mit eigenen Augen gesehen!

6Darum widerrufe ich meine Worte,

ich bereue in Staub und Asche!«

Gott stellt sich hinter Hiob

7Nachdem der Herr dies alles zu Hiob gesagt hatte, wandte er sich an Elifas aus Teman: »Ich bin voller Zorn über dich und deine beiden Freunde, ihr habt nicht die Wahrheit über mich gesagt, so wie mein Diener Hiob es tat! 8Bringt nun sieben junge Stiere und sieben Schafböcke, geht damit zu meinem Diener Hiob und bringt sie als Brandopfer dar! Hiob soll für euch beten, denn nur ihn will ich erhören und euch um seinetwillen nichts Böses tun. Denn ihr habt nicht wie er die Wahrheit über mich gesagt.«

9Da taten Elifas aus Teman, Bildad aus Schuach und Zofar aus Naama, was ihnen der Herr befohlen hatte. Und Gott erhörte Hiobs Gebet.

10Als Hiob für seine Freunde betete, da wendete der Herr für ihn alles zum Guten. Er gab ihm doppelt so viel, wie er früher besessen hatte. 11Alle seine Brüder und Schwestern und die früheren Bekannten besuchten ihn wieder. Sie aßen mit ihm in seinem Haus und trösteten ihn wegen des Unglücks, das der Herr über ihn gebracht hatte. Jeder schenkte ihm ein Silberstück und einen Ring aus Gold.

12Der Herr segnete Hiob von jetzt an mehr als zuvor. Bald besaß er 14.000 Schafe und Ziegen, 6000 Kamele, 1000 Rindergespanne und 1000 Esel. 13Er bekam auch wieder sieben Söhne und drei Töchter. 14Die erste nannte er Jemima (»Täubchen«), die zweite Kezia (»Zimtblüte«) und die dritte Keren-Happuch (»Schminkdöschen«). 15Im ganzen Land gab es keine schöneren Frauen als Hiobs Töchter; sie durften mit ihren Brüdern das Erbe teilen.

16Hiob lebte noch 140 Jahre, er sah Kinder und Enkel bis in die vierte Generation. 17Schließlich starb er in hohem Alter nach einem reichen und erfüllten Leben.