Ayubu 40 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 40:1-24

140:1 Ay 5:8; 13:3; 13:3; 9:15; 9:3; 11:8; 33:13Bwana akamwambia Ayubu:

240:2 Rum 9:20“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha?

Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”

3Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:

440:4 Ay 42:6; Amu 18:19; Ay 29:9; Ezr 9:6; Zek 2:13“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe?

Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.

540:5 Ay 9:3; 9:15Nimesema mara moja, lakini sina jibu;

naam, nimesema mara mbili,

lakini sitasema tena.”

640:6 Kut 14:21; Ay 38:1Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:

740:7 Ay 38:3“Jikaze kama mwanaume;

nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.

840:8 Ay 15:25; Rum 3:3; Za 51:4“Je, utabatilisha hukumu yangu?

Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?

940:9 2Nya 32:8; Za 98:1; Kut 20:19; Za 29:3-4Je, una mkono kama wa Mungu,

nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?

1040:10 Za 29:1-2; 45:3; 93:1; 96:6; 104:1; 145:5Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari,

nawe uvae heshima na enzi.

1140:11 Nah 1:6; Sef 1:18; Za 18:27; Isa 32:19Fungulia ukali wa ghadhabu yako,

mtafute kila mwenye kiburi umshushe,

1240:12 Za 52:5; 1Pet 5:5; Dan 5:20; Mal 4:3; Lk 18:14mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze,

waponde waovu mahali wasimamapo.

1340:13 Hes 16:31-34; Ay 4:9Wazike wote mavumbini pamoja;

wafunge nyuso zao kaburini.

1440:14 Kut 15:6; Isa 63:5Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia

kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.

1540:15 Ay 9:9; Isa 11:7; 65:25“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi,40:15 Huyu alikuwa mnyama wa nyakati za zamani ambaye hajulikani hasa ni gani.

niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe,

anayekula majani kama ngʼombe.

1640:16 Ay 39:11; 41:9Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake,

uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!

1740:17 Ay 41:15Mkia wake hutikisika kama mwerezi;

mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.

1840:18 Ay 41:12; Isa 11:4; 49:2Mifupa yake ni bomba za shaba,

maungo yake ni kama fito za chuma.

1940:19 Za 40:5; Isa 27:1Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu,

lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.

2040:20 Za 104:14, 26Vilima humletea yeye mazao yake,

nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.

2140:21 Mwa 41:2; Za 68:30; Isa 35:7; Ay 8:11Hulala chini ya mimea ya yungiyungi,

katika maficho ya matete kwenye matope.

2240:22 Za 1:3; Isa 44:4Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake;

miti mirefu karibu na kijito humzunguka.

23Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu;

yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.

2440:24 2Fal 19:28; Isa 37:29Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho,

au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

New International Version – UK

Job 40:1-24

1The Lord said to Job:

2‘Will the one who contends with the Almighty correct him?

Let him who accuses God answer him!’

3Then Job answered the Lord:

4‘I am unworthy – how can I reply to you?

I put my hand over my mouth.

5I spoke once, but I have no answer –

twice, but I will say no more.’

6Then the Lord spoke to Job out of the storm:

7‘Brace yourself like a man;

I will question you,

and you shall answer me.

8‘Would you discredit my justice?

Would you condemn me to justify yourself?

9Do you have an arm like God’s,

and can your voice thunder like his?

10Then adorn yourself with glory and splendour,

and clothe yourself in honour and majesty.

11Unleash the fury of your wrath,

look at all who are proud and bring them low,

12look at all who are proud and humble them,

crush the wicked where they stand.

13Bury them all in the dust together;

shroud their faces in the grave.

14Then I myself will admit to you

that your own right hand can save you.

15‘Look at Behemoth,

which I made along with you

and which feeds on grass like an ox.

16What strength it has in its loins,

what power in the muscles of its belly!

17Its tail sways like a cedar;

the sinews of its thighs are close-knit.

18Its bones are tubes of bronze,

its limbs like rods of iron.

19It ranks first among the works of God,

yet its Maker can approach it with his sword.

20The hills bring it their produce,

and all the wild animals play nearby.

21Under the lotus plant it lies,

hidden among the reeds in the marsh.

22The lotuses conceal it in their shadow;

the poplars by the stream surround it.

23A raging river does not alarm it;

it is secure, though the Jordan should surge against its mouth.

24Can anyone capture it by the eyes,

or trap it and pierce its nose?