Ayubu 39 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 39:1-30

139:1 Kum 14:5“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?

Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?

239:2 Mwa 31:7-9Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?

Je, unajua majira yao ya kuzaa?

3Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;

utungu wa kuzaa unakoma.

4Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;

huenda zao wala hawarudi tena.

539:5 Mwa 16:12; Ay 6:5“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?

Ni nani aliyezifungua kamba zake?

639:6 Za 107:34; Yer 2:24; 14:6; Hos 8:9Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,

nchi ya chumvi kuwa makao yake.

739:7 Ay 5:22; 3:18Huzicheka ghasia za mji,

wala hasikii kelele za mwendesha gari.

839:8 Isa 32:20Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho

na kutafuta kila kitu kibichi.

939:9 Hes 23:22; Kum 33:17“Je, nyati atakubali kukutumikia?

Atakaa karibu na hori lako usiku?

1039:10 Ay 41:13; Za 32:9Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?

Je, atalima mabonde nyuma yako?

1139:11 Ay 40:16; 41:12, 22; Za 147:10Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?

Utamwachia yeye kazi zako nzito?

12Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani

kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?

1339:13 Zek 5:9“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,

lakini hayawezi kulinganishwa

na mabawa na manyoya ya korongo.

14Huyataga mayai yake juu ya ardhi,

na kuyaacha yapate joto mchangani,

1539:15 2Fal 14:9bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,

kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

1639:16 Ay 39:17; Mao 4:3Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;

hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,

1739:17 Ay 21:22; 39:16kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,

wala hakumpa fungu la akili njema.

1839:18 Ay 5:22Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,

humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

1939:19 Ay 39:11“Je, wewe humpa farasi nguvu

au kuivika shingo yake manyoya marefu?

2039:20 Yoe 2:4-5; Ufu 9:7; Yer 8:16Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,

akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

2139:21 Yer 8:6Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,

husonga mbele kukabiliana na silaha.

2239:22 Ay 5:22Huicheka hofu, haogopi chochote,

wala haukimbii upanga.

2339:23 Isa 5:28; Yer 5:16; Nah 3:3Podo hutoa sauti kando yake,

pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

2439:24 Hes 10:9; Eze 7:14Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,

wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

2539:25 Yos 6:5; Yer 8:6; Amo 2:2Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’

Hunusa harufu ya vita toka mbali,

sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

26“Je, mwewe huruka kwa hekima yako

na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

27Je, tai hupaa juu kwa amri yako

na kujenga kiota chake mahali pa juu?

28Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;

majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

29Kutoka huko hutafuta chakula chake;

macho yake hukiona kutoka mbali.

3039:30 Mt 24:28; Lk 17:37Makinda yake hujilisha damu,

na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

New International Version

Job 39:1-30

1“Do you know when the mountain goats give birth?

Do you watch when the doe bears her fawn?

2Do you count the months till they bear?

Do you know the time they give birth?

3They crouch down and bring forth their young;

their labor pains are ended.

4Their young thrive and grow strong in the wilds;

they leave and do not return.

5“Who let the wild donkey go free?

Who untied its ropes?

6I gave it the wasteland as its home,

the salt flats as its habitat.

7It laughs at the commotion in the town;

it does not hear a driver’s shout.

8It ranges the hills for its pasture

and searches for any green thing.

9“Will the wild ox consent to serve you?

Will it stay by your manger at night?

10Can you hold it to the furrow with a harness?

Will it till the valleys behind you?

11Will you rely on it for its great strength?

Will you leave your heavy work to it?

12Can you trust it to haul in your grain

and bring it to your threshing floor?

13“The wings of the ostrich flap joyfully,

though they cannot compare

with the wings and feathers of the stork.

14She lays her eggs on the ground

and lets them warm in the sand,

15unmindful that a foot may crush them,

that some wild animal may trample them.

16She treats her young harshly, as if they were not hers;

she cares not that her labor was in vain,

17for God did not endow her with wisdom

or give her a share of good sense.

18Yet when she spreads her feathers to run,

she laughs at horse and rider.

19“Do you give the horse its strength

or clothe its neck with a flowing mane?

20Do you make it leap like a locust,

striking terror with its proud snorting?

21It paws fiercely, rejoicing in its strength,

and charges into the fray.

22It laughs at fear, afraid of nothing;

it does not shy away from the sword.

23The quiver rattles against its side,

along with the flashing spear and lance.

24In frenzied excitement it eats up the ground;

it cannot stand still when the trumpet sounds.

25At the blast of the trumpet it snorts, ‘Aha!’

It catches the scent of battle from afar,

the shout of commanders and the battle cry.

26“Does the hawk take flight by your wisdom

and spread its wings toward the south?

27Does the eagle soar at your command

and build its nest on high?

28It dwells on a cliff and stays there at night;

a rocky crag is its stronghold.

29From there it looks for food;

its eyes detect it from afar.

30Its young ones feast on blood,

and where the slain are, there it is.”