Ayubu 39 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 39:1-30

139:1 Kum 14:5“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?

Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?

239:2 Mwa 31:7-9Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?

Je, unajua majira yao ya kuzaa?

3Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;

utungu wa kuzaa unakoma.

4Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;

huenda zao wala hawarudi tena.

539:5 Mwa 16:12; Ay 6:5“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?

Ni nani aliyezifungua kamba zake?

639:6 Za 107:34; Yer 2:24; 14:6; Hos 8:9Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,

nchi ya chumvi kuwa makao yake.

739:7 Ay 5:22; 3:18Huzicheka ghasia za mji,

wala hasikii kelele za mwendesha gari.

839:8 Isa 32:20Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho

na kutafuta kila kitu kibichi.

939:9 Hes 23:22; Kum 33:17“Je, nyati atakubali kukutumikia?

Atakaa karibu na hori lako usiku?

1039:10 Ay 41:13; Za 32:9Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?

Je, atalima mabonde nyuma yako?

1139:11 Ay 40:16; 41:12, 22; Za 147:10Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?

Utamwachia yeye kazi zako nzito?

12Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani

kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?

1339:13 Zek 5:9“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,

lakini hayawezi kulinganishwa

na mabawa na manyoya ya korongo.

14Huyataga mayai yake juu ya ardhi,

na kuyaacha yapate joto mchangani,

1539:15 2Fal 14:9bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,

kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

1639:16 Ay 39:17; Mao 4:3Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;

hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,

1739:17 Ay 21:22; 39:16kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,

wala hakumpa fungu la akili njema.

1839:18 Ay 5:22Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,

humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

1939:19 Ay 39:11“Je, wewe humpa farasi nguvu

au kuivika shingo yake manyoya marefu?

2039:20 Yoe 2:4-5; Ufu 9:7; Yer 8:16Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,

akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

2139:21 Yer 8:6Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,

husonga mbele kukabiliana na silaha.

2239:22 Ay 5:22Huicheka hofu, haogopi chochote,

wala haukimbii upanga.

2339:23 Isa 5:28; Yer 5:16; Nah 3:3Podo hutoa sauti kando yake,

pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

2439:24 Hes 10:9; Eze 7:14Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,

wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

2539:25 Yos 6:5; Yer 8:6; Amo 2:2Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’

Hunusa harufu ya vita toka mbali,

sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

26“Je, mwewe huruka kwa hekima yako

na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

27Je, tai hupaa juu kwa amri yako

na kujenga kiota chake mahali pa juu?

28Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;

majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

29Kutoka huko hutafuta chakula chake;

macho yake hukiona kutoka mbali.

3039:30 Mt 24:28; Lk 17:37Makinda yake hujilisha damu,

na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

New International Reader’s Version

Job 39:1-30

1“Job, do you know when mountain goats have their babies?

Do you watch when female deer give birth?

2Do you count the months until the animals have their babies?

Do you know the time when they give birth?

3They bend their back legs and have their babies.

Then their labor pains stop.

4Their little ones grow strong and healthy in the wild.

They leave and do not come home again.

5“Who let the wild donkeys go free?

Who untied their ropes?

6I gave them the dry and empty land as their home.

I gave them salt flats to live in.

7They laugh at all the noise in town.

They do not hear the shouts of the donkey drivers.

8They wander over the hills to look for grass.

They search for anything green to eat.

9“Job, will wild oxen agree to serve you?

Will they stay by your feed box at night?

10Can you keep them in straight rows with harnesses?

Will they plow the valleys behind you?

11Will you depend on them for their great strength?

Will you let them do your heavy work?

12Can you trust them to haul in your grain?

Will they bring it to your threshing floor?

13“The wings of ostriches flap with joy.

But they can’t compare with the wings and feathers of storks.

14Ostriches lay their eggs on the ground.

They let them get warm in the sand.

15They do not know that something might step on them.

A wild animal might walk all over them.

16Ostriches are mean to their little ones.

They treat them as if they did not belong to them.

They do not care that their work was useless.

17I did not provide ostriches with wisdom.

I did not give them good sense.

18But when they spread their feathers to run,

they laugh at a horse and its rider.

19“Job, do you give horses their strength?

Do you put flowing manes on their necks?

20Do you make them jump like locusts?

They terrify others with their proud snorting.

21They paw the ground wildly.

They are filled with joy.

They charge at their enemies.

22They laugh at fear. They are not afraid of anything.

They do not run away from swords.

23Many arrows rattle at their sides.

Flashing spears and javelins are also there.

24They are so excited that they race over the ground.

They can’t stand still when trumpets are blown.

25When they hear the trumpets they snort, ‘Aha!’

They catch the smells of battle far away.

They hear the shouts of commanders and the battle cries.

26“Job, are you wise enough to teach hawks where to fly?

They spread their wings and fly toward the south.

27Do you command eagles to fly so high?

They build their nests as high as they can.

28They live on cliffs and stay there at night.

High up on the rocks they think they are safe.

29From there they look for their food.

They can see it from far away.

30Their little ones like to eat blood.

Eagles gather where they see dead bodies.”