Ayubu 39 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 39:1-30

139:1 Kum 14:5“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?

Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?

239:2 Mwa 31:7-9Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?

Je, unajua majira yao ya kuzaa?

3Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;

utungu wa kuzaa unakoma.

4Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;

huenda zao wala hawarudi tena.

539:5 Mwa 16:12; Ay 6:5“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?

Ni nani aliyezifungua kamba zake?

639:6 Za 107:34; Yer 2:24; 14:6; Hos 8:9Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,

nchi ya chumvi kuwa makao yake.

739:7 Ay 5:22; 3:18Huzicheka ghasia za mji,

wala hasikii kelele za mwendesha gari.

839:8 Isa 32:20Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho

na kutafuta kila kitu kibichi.

939:9 Hes 23:22; Kum 33:17“Je, nyati atakubali kukutumikia?

Atakaa karibu na hori lako usiku?

1039:10 Ay 41:13; Za 32:9Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?

Je, atalima mabonde nyuma yako?

1139:11 Ay 40:16; 41:12, 22; Za 147:10Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?

Utamwachia yeye kazi zako nzito?

12Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani

kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?

1339:13 Zek 5:9“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,

lakini hayawezi kulinganishwa

na mabawa na manyoya ya korongo.

14Huyataga mayai yake juu ya ardhi,

na kuyaacha yapate joto mchangani,

1539:15 2Fal 14:9bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,

kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

1639:16 Ay 39:17; Mao 4:3Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;

hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,

1739:17 Ay 21:22; 39:16kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,

wala hakumpa fungu la akili njema.

1839:18 Ay 5:22Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,

humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

1939:19 Ay 39:11“Je, wewe humpa farasi nguvu

au kuivika shingo yake manyoya marefu?

2039:20 Yoe 2:4-5; Ufu 9:7; Yer 8:16Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,

akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

2139:21 Yer 8:6Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,

husonga mbele kukabiliana na silaha.

2239:22 Ay 5:22Huicheka hofu, haogopi chochote,

wala haukimbii upanga.

2339:23 Isa 5:28; Yer 5:16; Nah 3:3Podo hutoa sauti kando yake,

pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

2439:24 Hes 10:9; Eze 7:14Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,

wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

2539:25 Yos 6:5; Yer 8:6; Amo 2:2Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’

Hunusa harufu ya vita toka mbali,

sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

26“Je, mwewe huruka kwa hekima yako

na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

27Je, tai hupaa juu kwa amri yako

na kujenga kiota chake mahali pa juu?

28Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;

majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

29Kutoka huko hutafuta chakula chake;

macho yake hukiona kutoka mbali.

3039:30 Mt 24:28; Lk 17:37Makinda yake hujilisha damu,

na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約伯記 39:1-30

1「你知道野山羊何時生產嗎?

你看過母鹿產仔嗎?

2你能算出牠們懷胎的月數嗎?

你知道牠們分娩的日期嗎?

3牠們幾時屈身產仔,

結束分娩之痛?

4幼仔健壯,在荒野長大,

離群而去,不再回來。

5「誰讓野驢逍遙自在?

誰解開了牠的韁繩?

6我使牠以曠野為家,

以鹽地作居所。

7牠嗤笑城邑的喧鬧,

不聽趕牲口的吆喝。

8牠以群山作草場,

尋找青翠之物。

9「野牛豈肯為你效勞,

在你的槽旁過夜?

10你豈能用韁繩把野牛牽到犁溝?

牠豈肯跟著你在山谷耕地?

11你豈能倚靠牠的大力,

把你的重活交給牠?

12豈能靠牠運回糧食,

替你堆聚到麥場?

13「鴕鳥歡然拍動翅膀,

牠豈有白鸛的翎羽?

14牠將蛋產在地上,

使蛋得到沙土的溫暖,

15卻不知蛋會被踩碎,

或遭野獸踐踏。

16牠苛待雛鳥,好像牠們並非己出,

就算徒勞一場,牠也不怕。

17因為上帝未賜牠智慧,

沒有給牠悟性。

18然而,一旦牠展翅奔跑,

必嗤笑馬兒和騎士。

19「馬的力量豈是你賜的?

牠頸上的鬃毛豈是你披的?

20豈是你使牠跳躍如蝗蟲,

發出令人膽寒的長嘶?

21牠在谷中刨地,

炫耀力量,奮力衝向敵軍。

22牠嘲笑恐懼,毫不害怕,

不因刀劍而退縮。

23牠背上的箭袋錚錚作響,

長矛和投槍閃閃發光。

24角聲一響,牠便無法靜立,

狂烈地顫抖,急於馳騁大地。

25聽到角聲,牠就發出長嘶,

牠老遠便嗅到戰爭的氣味,

並聽見吶喊和將領的號令。

26「鷹隼展翅翱翔,飛往南方,

豈是靠你的智慧?

27禿鷹騰飛,在高處搭窩,

豈是奉你的命令?

28牠居住在懸崖上,

盤踞在山岩峭壁,

29牠從那裡搜尋獵物,

牠的目光直達遠方。

30牠的幼雛噬血,

哪裡有屍體,牠就在哪裡。」