Ayubu 38 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 38:1-41

Sehemu Ya Nne: Mungu Anazungumza

(Ayubu 38–41)

Bwana Anamjibu Ayubu

138:1 1Sam 2:10; Eze 1:4; Kut 19:16-18; Ay 11:5; 40:6; Isa 21:1Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:

238:2 Mk 10:38; 1Tim 1:7“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza

kwa maneno yasiyo na maarifa?

338:3 Ay 40:7; 42:4; Mk 11:29; 1Fal 18:46Jikaze kama mwanaume;

nitakuuliza swali,

nawe unijibu.

438:4 Mwa 1:1; Mit 8:29; Za 104:5“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?

Niambie, kama unafahamu.

538:5 Za 102:25; Yer 31:37Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?

Hakika wewe unajua!

Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?

638:6 Mit 8:25; Ay 26:7Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,

au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,

738:7 Mwa 1:16; Za 19:1-4; 148:2-3; 1Fal 22:19; Kum 16:15wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,

na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?

838:8 Za 33:7; Yer 5:22; Mwa 1:9-10“Ni nani aliyeifungia bahari milango

ilipopasuka kutoka tumbo,

938:9 Mwa 1:2nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,

na kuyafungia katika giza nene,

1038:10 Za 33:7; Neh 3:3; Isa 40:12; Ay 7:12nilipoamuru mipaka yake,

na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,

1138:11 Za 65:7; 89:9; 104:6-9niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi;

hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?

1238:12 Za 57:8; 74:16; Amo 5:8“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke,

au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,

13yapate kushika miisho ya dunia,

na kuwakungʼuta waovu waliomo?

1438:14 Kut 28:11Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri;

sura yake hukaa kama ile ya vazi.

1538:15 Kum 28:29; Ay 15:22; Mwa 17:14; Za 10:15Waovu huzuiliwa nuru yao,

nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.

1638:16 Mwa 1:7; Ay 9:8“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?

Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?

1738:17 Za 9:13; Mt 16:18Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti?

Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?

1838:18 Ay 28:24; Isa 40:12; Ay 38:4Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia?

Niambie kama unajua haya yote.

1938:19 Mwa 1:4; Ay 28:3; Za 139:11-12“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi?

Nako maskani mwa giza ni wapi?

2038:20 Ay 24:13Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake?

Unajua njia za kufika maskani mwake?

2138:21 Ay 15:7Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa!

Kwani umeishi miaka mingi!

2238:22 Ay 37:6; Kum 28:12; Za 105:32; 147:17“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji,

au kuona ghala za mvua ya mawe,

2338:23 Za 27:5; Isa 28:17; Eze 13:13; Ufu 16:21; Kut 9:18; Za 9:13ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu,

na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?

2438:24 Ay 28:24; 27:21; Yer 10:13; 51:16Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa,

au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?

2538:25 Ay 28:26Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi

na njia ya umeme wa radi,

2638:26 Ay 36:27; Za 84:6; 107:35; Isa 41:18ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu,

jangwa lisilo na yeyote ndani yake,

2738:27 Ay 28:26; 37:13; Za 104:14ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa,

na majani yaanze kumea ndani yake?

2838:28 2Sam 1:21; Yer 14:22Je, mvua ina baba?

Ni nani baba azaaye matone ya umande?

2938:29 Za 147:16-17Barafu inatoka tumbo la nani?

Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,

3038:30 Ay 37:10wakati maji yawapo magumu kama jiwe,

wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?

3138:31 Ay 9:9; Amo 5:8“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia?

Waweza kulegeza kamba za Orioni?

3238:32 2Fal 23:5; Isa 13:10; 40:26; 45:12; Yer 19:13; Mwa 1:16Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake,

au kuongoza Dubu na watoto wake?

3338:33 Za 148:6; Yer 31:38Je, unajua sheria zinazotawala mbingu?

Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?

3438:34 Ay 5:10; 22:11“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni,

na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?

3538:35 Ay 36:32Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake?

Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?

3638:36 Ay 34:32; Yak 1:5; Za 51:6; Mhu 2:26Ni nani aliyeujalia moyo hekima

au kuzipa akili ufahamu?

3738:37 Yos 3:16; Ay 22:11Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu?

Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni

3838:38 Law 26:19wakati mavumbi yawapo magumu,

na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?

3938:39 Mwa 49:9; Za 104:21“Je, utamwindia simba jike mawindo,

na kuwashibisha simba wenye njaa

4038:40 Ay 37:8; Mwa 49:9wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao,

au wakivizia kichakani?

4138:41 Mwa 8:7; Lk 12:24; Za 147:9; Mt 6:26Ni nani ampaye kunguru chakula

wakati makinda yake yanamlilia Mungu,

yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

Swedish Contemporary Bible

Job 38:1-38

Herren talar och svarar Job

(38:1—41:25)

Herrens första tal: skapelsen och naturen

1Då svarade Herren Job från stormen:

2Vem är denne som höljer mitt råd i mörker,

med ord utan kunskap?

3Gör dig nu beredd och var som en man,

för jag tänker ställa frågor som du får svara på.

4Var var du när jag lade grunden till jorden?

Tala om det för mig, om du nu vet och förstår så mycket.

5Vem som bestämde dess mått vet du nog!

Vem spände mätsnöret över den?

6På vad fästes dess grund,

och vem lade dit hörnstenen

7medan morgonstjärnorna sjöng tillsammans

och Guds söner jublade av glädje?

8Vem spärrade in havet,

när det forsade fram ur djupen,38:8 Det hebreiska bildspråket är ibland starkt, som här – en mer ordagrann översättning skulle lyda: Han stängde in havet bakom dörrar, när det forsade/bröt fram ur moderlivet.

9när jag klädde det med moln

och lindade in det i tjockt mörker,

10när jag bestämde dess gräns

och satte dörrar och bommar för det,

11när jag sa: ”Så långt men inte längre får du komma,

här ska dina stolta vågor stanna!”?

12Har du någonsin befallt morgonen att komma

eller ljuset att bryta fram där det ska,

13för att det ska gripa tag i jordens hörn

och skaka bort de onda därifrån?

14Jorden tar form likt en lerklump under ett sigill,

och den står där, formad som en dräkt.38:14 Grundtextens innebörd är osäker.

15De ogudaktiga berövas sitt ljus,

och deras makt krossas.

16Har du gått till havets källor

eller vandrat på havsdjupens grund?

17Har dödsrikets portar uppenbarats för dig?

Har du sett portarna till det djupaste mörkret?

18Kan du fatta jordens vidder?

Tala om det för mig, om du vet allt detta!

19Var är vägen till ljusets boplats,

och var håller mörkret hus?

20Kan du leda dem till de platser de kommer ifrån?

Vet du vägen till deras vistelseort?

21Naturligtvis vet du allt detta,

för då var du ju redan född,

du som redan levt så länge!

22Har du varit i snöns förrådshus

eller sett haglets förrådshus,

23som jag förvarat till nödens tid,

till stridens och krigets tider?

24Vet du vägen till den plats där ljuset38:24 Eller blixten. delar sig?

Hur sprider sig östanvinden över jorden?

25Vem öppnar rännor för regnfloderna

och ger åskvädret dess bana,

26så att den kan få regnet att falla där ingen bor,

på ökenlandet där ingen människa finns,

27för att mätta ödemarken med vatten,

så att gräs kan växa upp?

28Har regnet någon far?

Vem härstammar daggen ifrån?

29Från vems sköte kommer isen,

och vem föder himlens rimfrost,

30som får vattnen att bli hårda som sten,

när djupets yta fryser till?

31Kan du binda ihop Plejaderna

eller lösa Orions band?38:31 Det är osäkert vilka stjärnbilder/stjärnor som avses.

32Kan du leda fram stjärnbilderna i rätt tid

och visa vägen för Stora och Lilla Björn?

33Känner du till himlens lagar,

och bestämmer du hur de råder över jorden?

34Kan du ropa till molnen

och få dem att överskölja dig med regnvatten?

35Kan du skicka efter blixtar

som svarar dig: ”Här är vi!”?

36Vem har lagt vishet i ibisen,

och vem gav förstånd till tuppen?38:36 Grundtextens innebörd är osäker.

37Vem har vishet att räkna molnen?

Vem kan tömma himlens vattenbehållare,

38när marken är hård

och kokorna klibbar ihop?