Ayubu 37 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 37:1-24

137:1 Za 38:10; Isa 15:5; Yer 4:19; Hab 3:16“Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

237:2 Za 18:13; 29:3-9Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

337:3 2Sam 22:13; Za 18:14; Ay 36:32; Mt 24:27; Lk 17:24Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

437:4 1Sam 2:10; Kut 20:19Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

537:5 Ay 11:7-9Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

637:6 Kum 28:12; Ay 38:22; Mwa 7:4; Ay 36:27Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

737:7 Ay 12:14; Za 111:2; 109:27; 104:19-23Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

837:8 Ay 28:26; 38:40; Za 104:22Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

937:9 Za 50:3; 147:17Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

1037:10 Ay 38:29-30; Za 147:17Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

1137:11 Ay 26:8; 36:30; 28:26Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

1237:12 Za 147:16; 148:8; Ay 37:3Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

1337:13 Kut 9:22-23; 1Sam 12:17; Kut 9:18; 1Fal 18:45Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

1437:14 Ay 32:10; 5:9“Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

1537:15 Ay 36:30, 32Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

1637:16 Ay 36:29; 5:9; 36:4Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

1737:17 Mdo 27:13Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

1837:18 Mwa 1:1, 8; Ay 22:14; Kum 28:23; Za 104:2je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

1937:19 Rum 8:26; Ay 13:18; 9:3“Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

2137:21 Amu 5:31; Mdo 22:1; 26:13Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

2237:22 Za 19:5; Kut 24:17Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

2337:23 Ay 5:9; Rum 11:33; Ay 8:3; Yer 25:5; Mao 3:33Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

2437:24 Mik 6:8; Mt 10:28; 11:25; Efe 5:15Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

O Livro

Job 37:1-24

1O meu coração treme com estas coisas.

2Escuta, escuta o trovão da sua voz,

que ecoa através dos céus!

3Os seus relâmpagos dardejam em todas as direções.

4Depois vem o rugir dos trovões;

ali ecoa a voz tremenda da sua majestade;

quando a sua voz ressoa, ninguém se aguenta em pé.

5Em cada trovão, essa voz é cheia de glória;

não podemos compreender a grandeza do seu poder.

6Porque ele diz à neve, aos aguaceiros e às tempestades

para caírem sobre a Terra.

7Nessas ocasiões, o trabalho do homem cessa,

para que toda a gente possa reconhecer o seu poder.

8Os animais selvagens escondem-se nas rochas e nas tocas.

9O vento do sul traz a chuva;

o do norte, o frio.

10Deus sopra sobre as torrentes

e até os rios mais vastos gelam.

11Carrega as nuvens com humidade

e elas disparam relâmpagos.

12Os raios são dirigidos pela sua mão

e fazem o que lhes manda, por toda a Terra.

13Manda tempestades, ora como castigo para os homens,

ora para regar favoravelmente a sua terra.

14Ouve, Job, detém-te um pouco!

Considera as maravilhas de Deus!

15Sabes como Deus controla toda a natureza

e como faz relampejar através das nuvens?

16Compreendes como é feito, o equilíbrio das nuvens,

por aquele que é perfeito em conhecimento?

17Percebes o calor que te incomoda, quando sopra o vento do sul

e há calma sobre a terra?

18Saberias tu estender o firmamento,

que é sólido como um espelho fundido?

19Tu, que julgas saber tanto, ensina-nos a nós

como deveremos aproximar-nos de Deus.

Somos, talvez, demasiado ignorantes para saber essas coisas!

20Poderá Deus ser notificado, de que eu vou falar?

Haverá algum homem que aceite,

de boa vontade, ser engolido vivo?

21Não podemos olhar para o Sol, por causa da sua luminosidade,

quando os ventos limpam o firmamento de nuvens.

22Do norte vêm resplendores de luz dourada;

Deus está rodeado de temível majestade.

23Não podemos, sequer, imaginar o poder do Todo-Poderoso!

Mesmo assim, é tão justo e misericordioso que não nos destrói.

24Não admira que toda a gente, em toda a parte, o tema!

Ele não se deixa impressionar pelo mais sábio dos homens.”