Ayubu 37 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 37:1-24

137:1 Za 38:10; Isa 15:5; Yer 4:19; Hab 3:16“Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

237:2 Za 18:13; 29:3-9Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

337:3 2Sam 22:13; Za 18:14; Ay 36:32; Mt 24:27; Lk 17:24Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

437:4 1Sam 2:10; Kut 20:19Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

537:5 Ay 11:7-9Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

637:6 Kum 28:12; Ay 38:22; Mwa 7:4; Ay 36:27Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

737:7 Ay 12:14; Za 111:2; 109:27; 104:19-23Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

837:8 Ay 28:26; 38:40; Za 104:22Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

937:9 Za 50:3; 147:17Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

1037:10 Ay 38:29-30; Za 147:17Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

1137:11 Ay 26:8; 36:30; 28:26Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

1237:12 Za 147:16; 148:8; Ay 37:3Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

1337:13 Kut 9:22-23; 1Sam 12:17; Kut 9:18; 1Fal 18:45Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

1437:14 Ay 32:10; 5:9“Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

1537:15 Ay 36:30, 32Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

1637:16 Ay 36:29; 5:9; 36:4Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

1737:17 Mdo 27:13Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

1837:18 Mwa 1:1, 8; Ay 22:14; Kum 28:23; Za 104:2je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

1937:19 Rum 8:26; Ay 13:18; 9:3“Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

2137:21 Amu 5:31; Mdo 22:1; 26:13Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

2237:22 Za 19:5; Kut 24:17Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

2337:23 Ay 5:9; Rum 11:33; Ay 8:3; Yer 25:5; Mao 3:33Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

2437:24 Mik 6:8; Mt 10:28; 11:25; Efe 5:15Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約伯記 37:1-24

1「因此我心戰慄,

在胸膛跳動。

2請仔細聽祂發出的雷聲,

聽祂口中發出的轟鳴。

3祂使閃電劃過整個天空,

亮光直照到地極。

4隨後雷聲隆隆,

祂發出威嚴之聲。

祂一發聲,雷電交加。

5上帝發出奇妙的雷聲,

我們無法測度祂偉大的作為。

6祂命雪降在大地,

令雨傾盆倒下,

7使人們停下工作,

以便世人都知道祂的作為。

8野獸躲進窩裡,

留在洞中。

9暴風從南天而來,

寒流由北方而至。

10上帝噓氣成冰,

使寬闊的水面凝結。

11祂使密雲佈滿水氣,

從雲端發出閃電。

12雲隨祂的指令旋轉,

在地面之上完成祂的吩咐,

13或為懲罰大地,

或為彰顯慈愛。

14約伯啊,請留心聽,

要駐足沉思上帝的奇妙作為。

15你知道上帝如何發出命令,

使雲中電光閃爍嗎?

16你知道全知者的奇妙作為——

祂如何使雲彩飄浮嗎?

17南風吹來,大地沉寂時,

你就汗濕衣襟,你知道為何嗎?

18你能像祂那樣鋪展堅如銅鏡的穹蒼嗎?

19我們因愚昧而無法陳訴,

請指教我們如何與祂對話。

20我怎敢與祂對話?

豈有人自取滅亡?

21風吹散天空的雲後,

無人能仰視太陽的強光。

22北方出現金色的光芒,

上帝充滿可怕的威嚴。

23我們無法測度全能者,

祂充滿能力,無比正直公義,

不恃強凌弱。

24所以,人們都敬畏祂,

祂不看顧自以為有智慧的人。」