Ayubu 37 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 37:1-24

137:1 Za 38:10; Isa 15:5; Yer 4:19; Hab 3:16“Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

237:2 Za 18:13; 29:3-9Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

337:3 2Sam 22:13; Za 18:14; Ay 36:32; Mt 24:27; Lk 17:24Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

437:4 1Sam 2:10; Kut 20:19Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

537:5 Ay 11:7-9Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

637:6 Kum 28:12; Ay 38:22; Mwa 7:4; Ay 36:27Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

737:7 Ay 12:14; Za 111:2; 109:27; 104:19-23Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

837:8 Ay 28:26; 38:40; Za 104:22Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

937:9 Za 50:3; 147:17Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

1037:10 Ay 38:29-30; Za 147:17Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

1137:11 Ay 26:8; 36:30; 28:26Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

1237:12 Za 147:16; 148:8; Ay 37:3Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

1337:13 Kut 9:22-23; 1Sam 12:17; Kut 9:18; 1Fal 18:45Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

1437:14 Ay 32:10; 5:9“Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

1537:15 Ay 36:30, 32Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

1637:16 Ay 36:29; 5:9; 36:4Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

1737:17 Mdo 27:13Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

1837:18 Mwa 1:1, 8; Ay 22:14; Kum 28:23; Za 104:2je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

1937:19 Rum 8:26; Ay 13:18; 9:3“Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

2137:21 Amu 5:31; Mdo 22:1; 26:13Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

2237:22 Za 19:5; Kut 24:17Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

2337:23 Ay 5:9; Rum 11:33; Ay 8:3; Yer 25:5; Mao 3:33Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

2437:24 Mik 6:8; Mt 10:28; 11:25; Efe 5:15Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Аюб 37:1-24

1От этого сердце моё трепещет

и бросается с места прочь.

2Слушайте! Слушайте гром Его голоса

и грохот из уст Его!

3По всему поднебесью посылает Он молнии,

посылает их до краёв земли.

4Голос Его рокочет вослед;

гласом величия Он гремит

и не сдерживает зарниц,

когда голос Его услышан.

5Дивно грохочет Всевышний Своим голосом;

Он творит великое – не постичь нам.

6Говорит Он снегу: «Пади на землю»,

дождю и ливню: «Лейте сильнее!»

7Он прекращает труды каждого человека,

чтобы все люди знали дела Его.

8И уходят звери в свои убежища

и в берлогах своих лежат.

9Из Его покоев приходит вихрь,

и северный ветер приносит стужу.

10Дыханием Всевышнего творится лёд,

и твердеют вольные воды.

11Наполняет Он тучи влагой

и молнии мечет из облаков.

12Облака кружат по Его воле

над лицом всей земли,

совершая, что Он повелит.

13То приходят, как бич, покарать людей,

то, даруя им милость, насыщают землю.

14Выслушай это, Аюб;

подумай, как чудны дела Всевышнего.

15Знаешь ли ты, как управляет тучами Всевышний,

как блестит зарницей из облака Своего?

16Знаешь ли ты, как уравновешены облака,

знаешь ли чудеса Того, Кто познанием совершенен?

17О ты, кому жарко в своей одежде,

когда замолкнет земля перед южным ветром,

18ты ли вместе с Ним распростёр небеса,

твёрдые, словно литое зеркало?

19Научи нас, что нам Ему сказать;

мы не знаем из-за своего невежества.

20Сообщить ли Ему, что хочу с Ним говорить?

Но кто себе желает смерти?

21Никто не может взглянуть на солнце,

когда оно блестит в небесах,

после того, как расчистит их ветер.

22С севера идёт Всевышний в золотом сиянии,

приближается в страшном великолепии.

23Всемогущий – мы не можем Его постичь;

силой и правдой Он велик,

праведностью богат, никого не угнетает.

24Поэтому люди боятся Его,

и мудрые сердцем смотрят на Него.