Ayubu 35 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 35:1-16

Elihu Analaumu Mtu Kujiona Kuwa Mwenye Haki

1Ndipo Elihu akasema:

235:2 Ay 33:32; 2:9; 32:2“Je, unadhani hili ni haki?

Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’

335:3 Ay 21:15; 34:9Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata,

na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’

4“Ningependa nikujibu wewe

pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe.

535:5 Kum 10:14; Mwa 15:5; Ay 22:12; Za 19:1-4Tazama juu mbinguni ukaone;

yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.

635:6 Ay 7:20; Mit 8:36Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu?

Kama dhambi zako zikiwa nyingi,

hilo linamfanyia nini Mungu?

735:7 Rum 11:35; Mit 9:12; 1Kor 4:7; Lk 17:10Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini,

au yeye anapokea nini mkononi kwako?

835:8 Eze 18:24; 18:5-9; Zek 7:9-10Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe,

nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.

935:9 Kut 2:23; Ay 5:15; 12:19; Lk 18:3-7“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso;

huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.

1035:10 Ay 4:17; Isa 51:13; Za 77:6; Mdo 16:25; 1Pet 4:19Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu,

yeye anifanyaye niimbe usiku,

1135:11 Za 94:12; Lk 12:24; Ay 32:8yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia,

na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’

1235:12 1Sam 8:18; Mit 1:1Yeye hajibu wakati watu waliapo

kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

1335:13 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Ay 15:31; Mit 15:8Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili;

Mwenyezi hayazingatii.

1435:14 Ay 9:11; Yer 11:11Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza

wewe usemapo humwoni,

tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake

na wewe lazima umngojee,

15pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu

wala haangalii uovu hata kidogo?

1635:16 Ay 34:35-37; 1Kor 4:20Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana;

anaongea maneno mengi bila maarifa.”

New International Version – UK

Job 35:1-16

1Then Elihu said:

2‘Do you think this is just?

You say, “I am in the right, not God.”

3Yet you ask him, “What profit is it to me,35:3 Or you

and what do I gain by not sinning?”

4‘I would like to reply to you

and to your friends with you.

5Look up at the heavens and see;

gaze at the clouds so high above you.

6If you sin, how does that affect him?

If your sins are many, what does that do to him?

7If you are righteous, what do you give to him,

or what does he receive from your hand?

8Your wickedness only affects humans like yourself,

and your righteousness only other people.

9‘People cry out under a load of oppression;

they plead for relief from the arm of the powerful.

10But no-one says, “Where is God my Maker,

who gives songs in the night,

11who teaches us more than he teaches35:10,11 Or night, / 11 who teaches us by the beasts of the earth

and makes us wiser than35:11 Or us wise by the birds in the sky?”

12He does not answer when people cry out

because of the arrogance of the wicked.

13Indeed, God does not listen to their empty plea;

the Almighty pays no attention to it.

14How much less, then, will he listen

when you say that you do not see him,

that your case is before him

and you must wait for him,

15and further, that his anger never punishes

and he does not take the least notice of wickedness.35:15 Symmachus, Theodotion and Vulgate; the meaning of the Hebrew for this word is uncertain.

16So Job opens his mouth with empty talk;

without knowledge he multiplies words.’