Ayubu 34 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 34:1-37

Elihu Anatangaza Haki Ya Mungu

1Kisha Elihu akasema:

234:2 Ay 32:10“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima;

nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.

334:3 Ay 12:11Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno

kama vile ulimi uonjavyo chakula.

434:4 1The 5:21Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa,

nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.

534:5 Ay 33:9; 6:29; 27:2; 9; 17“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia,

lakini Mungu ameninyima haki yangu.

634:6 Yer 10:19; Ay 10:3Ingawa niko sawa,

ninaonekana mwongo;

nami ingawa sina kosa,

kidonda changu hakiponi.’

734:7 Ay 9:21; 15:16Ni mtu gani aliye kama Ayubu,

anywaye dharau kama maji?

834:8 Ay 22:15; Za 50:18Ashirikianaye na watenda mabaya

na kuchangamana na watu waovu.

934:9 Ay 9:29-31Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote

anapojitahidi kumpendeza Mungu.’

1034:10 Mwa 18:25; Za 92:15; Rum 3:5“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu.

Kamwe Mungu hatendi uovu,

Mwenyezi hafanyi kosa.

1134:11 Ay 21:31; 2Kor 5:10; Yer 17:10; Eze 33; 20; Mit 24:12Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda;

huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.

1234:12 Za 9:16; Kol 3:25Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa,

kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.

1334:13 Ay 36:23; Isa 40:14Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia?

Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?

1434:14 Hes 16:22; Za 104:29; Mhu 12:7Kama lilikuwa kusudi la Mungu,

naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,

1534:15 Za 90:10; Mwa 2:7wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja,

na mtu angerudi mavumbini.

1634:16 Ay 32:10; 34:30“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili;

sikilizeni hili nisemalo.

1734:17 Mwa 18:23; 2Sam 23:3-4; Mit 20:8; Rum 3:5-7; Ay 10:7Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala?

Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?

1834:18 Kut 22:28; Isa 40:24Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’

nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’

1934:19 Kum 10:17; Mdo 10:34; Law 19:15; Yak 2:5yeye asiyependelea wakuu,

wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini,

kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?

2034:20 Kut 11:4; 12:29; Ay 12:19Wanakufa ghafula, usiku wa manane;

watu wanatikiswa nao hupita;

wenye nguvu huondolewa

bila mkono wa mwanadamu.

2134:21 Mit 15:3; Ebr 4:13“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu;

anaona kila hatua yao.

2234:22 Za 74:20; Ay 3:5; Amo 9:2-3Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa,

ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.

2334:23 Ay 11:11; Ezr 9:13Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana,

ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.

2434:24 Ay 12:19; Dan 2:21Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi

na kuwaweka wengine mahali pao.

2534:25 Ay 11:11; Mit 5:21-23Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote,

huwaondoa usiku, nao wakaangamia.

2634:26 Mwa 6:5; Ay 8:22; 28:24; Za 9:5; Yer 44:5Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao

mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,

2734:27 Za 14:3; Isa 5:12; 1Sam 15:11kwa sababu wameacha kumfuata Mungu,

nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.

2834:28 Kut 22:23; Yak 5:4; Mhu 5:8Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake,

hivyo akasikia kilio cha wahitaji.

2934:29 Za 28:1; 83:1; 109:1; Rum 8:34; Za 13:1; 97:9; 83:18Lakini kama akinyamaza kimya,

ni nani awezaye kumhukumu?

Kama akiuficha uso wake,

ni nani awezaye kumwona?

Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,

3034:30 Za 25:15; Mit 29:2-12; 1Fal 12:28-30ili kumzuia mtu mwovu kutawala,

au wale ambao huwategea watu mitego.

31“Kama mwanadamu akimwambia Mungu,

‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.

3234:32 Kut 33:13; Za 27:11; Lk 19:8; Ay 33:27Nifundishe nisichoweza kuona;

kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’

3334:33 Mit 17:23; Yn 3:8Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako,

wakati wewe umekataa kutubu?

Yakupasa wewe uamue, wala si mimi;

sasa niambie lile ulijualo.

34“Wanadamu wenye ufahamu husema,

wenye hekima wanaonisikia huniambia,

3534:35 Ay 35:16; 38:2; 42:3; 26:3‘Ayubu huongea bila maarifa;

maneno yake hayana busara.’

3634:36 Ay 6:29; 22:15Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho,

kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!

37Kwenye dhambi yake huongeza uasi;

kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu,

na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

Ketab El Hayat

أيوب 34:1-37

1وَأَضَافَ أَلِيهُو قَائِلاً: 2«اسْتَمِعُوا إِلَى أَقْوَالِي أَيُّهَا الْحُكَمَاءُ، وَأَصْغُوا إِلَيَّ يَا ذَوِي الْمَعْرِفَةِ، 3لأَنَّ الأُذُنَ تُمَحِّصُ الأَقْوَالَ كَمَا يَتَذَوَّقُ الْحَنَكُ الطَّعَامَ. 4لِنَتَدَاوَلْ فِيمَا بَيْنَنَا لِنُمَيِّزَ مَا هُوَ أَصْوَبُ لَنَا، وَنَتَعَلَّمَ مَعاً مَا هُوَ صَالِحٌ.

5يَقُولُ أَيُّوبُ: ’إِنِّي بَارٌّ، وَلَكِنَّ اللهَ قَدْ تَنَكَّرَ لِحَقِّي، 6وَمَعَ أَنِّي مُحِقٌّ فَأَنَا أُدْعَى كَاذِباً، وَمَعَ أَنِّي بَرِيءٌ فَإِنَّ سَهْمَهُ أَصَابَنِي بِجُرْحٍ مُسْتَعْصٍ‘. 7فَمَنْ هُوَ نَظِيرُ أَيُّوبَ الَّذِي يَجْرَعُ الْهُزْءَ كَالْمَاءِ، 8يُوَاظِبُ عَلَى مُعَاشَرَةِ فَاعِلِي الإِثْمِ، وَيَأْتَلِفُ مَعَ الأَشْرَارِ، 9لأَنَّهُ يَقُولُ: لَا يَنْتَفِعُ الإِنْسَانُ شَيْئاً مِنْ إِرْضَاءِ اللهِ.

10لِذَلِكَ أَصْغُوا إِلَيَّ يَا ذَوِي الْفَهْمِ: حَاشَا لِلهِ أَنْ يَرْتَكِبَ شَرّاً أَوْ لِلْقَدِيرِ أَنْ يَقْتَرِفَ خَطَأً، 11لأَنَّهُ يُجَازِي الإِنْسَانَ بِمُوْجِبِ أَعْمَالِهِ، وَبِمُقْتَضَى طَرِيقِهِ يُحَاسِبُهُ. 12إِذْ حَاشَا لِلهِ أَنْ يَرْتَكِبَ شَرّاً، وَالْقَدِيرِ أَنْ يُعَوِّجَ الْقَضَاءَ. 13مَنْ وَكَّلَ اللهَ بِالأَرْضِ؟ وَمَنْ عَهِدَ إِلَيْهِ بِالْمَسْكُونَةِ؟ 14إِنِ اسْتَرْجَعَ رُوحَهُ إِلَيْهِ وَاسْتَجْمَعَ نَسَمَتَهُ إِلَى نَفْسِهِ 15فَالْبَشَرُ جَمِيعاً يَفْنَوْنَ مَعاً، وَيَعُودُ الإِنْسَانُ إِلَى التُّرَابِ.

16فَإِنْ كُنْتَ مِنْ أُولِي الْفَهْمِ، فَاسْتَمِعْ إِلَى هَذَا، وَأَنْصِتْ لِمَا أَقُولُ: 17أَيُمْكِنُ لِمُبْغِضِ الْعَدْلِ أَنْ يَحْكُمَ؟ أَتَدِينُ الْبَارَّ الْقَدِيرَ؟ 18الَّذِي يَقُولُ لِلْمَلِكِ: أَنْتَ عَدِيمُ الْقِيمَةِ، وَلِلنُّبَلاءِ: أَنْتُمْ أَشْرَارٌ؟ 19الَّذِي لَا يُحَابِي الأُمَرَاءَ، وَلا يُؤْثِرُ الأَغْنِيَاءَ عَلَى الْفُقَرَاءِ، لأَنَّهُمْ جَمِيعاً عَمَلُ يَدَيْهِ. 20فِي لَحْظَةٍ يَمُوتُونَ، تُفَاجِئُهُمُ الْمَنِيَّةُ فِي مُنْتَصَفِ اللَّيْلِ، تَتَزَعْزَعُ الشُّعُوبُ فَيَفْنَوْنَ، وَيُسْتَأْصَلُ الأَعِزَّاءُ مِنْ غَيْرِ عَوْنٍ بَشَرِيٍّ، 21لأَنَّ عَيْنَيْهِ عَلَى طُرُقِ الإِنْسَانِ وَهُوَ يُرَاقِبُ خَطْوَاتِهِ. 22لَا تُوجَدُ ظُلْمَةٌ، وَلا ظِلُّ مَوْتٍ، يَتَوَارَى فِيهِمَا فَاعِلُو الإِثْمِ، 23لأَنَّهُ لَا يَحْتَاجُ أَنْ يَفْحَصَ الإِنْسَانَ مَرَّةً أُخْرَى حَتَّى يَدْعُوهُ لِلْمُثُولِ أَمَامَهُ فِي مُحَاكَمَةٍ. 24يُحَطِّمُ الأَعِزَّاءَ مِنْ غَيْرِ إِجْرَاءِ تَحْقِيقٍ، وَيُقِيمُ آخَرِينَ مَكَانَهُمْ 25لِذَلِكَ هُوَ مُطَّلِعٌ عَلَى أَعْمَالِهِمْ، فَيُطِيحُ بِهِمْ فِي اللَّيْلِ فَيُسْحَقُونَ. 26يَضْرِبُهُمْ لِشَرِّهِمْ عَلَى مَرْأَى مِنَ النَّاسِ، 27لأَنَّهُمُ انْحَرَفُوا عَنِ اتِّبَاعِهِ، وَلَمْ يَتَأَمَّلُوا فِي طُرُقِهِ، 28فَكَانُوا سَبَباً فِي ارْتِفَاعِ صُرَاخِ الْبَائِسِ إِلَيْهِ، وَاللهُ يَسْتَجِيبُ اسْتِغَاثَةَ الْمِسْكِينِ. 29فَإِنْ هَيْمَنَ بِسَكِينَتِهِ فَمَنْ يَدِينُهُ؟ وَإِنْ وَارَى وَجْهَهُ فَمَنْ يُعَايِنُهُ؟ سَوَاءٌ أَكَانُوا شَعْباً أَمْ فَرْداً 30لِكَيْ لَا يَسُودَ الْفَاجِرُ، لِئَلّا تَعْثُرَ الأُمَّةُ.

31هَلْ قَالَ أَحَدٌ للهِ: لَقَدْ تَحَمَّلْتُ الْعِقَابَ فَلَنْ أَعُودَ إِلَى الإِسَاءَةِ؟ 32عَلِّمْنِي مَا لَا أَرَاهُ، وَإِنْ كُنْتُ قَدْ أَثِمْتُ فَإِنَّنِي عَنْهُ أَرْتَدِعُ. 33أَيُجْزِيكَ اللهُ إِذاً بِمُقْتَضَى رَأْيِكَ إِذَا رَفَضْتَ التَّوْبَةَ؟ لأَنَّ عَلَيْكَ أَنْتَ أَنْ تَخْتَارَ لَا أَنَا، فَأَخْبِرْنِي بِمَا تَعْرِفُ. 34إِنَّ ذَوِي الْفَهْمِ يُعْلِنُونَ، وَالْحُكَمَاءَ الَّذِينَ يُنْصِتُونَ إِلَى كَلامِي يَقُولُونَ لِي: 35إِنَّ أَيُّوبَ يَتَكَلَّمُ بِجَهْلٍ، وَكَلامُهُ يَفْتَقِرُ إِلَى التَّعَقُّلِ. 36يَا لَيْتَ أَيُّوبَ يُمْتَحَنُ أَقْسَى امْتِحَانٍ، لأَنَّهُ أَجَابَ كَمَا يُجِيبُ أَهْلُ الشَّرِّ. 37لَكِنَّهُ أَضَافَ إِلَى خَطِيئَتِهِ عِصْيَاناً، إِذْ يُصَفِّقُ بَيْنَنَا بِاحْتِقَارٍ، مُثَرْثِراً بِأَقْوَالٍ ضِدَّ اللهِ!»