Ayubu 31 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 31:1-40

131:1 Kum 5:18; Mt 5:18“Nimefanya agano na macho yangu

yasimtazame msichana kwa kumtamani.

231:2 Ay 16:19; 20:29Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu,

urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?

331:3 Ay 21:30; 34:22; Rum 2:9Je, si uharibifu kwa watu waovu,

maangamizi kwa wale watendao mabaya?

431:4 2Nya 16:9; Mit 5:21; Yer 32:19; Dan 4:37Je, yeye hazioni njia zangu

na kuihesabu kila hatua yangu?

531:5 Ay 15:31; Mik 2:11“Kama nimeishi katika uongo

au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,

631:6 Law 19:36; Ay 6:2Mungu na anipime katika mizani za uaminifu,

naye atajua kwamba sina hatia:

731:7 Ay 9:30; Hes 15:39; Eze 6:9; Mt 5:29; Mhu 11:9kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia,

kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu,

au kama mikono yangu imetiwa unajisi,

831:8 Law 26:16; Yn 4:37; Mik 6:15basi wengine na wale nilichokipanda,

nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.

931:9 Kum 11:16; Yak 1:14“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke,

au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,

1031:10 Kum 28:30; Yer 8:16; Mit 14:31basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine,

nao wanaume wengine walale naye.

1131:11 Law 20:10; Yn 8:4-5Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu,

naam, dhambi ya kuhukumiwa.

1231:12 Ay 15:30; 26:6Ni moto uwakao kwa Uharibifu;31:12 Kwa Kiebrania ni Abadon (Ay 26:6; Mit 15:11).

ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.

1331:13 Kut 21:2-11; Law 25:39-46“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu,

walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,

1431:14 Ay 33:5; Hos 9:7; Za 10:13, 15; Isa 10:3; Yer 5:31nitafanya nini Mungu atakaponikabili?

Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?

1531:15 Ay 10:3; Efe 6:9Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu,

si ndiye aliwaumba?

Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote

ndani ya mama zetu?

1631:16 Law 25:17; Ay 20:19; Yak 1:27“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao,

au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,

1731:17 Ay 6:27; 29:12kama nimekula chakula changu mwenyewe,

bila kuwashirikisha yatima;

1831:18 Isa 51:18lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya,

nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:

1931:19 Ay 22:6; 24:4; Isa 58:7kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo,

au mtu mhitaji asiye na mavazi

2031:20 Ay 29:13; Amu 6:37ambaye wala moyo wake haukunibariki

kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,

2131:21 Ay 22:7-9; Yak 1:27na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima,

nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,

2231:22 Hes 15:30; Za 10:15basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu,

nao na uvunjike kutoka kiungio chake.

2331:23 Ay 10:3; 13:11; Mwa 20:11Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu,

nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.

2431:24 Ay 22:25; Mk 10:24; Lk 12:15“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu,

au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’

2531:25 Mwa 12:16; Isa 10:14kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu,

ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,

2631:26 Hes 11:20; Kum 4:19; Eze 8:16kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake

au mwezi ukienda kwa fahari yake,

2731:27 Ay 24:15; Yak 1:14; Yer 8:2; 16:11hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri,

au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,

2831:28 Mwa 38:24; Kum 17:2-7; Yos 24:23-27; Mit 30:9basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa,

kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.

2931:29 Za 35:15; Mt 5:44; Mit 17:5; 24:17-18“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu,

au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,

30lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi

kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;

31kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema,

‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’

3231:32 Amu 19:20; Mt 25:35; Ebr 13:2; 1Pet 4:9Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani,

kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;

3331:33 Za 32:5; Mit 28:13; Mwa 3:8kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo,

kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,

3431:34 Kut 23:2; Mit 29:25kwa sababu ya kuogopa umati wa watu,

na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa,

nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:

35(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia!

Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu:

Mwenyezi na anijibu;

mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.

36Hakika ningeyavaa begani mwangu,

ningeyavaa kama taji.

3731:37 Ay 1:3; 21:28Ningempa hesabu ya kila hatua yangu,

ningemwendea kama mwana wa mfalme.)

3831:38 Mwa 4:10“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu,

na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,

3931:39 1Fal 21:19; Law 19:13; Yak 5:4kama nimekula mazao yake bila malipo,

au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,

4031:40 Mwa 3:18; Mit 13:7basi miiba na iote badala ya ngano,

na magugu badala ya shayiri.”

Mwisho wa maneno ya Ayubu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约伯记 31:1-40

约伯最后的申辩

1“我跟自己的眼睛立了约,

决不贪看女色。

2天上的上帝所定的是什么?

高天的全能者赐下什么产业?

3岂不是降灾难给不义之人,

降祸患给作恶的人?

4上帝岂不鉴察我走的路,

数算我的脚步?

5我何曾与虚假同行,

疾步追随诡诈?

6愿上帝把我放在公义的天平上称量,

让祂知道我的清白。

7倘若我的脚偏离正路,

贪图眼目之欲,

或手上粘着罪污,

8愿我种的庄稼被别人享用,

我田中的出产被连根拔起。

9我的心若迷恋女人,

在邻居的门口窥探,

10愿我妻子为别人推磨,

愿别人与她同房。

11因为这是大恶,

是当受审判的罪,

12是烧向灭亡的火焰,

会吞噬我所有家业。

13我的仆婢告我,

我也会讲公道,

14否则上帝追究,我怎么办?

祂审问我,我如何回答?

15祂创造了我,岂不也创造了他们?

岂不是同一位使我们在母腹中成胎?

16我何曾拒绝穷人的请求,

或使寡妇眼露失望之情,

17或独吞我的食物,

不与孤儿同享?

18我自幼就如父亲般抚养孤儿,

我自出母胎就照顾寡妇。

19倘若我见有人冻得要死,

或有穷人衣不蔽体,

20却没有把我的羊毛给他们御寒,

以致他们向我道谢;

21倘若我仗着在城门口有势力,

就动手欺负孤儿,

22情愿我的肩膀从肩胛脱落,

我的手臂从手肘折断。

23因为我惧怕上帝降灾祸,

我无法承担祂的威严。

24“我若仰仗金子,

依靠纯金,

25因财富充裕、

或家产丰足而欢喜;

26我若见太阳发光,

明月在天上移动,

27就暗自心生迷恋,

向它们吻手示敬,

28就是犯了当受审判的罪恶,

因为这等于我背弃了天上的上帝。

29“我何曾因敌人遭殃而欢喜,

因他们遇祸而快乐?

30我从未咒诅他们丧命,

以致我的口犯罪。

31住在我帐篷中的人,

谁没饱餐我的肉食呢?

32我的家门向路人敞开,

从未有旅客露宿街头。

33我何曾像亚当一样遮掩我的过犯,

将罪恶藏在怀中,

34因惧怕群众,

被族人藐视,

就默不作声、不敢出门?

35“但愿有人听我申诉!

看啊,我在这里画押,愿全能者回答我!

愿我的控诉者写好状词!

36我会把状词披在肩上,

如冠冕一般戴在头上。

37我会像王者一样到祂面前,

向祂交代我的一切所为。

38“若我的田地向我喊冤,

条条犁沟一同哭诉;

39若我白吃地的出产,

或使地的主人丧命,

40愿地长出蒺藜而非麦子,

长出杂草而非大麦。”

约伯的话说完了。