Ayubu 30 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 30:1-31

130:1 Ay 12:4; Za 119:21“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki,

watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau

kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.

2Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu,

kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?

330:3 Isa 8:21; Ay 24:5; Yer 17:6Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa,

walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.

430:4 Ay 39:6; 1Fal 19:4Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi,

nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.

5Walifukuzwa mbali na watu wao,

wakipigiwa kelele kama wevi.

630:6 Isa 2:19; Hos 10:8Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka,

kwenye majabali na mahandaki.

730:7 Ay 6:5; 39:5-6Kwenye vichaka walilia kama punda,

na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.

830:8 Amu 9:4; Ay 18:18Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya,

waliofukuzwa watoke katika nchi.

930:9 Ay 16:10; 12:4; Za 69:11; Mao 3:14; Ay 16:10; Za 69:11; Ay 12:4; Mao 3:14, 63; Ay 17:6“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo;

nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.

1030:10 Hes 12:14; Mt 26:67Wananichukia sana na kujitenga nami,

wala hawasiti kunitemea mate usoni.

1130:11 Mwa 12:17; Rut 1:21; Ay 41:13; Za 32:9Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa,

wamekuwa huru kunitendea waonavyo.

1230:12 Za 109:6; Zek 3:1; Za 140:4-5; Ay 16:10Kuume kwangu kundi linashambulia;

wao huitegea miguu yangu tanzi,

na kunizingira.

1330:13 Isa 3:12; Za 69:26Huizuia njia yangu,

nao hufanikiwa katika kuniletea maafa,

nami sina yeyote wa kunisaidia.

14Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana;

katikati ya magofu huja na kunishambulia.

1530:15 Kut 3:6; Za 55:4-5; Hos 13:3; Ay 3:25Vitisho vimenifunika;

heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo,

salama yangu imetoweka kama wingu.

1630:16 Za 22:14; Isa 53:12“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho;

siku za mateso zimenikamata.

17Usiku mifupa yangu inachoma;

maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.

18Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo;

hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.

1930:19 Za 40:2; Yer 38:6, 22Yeye amenitupa kwenye matope,

nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.

2030:20 Ay 19:7; Mao 3:8; Mt 15:23“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu;

ninasimama, nawe unanitazama tu.

2130:21 Ay 19:6; Yer 6:23; Isa 9:12; Eze 6:14; Ay 10:3Wewe unanigeukia bila huruma;

unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.

2230:22 Ay 27:21; 9:17; Yud 12Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo;

umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.

2330:23 2Sam 14:14; Ay 3:19; 10:8Ninajua utanileta mpaka kifoni,

mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.

24“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji,

anapoomba msaada katika shida yake.

2530:25 Za 35:13-14; Rum 12:15; Yn 11:35Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu?

Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?

2630:26 Za 82:5; Yer 8:15Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia;

nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.

2730:27 Za 38:8; Mao 2:11Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii;

siku za mateso zinanikabili.

2830:28 Mao 4:8; Za 38:6; Ay 19:7; 24:12Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua;

ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.

2930:29 Isa 34:13; Yer 9:11; Za 102:6; Mik 1:8Nimekuwa ndugu wa mbweha,

rafiki wa mabundi.

3030:30 Mao 3:4; 4:8; 5:10; Kum 28:35Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika;

mifupa yangu inaungua kwa homa.

3130:31 Mwa 8:8; Za 137:2Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo,

nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

King James Version

Job 30:1-31

1But now they that are younger than I have me in derision, whose fathers I would have disdained to have set with the dogs of my flock.30.1 younger…: Heb. of fewer days than I 2Yea, whereto might the strength of their hands profit me, in whom old age was perished? 3For want and famine they were solitary; fleeing into the wilderness in former time desolate and waste.30.3 solitary: or, dark as the night30.3 in…: Heb. yesternight 4Who cut up mallows by the bushes, and juniper roots for their meat. 5They were driven forth from among men, (they cried after them as after a thief;) 6To dwell in the clifts of the valleys, in caves of the earth, and in the rocks.30.6 caves: Heb. holes 7Among the bushes they brayed; under the nettles they were gathered together. 8They were children of fools, yea, children of base men: they were viler than the earth.30.8 base…: Heb. men of no name 9And now am I their song, yea, I am their byword. 10They abhor me, they flee far from me, and spare not to spit in my face.30.10 and…: Heb. and withhold not spittle from 11Because he hath loosed my cord, and afflicted me, they have also let loose the bridle before me. 12Upon my right hand rise the youth; they push away my feet, and they raise up against me the ways of their destruction. 13They mar my path, they set forward my calamity, they have no helper. 14They came upon me as a wide breaking in of waters: in the desolation they rolled themselves upon me.

15Terrors are turned upon me: they pursue my soul as the wind: and my welfare passeth away as a cloud.30.15 my soul: Heb. my principal one 16And now my soul is poured out upon me; the days of affliction have taken hold upon me. 17My bones are pierced in me in the night season: and my sinews take no rest. 18By the great force of my disease is my garment changed: it bindeth me about as the collar of my coat. 19He hath cast me into the mire, and I am become like dust and ashes. 20I cry unto thee, and thou dost not hear me: I stand up, and thou regardest me not. 21Thou art become cruel to me: with thy strong hand thou opposest thyself against me.30.21 become…: Heb. turned to be cruel30.21 thy…: Heb. the strength of thy hand 22Thou liftest me up to the wind; thou causest me to ride upon it, and dissolvest my substance.30.22 substance: or, wisdom 23For I know that thou wilt bring me to death, and to the house appointed for all living. 24Howbeit he will not stretch out his hand to the grave, though they cry in his destruction.30.24 grave: Heb. heap 25Did not I weep for him that was in trouble? was not my soul grieved for the poor?30.25 in trouble: Heb. hard of day? 26When I looked for good, then evil came unto me: and when I waited for light, there came darkness. 27My bowels boiled, and rested not: the days of affliction prevented me. 28I went mourning without the sun: I stood up, and I cried in the congregation. 29I am a brother to dragons, and a companion to owls.30.29 owls: or, ostriches 30My skin is black upon me, and my bones are burned with heat. 31My harp also is turned to mourning, and my organ into the voice of them that weep.