Ayubu 29 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 29:1-25

Ayubu Anamaliza Utetezi Wake

129:1 Za 18:28; Ay 13:12Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:

229:2 Yer 1:12; 44:27“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita,

zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,

329:3 Ay 11:17; 12:25wakati taa yake iliniangazia kichwani changu,

na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!

429:4 Za 25:14; Mit 3:32Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu,

wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,

529:5 Za 127:3-5; 128:3; Rum 4:1wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami,

nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,

629:6 Ay 20:17; Za 81:16; Mwa 49:20; Kum 32:13wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi,

nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.

729:7 Ay 5:4; 31:21; Yer 20:2; 38:7“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji

na kuketi katika kiwanja,

829:8 1Tim 5:1; Law 19:32vijana waliniona wakakaa kando,

nao wazee walioketi wakasimama;

929:9 Amu 16:19; Mit 30:32wakuu wakaacha kuzungumza

na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;

1029:10 Za 137:6wenye vyeo wakanyamazishwa,

nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.

1129:11 Ay 4:4; Ebr 11:4Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu,

nao walioniona walinisifu,

1229:12 Kum 24:17; Ay 31:17-21; Za 72:12; Mit 21:13kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada,

naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.

1329:13 Ay 31:20; 22:9; Kum 10:18Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki,

nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.

1429:14 2Sam 8:15; Rum 13:14; Efe 6:14Niliivaa haki kama vazi langu;

uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.

1529:15 Hes 10:31Nilikuwa macho ya kipofu

na miguu kwa kiwete.

1629:16 Ay 24:4; Mit 29:7Nilikuwa baba kwa mhitaji;

nilimtetea mgeni.

1729:17 Ay 24:9; 4:10, 11; Za 3:7Niliyavunja meno makali ya waovu,

na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.

1829:18 Za 62:2; Mit 3:1-2“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe,

nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.

1929:19 Hes 24:6; Yer 17:8Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji,

nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.

2029:20 Za 18:34; Isa 38:12; Mwa 49:24Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu,

upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’

2129:21 Ay 29:21“Watu walinisikiliza kwa tumaini,

wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.

2229:22 Kum 32:2Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi;

maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.

23Waliningojea kama manyunyu ya mvua

na kuyapokea maneno yangu

kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.

24Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha;

nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.

2529:25 Ay 31:31; 4:4Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao;

niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake;

nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

New International Version

Job 29:1-25

Job’s Final Defense

1Job continued his discourse:

2“How I long for the months gone by,

for the days when God watched over me,

3when his lamp shone on my head

and by his light I walked through darkness!

4Oh, for the days when I was in my prime,

when God’s intimate friendship blessed my house,

5when the Almighty was still with me

and my children were around me,

6when my path was drenched with cream

and the rock poured out for me streams of olive oil.

7“When I went to the gate of the city

and took my seat in the public square,

8the young men saw me and stepped aside

and the old men rose to their feet;

9the chief men refrained from speaking

and covered their mouths with their hands;

10the voices of the nobles were hushed,

and their tongues stuck to the roof of their mouths.

11Whoever heard me spoke well of me,

and those who saw me commended me,

12because I rescued the poor who cried for help,

and the fatherless who had none to assist them.

13The one who was dying blessed me;

I made the widow’s heart sing.

14I put on righteousness as my clothing;

justice was my robe and my turban.

15I was eyes to the blind

and feet to the lame.

16I was a father to the needy;

I took up the case of the stranger.

17I broke the fangs of the wicked

and snatched the victims from their teeth.

18“I thought, ‘I will die in my own house,

my days as numerous as the grains of sand.

19My roots will reach to the water,

and the dew will lie all night on my branches.

20My glory will not fade;

the bow will be ever new in my hand.’

21“People listened to me expectantly,

waiting in silence for my counsel.

22After I had spoken, they spoke no more;

my words fell gently on their ears.

23They waited for me as for showers

and drank in my words as the spring rain.

24When I smiled at them, they scarcely believed it;

the light of my face was precious to them.29:24 The meaning of the Hebrew for this clause is uncertain.

25I chose the way for them and sat as their chief;

I dwelt as a king among his troops;

I was like one who comforts mourners.