Ayubu 28 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 28:1-28

Mapumziko: Imani Inakopatikana

128:1 Za 12:6; 66:10; Yer 9:7; Mal 3:3; Dan 11:35“Kuna machimbo ya fedha,

na mahali dhahabu isafishwapo.

228:2 Kum 8:9Chuma hupatikana ardhini,

nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.

328:3 Mhu 7:25; 8:17; Mit 2:4Mwanadamu hukomesha giza;

huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali,

kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini

katika giza jeusi sana.

428:4 2Sam 5:8Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu,

mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu;

mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.

528:5 Mwa 1:29; Za 145:15Ardhi, ambako chakula hutoka,

chini hugeuzwa kwa moto;

628:6 Isa 54:11; Wim 5:14; Ay 22:24yakuti samawi hutoka katika miamba yake,

nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.

728:7 Ay 28:21Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika,

wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.

828:8 Ay 41:34; Isa 35:9Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga,

wala simba azungukaye huko.

928:9 Kum 8:15; Yn 2:6Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana,

na kuiacha wazi mizizi ya milima.

1028:10 Mit 2:4; Ay 28:4Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba;

macho yake huona hazina zake zote.

1128:11 Mwa 7:11; Isa 48:6; Yer 33:3Hutafuta vyanzo vya mito

na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.

1228:12 Mit 1:20; Mhu 7:24“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi?

Ufahamu unakaa wapi?

1328:13 Mit 3:15; Mt 13:44-46Mwanadamu hatambui thamani yake;

haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.

14Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’;

bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’

1528:15 Mit 16:16; Mdo 8:20Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote,

wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.

16Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri,

kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.

1728:17 Za 119:72; Mit 8:10; Ay 28:15Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo,

wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.

18Marijani na yaspi hazistahili kutajwa;

thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.

1928:19 Mit 3:14-15; 8:10-19Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,

wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.

20“Ni wapi basi hekima itokako?

Ufahamu hukaa wapi?

2128:21 Ay 28:7Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai,

imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.

2228:22 Ay 26:6Uharibifu na Mauti husema,

‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’

2328:23 Mdo 15:18; Ay 22:22; Mit 8:22-31Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima

na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,

2428:24 Isa 11:12; Yos 3:11; Ebr 4:13; Za 66:7kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia

na huona kila kitu chini ya mbingu.

2528:25 Ay 38:8-11; Za 135:7Alipofanyiza nguvu za upepo

na kuyapima maji,

2628:26 Ay 38:25-27; Isa 35:7; Yer 14:22alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua

na njia kwa ajili ya umeme wa radi,

27ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake,

akaithibitisha na kuihakikisha.

2828:28 Kut 20:20; Kum 4:6Naye Mungu akamwambia mwanadamu,

‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima,

nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’ ”

New International Reader’s Version

Job 28:1-28

The Place Where Wisdom Is Found Is Explained

1There are mines where silver is found.

There are places where gold is purified.

2Iron is taken out of the earth.

Copper is melted down from ore.

3Human beings light up the darkness.

They search for ore in the deepest pits.

They look for it in the blackest darkness.

4Far from where people live they cut a tunnel.

They do it in places where other people don’t go.

Far away from people they swing back and forth on ropes.

5Food grows on the surface of the earth.

But far below, the earth is changed as if by fire.

6Lapis lazuli is taken from the rocky earth.

Its dust contains nuggets of gold.

7No bird knows that hidden path.

No falcon’s eye has seen it.

8Proud animals don’t walk on it.

Lions don’t prowl there.

9Human hands attack the hardest rock.

Their strong hands uncover the base of the mountains.

10They tunnel through the rock.

Their eyes see all its treasures.

11They search the places where the rivers begin.

They bring hidden things out into the light.

12But where can wisdom be found?

Where does understanding live?

13No human being understands how much it’s worth.

It can’t be found anywhere in the world.

14The ocean says, “It’s not in me.”

The sea says, “It’s not here either.”

15It can’t be bought with the finest gold.

Its price can’t be weighed out in silver.

16It can’t be bought with gold from Ophir.

It can’t be bought with priceless onyx or lapis lazuli.

17Gold or crystal can’t compare with it.

It can’t be bought with jewels made of gold.

18Don’t bother to talk about coral and jasper.

Wisdom is worth far more than rubies.

19A topaz from Cush can’t compare with it.

It can’t be bought with the purest gold.

20So where does wisdom come from?

Where does understanding live?

21It’s hidden from the eyes of every living thing.

Even the birds in the sky can’t find it.

22Death and the Grave say,

“Only reports about it have reached our ears.”

23But God understands the way to it.

He is the only one who knows where it lives.

24He sees from one end of the earth to the other.

He views everything in the world.

25He made the mighty wind.

He measured out the waters.

26He gave orders for the rain to fall.

He made paths for the thunderstorms.

27Then he looked at wisdom and set its price.

He established it and tested it.

28He said to human beings,

“Have respect for the Lord. That will prove you are wise.

Avoid evil. That will show you have understanding.”