Ayubu 24 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 24:1-25

Ayubu Analalamikia Jeuri Duniani

124:1 Yer 46:10; 2Pet 3:7; Ay 15:20; Mdo 1:7“Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu?

Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?

224:2 Kum 19:14; 27:17; Mit 23:10Watu husogeza mawe ya mpaka;

huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.

324:3 Kum 24:6-10; 12:17; Ay 6:27Huwanyangʼanya yatima punda wao,

na kumchukua rehani fahali wa mjane.

424:4 Mit 28:28; Ay 20:19; Isa 11:4; Za 12:5Humsukuma mhitaji kutoka njia,

na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.

524:5 Mwa 16:12; Za 104:23; Ay 30:3Kama punda-mwitu jangwani,

maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula;

mahali palipo jangwa

huwapa chakula cha watoto wao.

624:6 Ay 6:5; Rut 2:22; 1Fal 21:19Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo

katika mashamba ya mizabibu ya waovu.

724:7 Kut 22:26-27; Kum 24:12; Ay 22:6Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi;

hawana chochote cha kujifunika baridi.

824:8 Dan 4:25, 33; Mao 4:5Hutota kwa mvua za mlimani,

nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.

924:9 Kum 24:17Mtoto yatima hupokonywa matitini;

mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.

1024:10 Kum 24:12-13; Law 19:9Kwa kukosa nguo, hutembea uchi;

hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.

1124:11 Isa 5:2; 16:10; Hag 2:16; Mik 6:15Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia;

hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.

1224:12 Isa 30:19; Ay 9:23; Ufu 6:10; Mhu 8:11Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini,

nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada.

Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote

kwa kutenda mabaya.

1324:13 Ay 38:15; 1The 5:4-5; Za 18:28; Efe 5:8-14“Wako wale wanaoiasi nuru,

wasiofahamu njia zake

wala hawakai katika mapito yake.

1424:14 Isa 3:15; Mik 3:3; Ay 20:19; Za 37:32; 10:9Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka

naye huwaua maskini na mhitaji;

wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.

1524:15 Mit 7:8-9; Za 10:11Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza,

naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’

naye huuficha uso wake.

1624:16 Kut 22:2; Mt 6:19; Yn 3:20Katika giza, huvunja majumba,

lakini wakati wa mchana hujifungia ndani;

hawataki kufanya lolote nuruni.

1724:17 Ay 18:11; 15:22; 18:5Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao;

hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.

1824:18 Ay 9:26; 22:16; Yud 23; Isa 57:20“Lakini wao ni povu juu ya maji;

sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa,

hivyo hakuna hata mmoja

aendaye kwenye shamba la mizabibu.

1924:19 Ay 6:17; 21:13Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka,

ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi.

2024:20 Ay 18:17; Mit 10:7; Dan 4:14; Za 31:12Tumbo lililowazaa huwasahau,

nao huwa karamu ya mabuu;

watu waovu hawakumbukwi tena,

lakini huvunjika kama mti.

2124:21 Ay 22:9Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto,

nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.

2224:22 Kum 28:66; Mt 6:27Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake;

ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.

2324:23 Ay 9:24; Amo 6:1; 2Nya 16:9; Ay 10:4Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama,

lakini macho yake yanaona njia zao.

2424:24 2Fal 19:35; Za 37:35-36; 83:13; Isa 17:5Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka;

hushushwa na kukusanywa kama wengine wote,

hukatwa kama masuke ya nafaka.

2524:25 Ay 16:17; 27:4“Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo,

na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”

King James Version

Job 24:1-25

1Why, seeing times are not hidden from the Almighty, do they that know him not see his days? 2Some remove the landmarks; they violently take away flocks, and feed thereof.24.2 feed…: or, feed them 3They drive away the ass of the fatherless, they take the widow’s ox for a pledge. 4They turn the needy out of the way: the poor of the earth hide themselves together. 5Behold, as wild asses in the desert, go they forth to their work; rising betimes for a prey: the wilderness yieldeth food for them and for their children. 6They reap every one his corn in the field: and they gather the vintage of the wicked.24.6 corn: Heb. mingled corn, or, dredge24.6 they gather…: Heb. the wicked gather the vintage 7They cause the naked to lodge without clothing, that they have no covering in the cold. 8They are wet with the showers of the mountains, and embrace the rock for want of a shelter. 9They pluck the fatherless from the breast, and take a pledge of the poor. 10They cause him to go naked without clothing, and they take away the sheaf from the hungry; 11Which make oil within their walls, and tread their winepresses, and suffer thirst. 12Men groan from out of the city, and the soul of the wounded crieth out: yet God layeth not folly to them.

13They are of those that rebel against the light; they know not the ways thereof, nor abide in the paths thereof. 14The murderer rising with the light killeth the poor and needy, and in the night is as a thief. 15The eye also of the adulterer waiteth for the twilight, saying, No eye shall see me: and disguiseth his face.24.15 disguiseth…: Heb. setteth his face in secret 16In the dark they dig through houses, which they had marked for themselves in the daytime: they know not the light. 17For the morning is to them even as the shadow of death: if one know them, they are in the terrors of the shadow of death.

18He is swift as the waters; their portion is cursed in the earth: he beholdeth not the way of the vineyards. 19Drought and heat consume the snow waters: so doth the grave those which have sinned.24.19 consume: Heb. violently take 20The womb shall forget him; the worm shall feed sweetly on him; he shall be no more remembered; and wickedness shall be broken as a tree. 21He evil entreateth the barren that beareth not: and doeth not good to the widow. 22He draweth also the mighty with his power: he riseth up, and no man is sure of life.24.22 no…: or, he trusteth not his own life 23Though it be given him to be in safety, whereon he resteth; yet his eyes are upon their ways. 24They are exalted for a little while, but are gone and brought low; they are taken out of the way as all other, and cut off as the tops of the ears of corn.24.24 are gone: Heb. are not24.24 taken…: Heb. closed up 25And if it be not so now, who will make me a liar, and make my speech nothing worth?