Ayubu 20 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 20:1-29

Sofari Anasema: Uovu Hupokea Malipo Ya Haki

120:1 Ay 2:11Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:

220:2 Za 42:5; Mao 1:20“Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu,

kwa sababu nimehangaika sana.

320:3 Ay 19:3Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima,

nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.

420:4 Kum 4:32; Ay 32:7“Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani,

tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,

520:5 Ay 8:12; Za 73:19; 37:35macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi,

nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.

620:6 Ay 33:17; Isa 16:6; Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Oba 1:3-4Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni

na kichwa chake hugusa mawingu,

720:7 Ay 4:20; 7:8; 14:20ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe.

Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’

820:8 Za 90:5; 73:20; Mhu 6:12; 12:7; Ay 18:11-18; Isa 17:14; 29:7Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena,

amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.

920:9 Ay 7:8Jicho lililomwona halitamwona tena;

mahali pake hapatamwona tena.

1020:10 Ay 5:4; 20:15, 18, 20; 3:15Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini,

nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.

1120:11 Ay 13:26; 21:24; 17:16Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake,

zitalala naye mavumbini.

1220:12 Ay 15:16; Za 10:7; 140:3“Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake

naye huuficha chini ya ulimi wake,

1320:13 Hes 11:18-20ingawa hawezi kukubali kuuachia uende,

lakini huuweka kinywani mwake.

1420:14 Za 104:26; Ay 10:18; Mwa 1:21; Ay 41:1, 8, 10, 2520:14 Mit 20:17; Yer 2:19; 4:18; Ufu 10:9; Hes 21:6Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake,

nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.

1520:15 Ay 20:10; Law 18:25Atatema mali alizozimeza;

Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.

1620:16 Kum 32:24, 34Atanyonya sumu za majoka;

meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.

1720:17 Kum 32:13-14; Ay 29:6; Yer 17:6Hatafurahia vijito,

mito inayotiririsha asali na siagi.

1820:18 Ay 20:10; 5:5; Za 109:11Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila;

hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.

1920:19 Kum 15:11; Amo 8:4Kwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu;

amenyangʼanya kwa nguvu nyumba asizozijenga.

2020:20 Mhu 5:12-14“Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana;

hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.

2120:21 Ay 7:8Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale;

kufanikiwa kwake hakutadumu.

2220:22 Amu 2:15; Lk 2:16-20; Ay 20:29; 21:17, 30; 31:2-3Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata;

taabu itamjia kwa nguvu zote.

2320:23 Za 78:30-31Atakapokuwa amelijaza tumbo lake,

Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake,

na kumnyeshea mapigo juu yake.

2420:24 Yer 46:21; Amo 5:19; Isa 24:18Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma,

mshale wa shaba utamchoma.

2520:25 Ay 18:11; 16:13; Za 88:15-16Atauchomoa katika mgongo wake,

ncha ingʼaayo kutoka ini lake.

Vitisho vitakuja juu yake;

2620:26 Ay 5:14; 1:16; 15:34; 26:6; 28:22; 31:12; Za 21:9giza nene linavizia hazina zake.

Moto usiopepewa na mtu utamteketeza,

na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.

2720:27 Kum 31:28; Isa 26:21Mbingu zitaweka wazi hatia yake,

nayo nchi itainuka kinyume chake.

2820:28 Kum 28:31; Mt 7:26-27; Hes 14:28-32; Efe 5:6Mafuriko yataichukua nyumba yake,

maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.

2920:29 Yer 13:25; Kum 29:20, 28; Ufu 21:8; Mt 24:51Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu,

urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”

Ketab El Hayat

أيوب 20:1-29

صوفر

1فَأَجَابَ صُوفَرُ النَّعْمَاتِيُّ: 2«إِنَّ خَوَاطِرِي، مِنْ جَرَّاءِ كَلامِكَ، تَحْفِزُنِي لِلْكَلامِ وَتُثِيرُنِي لِلرَّدِّ عَلَيْكَ. 3سَمِعْتُ تَوْبِيخاً يُعَيِّرُنِي، وَأَجَابَنِي رُوحٌ مِنْ فِطْنَتِي.

4أَمَا عَلِمْتَ هَذَا مُنْذُ الْقِدَمِ، مُنْذُ أَنْ خُلِقَ الإِنْسَانُ عَلَى الأَرْضِ، 5أَنَّ طَرَبَ الشِّرِّيرِ إِلَى حِينٍ، وَأَنَّ فَرَحَ الْفَاجِرِ إِلَى لَحْظَةٍ؟ 6مَهْمَا بَلَغَتْ كِبْرِيَاؤُهُ السَّمَاوَاتِ وَمَسَّتْ هَامَتُهُ الْغَمَامَ، 7فَإِنَّهُ سَيَبِيدُ كَبِرَازِهِ، فَيَتَسَاءَلُ الَّذِينَ يَعْرِفُونَهُ، مُنْدَهِشِينَ: أَيْنَ هُوَ؟ 8يَتَلاشَى كَحُلْمٍ وَلا يَبْقَى مِنْهُ أَثَرٌ، وَيَضْمَحِلُّ كَرُؤْيَا اللَّيْلِ، 9وَالْعَيْنُ الَّتِي أَبْصَرَتْهُ لَا تَعُودُ تَرَاهُ ثَانِيَةً، وَلا يُعَايِنُهُ مَكَانُهُ فِيمَا بَعْدُ. 10يَسْتَجْدِي أَوْلادُهُ مِنَ الْفُقَرَاءِ، وَتَرُدُّ يَدَاهُ ثَرْوَتَهُ المَسْلُوبَةَ. 11حَيَوِيَّةُ عِظَامِهِ تُدْفَنُ فِي عِزِّ قُوَّتِهِ، 12يَتَذَوَّقُ الشَّرَّ فَيَحْلُو فِي فَمِهِ، فَيُبْقِيهِ تَحْتَ لِسَانِهِ، 13وَيَمْقُتُ أَنْ يَقْذِفَهُ، بَلْ يَدَّخِرُهُ فِي فَمِهِ! 14فَيَتَحَوَّلُ طَعَامُهُ فِي أَمْعَائِهِ إِلَى مَرَارَةٍ كَالسُّمُومِ. 15وَيَتَقَيَّأُ مَا ابْتَلَعَهُ مِنْ أَمْوَالٍ، وَيَسْتَخْرِجُهَا اللهُ مِنْ جَوْفِهِ. 16لَقَدْ رَضَعَ سُمَّ الصِّلِّ، فَقَتَلَهُ لِسَانُ الأَفْعَى. 17لَنْ تَكْتَحِلَ عَيْنَاهُ بِمَرْأَى الأَنْهَارِ الْجَارِيَةِ، وَلا بِالْجَدَاوِلِ الْفَيَّاضَةِ بِالْعَسَلِ وَالزُّبْدِ. 18يَرُدُّ ثِمَارَ تَعَبِهِ وَلا يَبْلَعُهُ وَلا يَسْتَمْتِعُ بِكَسْبِ تِجَارَتِهِ. 19لأَنَّهُ هَضَمَ حَقَّ الْفُقَرَاءِ وَخَذَلَهُمْ وَسَلَبَ بُيُوتاً لَمْ يَبْنِهَا.

20وَإِذْ لَا يَعْرِفُ طَمَعُهُ قَنَاعَةً، فَإِنَّهُ لَنْ يَدَّخِرَ شَيْئاً يَسْتَمْتِعُ بِهِ. 21لَمْ يُبْقِ نَهَمُهُ عَلَى شَيْءٍ، لِذَلِكَ لَنْ يَدُومَ خَيْرُهُ. 22فِي وَفْرَةِ سِعَتِهِ يُصِيبُهُ الضَّنْكُ، وَتَحُلُّ بِهِ أَقْسَى الْكَوَارِثِ. 23وَعِنْدَمَا يَمْلأُ بَطْنَهُ يَنْفُثُ عَلَيْهِ اللهُ غَضَبَهُ الْحَارِقَ وَيُمْطِرُهُ عَلَيْهِ طَعَاماً لَهُ. 24إِنْ فَرَّ مِنْ آلَةِ حَرْبٍ مِنْ حَدِيدٍ، تَخْتَرِقْهُ قَوْسُ النُّحَاسِ. 25اخْتَرَقَتْهُ عَمِيقاً وَخَرَجَتْ مِنْ جَسَدِهِ، وَنَفَذَ حَدُّهَا اللّامِعُ مِنْ مَرَارَتِهِ، وَحَلَّ بِهِ رُعْبٌ. 26كُلُّ ظُلْمَةٍ تَتَرَبَّصُ بِذَخَائِرِهِ، وَتَأْكُلُهُ نَارٌ لَمْ تُنْفَخْ، وَتَلْتَهِمُ مَا بَقِيَ مِنْ خَيْمَتِهِ. 27تَفْضَحُ السَّمَاوَاتُ إِثْمَهُ، وَتَتَمَرَّدُ الأَرْضُ عَلَيْهِ، 28تَفْنَى مُدَّخَرَاتُ بَيْتِهِ وَتحْتَرِقُ فِي يَوْمِ غَضَبِ الرَّبِّ. 29هَذَا هُوَ الْمَصِيرُ الَّذِي يُعِدُّهُ اللهُ للأَشْرَارِ، وَالْمِيرَاثُ الَّذِي كَتَبَهُ اللهُ لَهُمْ».