Ayubu 2 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 2:1-13

Jaribu La Pili La Ayubu

12:1 Ay 1:6; Mwa 6:2Siku nyingine wana wa Mungu walikuja kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao kujionyesha mbele zake. 22:2 Mwa 3:1Bwana akamuuliza Shetani, “Umetoka wapi?”

Shetani akamjibu Bwana “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”

32:3 Kut 20:20; Ay 6:29; 9:17; 13:18; Yak 1:12; Za 44:17; Ay 13:18; 27:5, 6; 1Pet 1:7; Mt 7:11; Yn 9:2Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, mtu asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Naye bado anadumisha uadilifu wake, ingawa ulinichochea dhidi yake, ili nimwangamize pasipo sababu.”

42:4 Ay 1:10Shetani akamjibu Bwana, “Ngozi kwa ngozi! Mwanadamu atatoa vyote alivyo navyo kwa ajili ya uhai wake. 52:5 Za 102:5; Ay 19:20; Mao 4:8; Za 32:3, 4; Ay 16:8; 1:11Lakini nyoosha mkono wako na kuipiga nyama yake na mifupa yake, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”

62:6 Ay 1:12; 2Kor 12:7Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, yeye yumo mikononi mwako, lakini lazima umwachie uhai wake.”

72:7 Kum 28:35; Ay 7:5; 16:16Basi Shetani akatoka mbele za Bwana naye akampiga Ayubu kwa majipu mabaya tangu nyayo za miguu yake hadi utosi wa kichwa. 82:8 2Sam 13:19; Za 7:5; Mt 11:21; Mwa 18:27; Es 4:3; Ay 16:15; 19:9; 42:6; Isa 5:8; 6:13; Yer 6:26; Mao 3:29; Eze 26:16; Yon 3:5-8Ndipo Ayubu akachukua kigae na kujikuna nacho huku akiketi kwenye majivu.

92:9 Ay 1:21; 13:15; 27:5; 33:9; 35:2; 1The 5:8; Kut 20:7; 2Fal 6:33Mke wake akamwambia, “Je, bado unashikamana na uadilifu wako? Mlaani Mungu nawe ukafe!”

102:10 Mhu 2:24; Mao 3:38-41; Yak 5:11; Za 39:1Akamjibu, “Unazungumza kama vile ambavyo mwanamke mpumbavu2:10 Mpumbavu hapa ina maana ya kupungukiwa maadili. yeyote angenena. Je, tupokee mema mikononi mwa Mungu, nasi tusipokee na udhia?”

Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi katika kusema kwake.

Marafiki Watatu Wa Ayubu

112:11 Mwa 25:2; 36:11; 37:35; Yer 49:7; Rum 12:15; Ay 11:1; 20:1; Yn 11:19Basi marafiki watatu wa Ayubu, ndio Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi na Sofari Mnaamathi, waliposikia juu ya taabu yote iliyompata Ayubu, wakajipanga toka manyumbani mwao, nao wakakutana pamoja kwa makubaliano kwenda kumtuliza katika taabu hiyo na kumfariji. 122:12 2Sam 1:2; Neh 9:1; Eze 27:30; Ay 17:7; Isa 52:14; Mwa 37:29; Mk 14:63; Yos 7:6Walipomwona kwa mbali, ilikuwa vigumu kumtambua. Wakaanza kulia kwa sauti kubwa, wakayararua majoho yao na kujirushia mavumbi juu ya vichwa vyao. 132:13 Mwa 50:10-12; Eze 3:15; Isa 3:26; 47:1; Eze 26:16; Yn 3:6; Hag 2:22; Mit 17:28; Isa 23:2; 47:5Kisha wakaketi chini kwenye udongo pamoja na Ayubu kwa siku saba usiku na mchana. Hakuna yeyote aliyesema naye neno, kwa sababu waliona jinsi mateso yake yalivyokuwa makubwa.

New International Version – UK

Job 2:1-13

1On another day the angels2:1 Hebrew the sons of God came to present themselves before the Lord, and Satan also came with them to present himself before him. 2And the Lord said to Satan, ‘Where have you come from?’

Satan answered the Lord, ‘From roaming throughout the earth, going to and fro on it.’

3Then the Lord said to Satan, ‘Have you considered my servant Job? There is no-one on earth like him; he is blameless and upright, a man who fears God and shuns evil. And he still maintains his integrity, though you incited me against him to ruin him without any reason.’

4‘Skin for skin!’ Satan replied. ‘A man will give all he has for his own life. 5But now stretch out your hand and strike his flesh and bones, and he will surely curse you to your face.’

6The Lord said to Satan, ‘Very well, then, he is in your hands; but you must spare his life.’

7So Satan went out from the presence of the Lord and afflicted Job with painful sores from the soles of his feet to the crown of his head. 8Then Job took a piece of broken pottery and scraped himself with it as he sat among the ashes.

9His wife said to him, ‘Are you still maintaining your integrity? Curse God and die!’

10He replied, ‘You are talking like a foolish2:10 The Hebrew word rendered foolish denotes moral deficiency. woman. Shall we accept good from God, and not trouble?’

In all this, Job did not sin in what he said.

11When Job’s three friends, Eliphaz the Temanite, Bildad the Shuhite and Zophar the Naamathite, heard about all the troubles that had come upon him, they set out from their homes and met together by agreement to go and sympathise with him and comfort him. 12When they saw him from a distance, they could hardly recognise him; they began to weep aloud, and they tore their robes and sprinkled dust on their heads. 13Then they sat on the ground with him for seven days and seven nights. No-one said a word to him, because they saw how great his suffering was.