Ayubu 16 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 16:1-22

Hotuba Ya Tano Ya Ayubu

Ayubu Anathibitisha Tena Hali Yake Ya Kutokuwa Na Hatia

1Kisha Ayubu akajibu:

216:2 Ay 6:15; 13:4; Za 69:20“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya,

nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!

316:3 Ay 6:26; 11:2; 18:2Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho?

Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?

416:4 Mt 27:29; Yer 18:16; Mao 2:15Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi,

kama mngekuwa katika hali yangu;

ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu,

na kuwatikisia ninyi kichwa changu.

516:5 Ay 29:25; Mwa 37:35Lakini kinywa changu kingewatia moyo;

faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.

616:6 Ay 6:3; 7:21“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi;

nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.

716:7 Amu 8:5; Ay 7:3; 1:19Ee Mungu, hakika umenichakaza;

umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.

816:8 Mao 5:17; Ay 10:17; 17:7; 19:20; Za 22:17; 88:9; 6:7Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi;

nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.

916:9 Ay 12:14; 13:24; Mao 2:16; Mdo 7:54; Hos 6:1; Ay 30:21; 9:5; 18:4; 19:11Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake,

na kunisagia meno yake;

adui yangu hunikazia macho yake makali.

1016:10 Za 22:13; Mao 3:30; Mdo 7:57; 23:2; Za 27:3; Mik 5:1Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki;

hunipiga shavuni mwangu kwa dharau,

na kuungana pamoja dhidi yangu.

1116:11 Ay 9:24Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya,

na kunitupa katika makucha ya waovu.

1216:12 Ay 9:17; 6:4; Mao 3:12Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja;

amenikamata shingo na kuniponda.

Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;

1316:13 Mit 7:23; Mao 3:13wapiga upinde wake wananizunguka.

Bila huruma, huchoma figo zangu,

na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.

1416:14 Ay 9:17; 10:3; Yoe 2:7Huniponda tena na tena;

hunishambulia kama shujaa wa vita.

1516:15 Mwa 37:34; Ay 2:8“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu

nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.

1616:16 Ay 16:20; 2:7; 17:7; 30:17, 30; Isa 52:14; Za 6:6Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia,

macho yangu yamepigwa na giza kuu.

1716:17 Yer 18:11; Yon 3:8Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri,

na maombi yangu ni safi.

1816:18 Mwa 4:10; Ay 27:9; Isa 26:21; Za 66:18-19; Ebr 11:4“Ee nchi, usiifunike damu yangu,

nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.

1916:19 Mwa 31:50; Rum 1:9; 1The 2:5; Ay 22:12; 19:27; Za 113:5; Isa 33:5Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni;

wakili wangu yuko juu.

2016:20 Mao 2:19; Rum 8:34; Yn 15:15; Ay 16:16Mwombezi wangu ni rafiki yangu

macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;

2116:21 1Fal 8:45; Za 140:12kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu

kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.

2216:22 Ay 10:21; Mhu 12:5“Ni miaka michache tu itapita

kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

Japanese Contemporary Bible

ヨブ 記 16:1-22

16

ヨブのことば

1ヨブの返答。

2「そんなことは、さんざん聞かされてきた。

あなたがたは慰め役としては失格だ。

3そんな話をいつまで続けるつもりなのか。

いったい、私が何を言ったというので、

そんなに長々としゃべり続けているのか。

4とはいっても、立場が逆だったら、

私も同じようなお説教をしていたかもしれない。

あきれ果てて、痛烈な批判を浴びせかけていただろう。

5ただ、私はあなたがたとは違う。

私なら、もっと励ましになることを話すはずだ。

あなたたちの悲しみを和らげようと、

一生懸命になるはずだ。

6しかし、私がどれほど自分を弁護したところで、

悲しみは消えるものではない。

だからといって、口をつぐんでいても、

どうにもならない。

7神が私を押しつぶし、家族を取り上げたからだ。

8ああ神よ、あなたは私を骨と皮ばかりになさいました。

彼らは、私が罪を犯した証拠だと責めます。

9神は私を憎み、

怒りにまかせて私の体を引き裂きます。

私に向かって歯ぎしりし、

生きている気配さえ消し去ってしまおうと

身構えておられるのです。

10ここにいる慰めにもならない慰め役たちは、

私を丸のみにしようと口を大きく開けています。

敵はいっせいに攻撃をしかけます。

11神は、私を罪人たちの手に渡し、

悪者の餌食にするのです。

12私は神にずたずたにされるまでは、

平穏無事な生活を送っていた。

ところが神は、私の首をつかまえ、

打ちつけて粉々にし、攻撃の的にした。

13私を取り巻く射手たちが、容赦なく矢を射たので、

傷口から流れ出る血で地は湿った。

14神はたたみかけるように攻撃し、

巨人のように襲いかかる。

15私はこうして荒布をまとって座り込み、

いっさいの望みをちりの中に埋めた。

16目は泣きはらして赤くなり、

まぶたには死の陰がただよっている。

17だが、だれが何と言おうと、

私は潔白で、私の祈りは純粋だ。

18大地よ、私の血を隠さないでくれ。

私の血が私のために大声で抗議できるように。

19今でも天には、私の身の潔白を証明するお方がいる。

私の弁護人は高い所にいる。

20友人たちは私をあざける。

だが私は、神の前で涙を流す。

21人が友のためにとりなすように、

その方に、私と神との間に立っていただきたい。

22私はもうすぐ、帰ることのない旅路につくのだから。