Ayubu 13 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 13:1-28

113:1 Ay 9:24“Macho yangu yameona hili lote,

masikio yangu yamesikia na kulielewa.

213:2 Ay 12:3Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua;

mimi si mtu duni kuliko ninyi.

313:3 Ay 5:8; 23:3-4; 5:17; 40:2Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi

na kuhojiana shauri langu na Mungu.

413:4 Isa 9:15; Yer 23:32; Za 119:69; Yer 8:22; Ay 6:15Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo;

ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!

513:5 Mit 17:28; Amo 5:13; Ay 13:13; Amu 18:19; Mhu 5:3; Yak 1:19Laiti wote mngenyamaza kimya!

Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.

613:6 Ay 33:1; 36:4Sikieni sasa hoja yangu;

sikilizeni kusihi kwangu.

713:7 Ay 16:17; 36:4; 17:5; Rum 3:5-8Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu?

Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?

813:8 Law 19:15; Mit 24:23Mtamwonyesha upendeleo?

Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?

913:9 Ay 12:16; 9:3; Gal 6:7Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi?

Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?

1013:10 Law 19:15; 2Nya 19:7Hakika angewakemea

kama mkiwapendelea watu kwa siri.

1113:11 Ay 31:23; Kut 3:6Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi?

Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?

1213:12 Neh 4:2-3Maneno yenu ni mithali za majivu;

utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.

1313:13 Ay 13:5; 7:11; 9:21“Nyamazeni kimya nipate kusema;

kisha na yanipate yatakayonipata.

1413:14 Amu 9:17; Za 119:109Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari

na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?

1513:15 Za 27:1; Dan 3:28; Ay 5:8; 27:5; Mit 14:32; Rum 8:38-39Ingawa ataniua, bado nitamtumaini;

hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.

1613:16 Hos 14:4; Flp 1:19; Isa 12:1-2Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu,

kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu

atakayethubutu kuja mbele yake!

1713:17 Ay 21:2Sikilizeni maneno yangu kwa makini;

nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.

1813:18 Ay 13:3; 23:4; 37:19; 2:3; 9:21Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu,

ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.

1913:19 Isa 50:8; Rum 8:33; Ay 3:13; 40:4; 9:15Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu?

Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.

20“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili,

nami sitajificha uso wako:

2113:21 Za 39:10; Ebr 10:31; Kut 9:3; Ay 6:4Ondoa mkono wako uwe mbali nami,

nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.

2213:22 Ay 9:35; 14:15Niite kwenye shauri nami nitajibu,

au niache niseme, nawe upate kujibu.

2313:23 1Sam 26:18; Ay 7:21; 9:21; 14:17; 33:9Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda?

Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.

2413:24 Isa 8:17; Za 88:14-15; Yer 30:14Kwa nini kuuficha uso wako

na kunihesabu mimi kuwa adui yako?

2513:25 Law 26:36; Isa 43:17; Hos 13:3Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo?

Je, utayasaka makapi makavu?

2613:26 Ay 21:23; Za 25:7Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu

na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.

2713:27 Mwa 40:15; Mdo 16:24Umeifunga miguu yangu kwenye pingu.

Unazichunga kwa makini njia zangu zote

kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.

2813:28 Hos 5:12; Yak 5:2“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza,

kama vazi lililoliwa na nondo.

New International Version – UK

Job 13:1-28

1‘My eyes have seen all this,

my ears have heard and understood it.

2What you know, I also know;

I am not inferior to you.

3But I desire to speak to the Almighty

and to argue my case with God.

4You, however, smear me with lies;

you are worthless physicians, all of you!

5If only you would be altogether silent!

For you, that would be wisdom.

6Hear now my argument;

listen to the pleas of my lips.

7Will you speak wickedly on God’s behalf?

Will you speak deceitfully for him?

8Will you show him partiality?

Will you argue the case for God?

9Would it turn out well if he examined you?

Could you deceive him as you might deceive a mortal?

10He would surely call you to account

if you secretly showed partiality.

11Would not his splendour terrify you?

Would not the dread of him fall on you?

12Your maxims are proverbs of ashes;

your defences are defences of clay.

13‘Keep silent and let me speak;

then let come to me what may.

14Why do I put myself in jeopardy

and take my life in my hands?

15Though he slay me, yet will I hope in him;

I will surely13:15 Or He will surely slay me; I have no hope – / yet I will defend my ways to his face.

16Indeed, this will turn out for my deliverance,

for no godless person would dare come before him!

17Listen carefully to what I say;

let my words ring in your ears.

18Now that I have prepared my case,

I know I will be vindicated.

19Can anyone bring charges against me?

If so, I will be silent and die.

20‘Only grant me these two things, God,

and then I will not hide from you:

21withdraw your hand far from me,

and stop frightening me with your terrors.

22Then summon me and I will answer,

or let me speak, and you reply to me.

23How many wrongs and sins have I committed?

Show me my offence and my sin.

24Why do you hide your face

and consider me your enemy?

25Will you torment a wind-blown leaf?

Will you chase after dry chaff?

26For you write down bitter things against me

and make me reap the sins of my youth.

27You fasten my feet in shackles;

you keep close watch on all my paths

by putting marks on the soles of my feet.

28‘So man wastes away like something rotten,

like a garment eaten by moths.