Ayubu 11 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 11:1-20

Sofari Anasema: Hatia Ya Ayubu Inastahili Adhabu

111:1 Ay 2:11Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:

211:2 Ay 8:2; 16:3; Mwa 41:6“Je, maneno haya yote yapite bila kujibiwa?

Je, huyu mnenaji athibitishwe kuwa na haki?

311:3 Efe 4:29; 5:4; Ay 12:4; 16:10; 17:2; 21:3Je, maneno yako ya upuzi yawafanye watu wanyamaze kimya?

Je, mtu asikukemee unapofanya dhihaka?

411:4 Ay 6:10; 9:21; 10:7; 1Pet 3:15Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili

nami ni safi mbele zako.’

5Aha! Laiti kwamba Mungu angesema,

kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,

611:6 Ay 9:4; 1Kor 2:10; Mao 3:22; Ezr 9:13naye akufunulie siri za hekima,

kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili.

Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.

711:7 Mhu 3:11; Rum 11:33; Isa 40:28; Ay 5:9; Mt 11:27; Efe 3:8“Je, waweza kujua siri za Mungu?

Je, waweza kuyachunguza mambo yote kumhusu Mwenyezi?

811:8 Za 57:10; Isa 55:9; Efe 3:18; Mwa 15:5; Ay 22:12; 25:2; Za 57:10; 139:8; Isa 55:9; Ay 7:9; 15:13, 25; 33:13; 40:2Ni juu mno kuliko mbingu: waweza kufanya nini?

Kina chake ni kirefu kuliko kuzimu:

wewe waweza kujua nini?

911:9 Efe 3:19-20; Ay 22:12; 35:5; 36:26; 37:5, 23; Isa 40:26Kipimo chake ni kirefu kuliko dunia,

nacho ni kipana kuliko bahari.

1011:10 Ay 9:12; Ufu 3:7“Kama akija na kukufunga gerezani,

na kuitisha mahakama, ni nani awezaye kumpinga?

1111:11 Ay 10:4; 31:37; 34:11, 25; 36:7; Za 10:14Hakika anawatambua watu wadanganyifu;

naye aonapo uovu, je, haangalii?

1211:12 Mwa 12:16; 2Nya 6:36Mpumbavu aweza kuwa mwenye hekima,

endapo mtoto wa punda-mwitu atazaliwa mwanadamu.

1311:13 1Sam 7:3; Za 78:8; 88:9; Kut 9:29; Ay 5:8, 27“Hata sasa ukiutoa moyo wako kwake

na kumwinulia mikono yako,

1411:14 Yos 24:14; Za 101:4; 22:23ukiiondolea mbali ile dhambi iliyo mkononi mwako

wala usiuruhusu uovu ukae hemani mwako,

1511:15 Ay 22:26; 1Yn 3:21; 1Tim 2:8; 1Sam 2:9; Za 20:8; 37:23; 40:2; Efe 6:14; Mwa 4:7ndipo utainua uso wako bila aibu;

utasimama imara bila hofu.

1611:16 Isa 26:16; 37:3; 65:16; Eze 21:7; Yos 7:5; Za 58:7; 112:10; Ay 22:11Hakika utaisahau taabu yako,

utaikumbuka tu kama maji yaliyokwisha kupita.

1711:17 Ay 22:28; Za 37:6; Isa 58:8, 10; 62:1; Ay 17:12; Za 18:28Maisha yako yatangʼaa kuliko adhuhuri,

nalo giza litakuwa kama alfajiri.

1811:18 Mhu 5:12; Isa 11:10; Zek 3:10; Za 127:2Utakuwa salama, kwa kuwa lipo tumaini;

utatazama pande zote na kupumzika kwa salama.

1911:19 Law 26:6; Isa 45:14Utalala, wala hakuna atakayekuogofya,

naam, wengi watajipendekeza kwako.

2011:20 Kum 28:65; Yer 11:11; Amo 2:14; Ay 8:13; 17:5Bali macho ya waovu hayataona,

wokovu utawaepuka;

tarajio lao litakuwa ni hangaiko

la mtu anayekata roho.”

Ketab El Hayat

أيوب 11:1-20

صوفر

1فَأَجَابَ صُوفَرُ النَّعْمَاتِيُّ: 2«هَلْ يُتْرَكُ هَذَا الْكَلامُ الْمُفَرِّطُ مِنْ غَيْرِ جَوَابٍ، أَمْ يَتَبَرَّأُ الرَّجُلُ الْمِهْذَارُ؟ 3أَيُفْحِمُ لَغْوُكَ النَّاسَ، أَمْ تَهَكُّمُكَ يَحُولُ دُونَ تَسْفِيهِكَ؟ 4إِذْ تَدَّعِي قَائِلاً: مَذْهَبِي صَالِحٌ، وَأَنَا بَارٌّ فِي عَيْنَيِ الرَّبِّ. 5وَلَكِنْ لَيْتَ اللهَ يَتَكَلَّمُ وَيَفْتَحُ شَفَتَيْهِ لِيَرُدَّ عَلَيْكَ، 6وَيَكْشِفَ لَكَ أَسْرَارَ حِكْمَتِهِ، فَلِلْحِكْمَةِ الصَّالِحَةِ وَجْهَانِ، فَتُدْرِكَ آنَئِذٍ أَنَّ اللهَ عَاقَبَكَ عَلَى إِثْمِكَ بِأَقَلَّ مِمَّا تَسْتَحِقُّ.

7أَلَعَلَّكَ تُدْرِكُ أَعْمَاقَ اللهِ، أَمْ تَبْلُغُ أَقْصَى قُوَّةِ الْقَدِيرِ؟ 8هُوَ أَسْمَى مِنَ السَّمَاوَاتِ، فَمَاذَا يُمْكِنُكَ أَنْ تَفْعَلَ؟ وَهُوَ أَبْعَدُ غَوْراً مِنَ الْهَاوِيَةِ، فَمَاذَا تَعْلَمُ؟ 9هُوَ أَطْوَلُ مِنَ الأَرْضِ وَأَعْرَضُ مِنَ الْبَحْرِ. 10فَإِنِ اجْتَازَ وَاعْتَقَلَكَ وَحَاكَمَكَ فَمَنْ يَرُدُّهُ؟ 11لأَنَّهُ عَالِمٌ بِالْمُنَافِقِينَ. إِنْ رَأَى الإِثْمَ، أَفَلا يَنْظُرُ فِي أَمْرِهِ؟ 12يُصْبِحُ الأَحْمَقُ حَكِيماً عِنْدَمَا يَلِدُ حِمَارُ الْوَحْشِ إِنْسَاناً.

13إِنْ هَيَّأْتَ قَلْبَكَ وَبَسَطْتَ إِلَيْهِ يَدَيْكَ، 14وَإِنْ نَبَذْتَ الإِثْمَ الَّذِي تَلَطَّخَتْ بِهِ كَفَّاكَ، فَلَمْ يَعُدِ الْجَوْرُ يُقِيمُ فِي خَيْمَتِكَ. 15حِينَئِذٍ تَرْفَعُ وَجْهَكَ بِكَرَامَةٍ، وَتَكُونُ رَاسِخاً مِنْ غَيْرِ خَوْفٍ، 16فَتَنْسَى مَا قَاسَيْتَ مِنْ مَشَقَّةٍ، وَلا تَذْكُرُهَا إِلّا كَمِيَاهٍ عَبَرَتْ. 17وَتُصْبِحُ حَيَاتُكَ أَكْثَرَ إِشْرَاقاً مِنْ نُورِ الظَّهِيرَةِ، وَيَتَحَوَّلُ ظَلامُهَا إِلَى صَبَاحٍ، 18وَتَطْمَئِنُّ لأَنَّ هُنَاكَ رَجَاءً، وَتَتَلَفَّتُ حَوْلَكَ وَتَرْقُدُ آمِناً. 19تَسْتَكِينُ إِذْ لَيْسَ مِنْ مُرَوِّعٍ، وَكَثِيرُونَ يَتَرَجَّوْنَ رِضَاكَ 20أَمَّا عُيُونُ الأَشْرَارِ فَيُصِيبُهَا التَّلَفُ، وَمَنَافِذُ الْهَرَبِ تَخْتَفِي مِنْ أَمَامِهِمْ، وَلا أَمَلَ لَهُمْ إِلّا فِي الْمَوْتِ».