Ayubu 10 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 10:1-22

Ayubu: Nayachukia Maisha Yangu

110:1 Hes 11:15; 1Sam 1:10; Ay 7:11; 9:18, 21; 1Fal 19:4“Nayachukia sana haya maisha yangu;

kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia,

nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.

210:2 Ay 13:3; 40:1; Isa 3:13; Hos 4:1; 5:1; Mik 6:2; Rum 8:33Nitamwambia Mungu: Usinihukumu,

bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.

310:3 Ay 9:24; 22:18; 31:23; Mwa 1:26; Za 138:8; Isa 60:21; 64:8; Za 8:6; 95:6; 100:3Je, inakupendeza wewe kunionea,

kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako,

huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?

410:4 Mit 5:21; Yer 16:17; 1Sam 16:7; Ay 11:11; 14:16; Za 11:4; 33:15; Mit 15:3; Yer 11:20-23Je, wewe una macho ya kimwili?

Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?

510:5 Za 102:24; 2Pet 3:8; Ay 36:26; Za 39:5; 90:2, 4Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu,

au miaka yako ni kama ile ya mtu,

610:6 Ay 14:16ili kwamba utafute makosa yangu

na kuichunguza dhambi yangu;

710:7 Ay 10:15; 6:29; 11:4; 16:17; Kum 32:39ingawa wajua kuwa mimi sina hatia,

na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?

810:8 Za 119:73; Isa 43:7; Mwa 2:7; 2Sam 14:14; Ay 30:15“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya.

Je, sasa utageuka na kuniangamiza?

910:9 Isa 29:16; 64:8; Mwa 2:7; Ay 7:21; 4:19Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi.

Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?

10Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa,

na kunigandisha kama jibini,

1110:11 Za 139:13, 15ukanivika ngozi na nyama,

na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?

1210:12 Mwa 2:7; 24:12; 45:5; 1Pet 2:25Umenipa uhai na kunitendea wema,

katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.

1310:13 Ay 23:13; Za 115:3“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako,

nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:

1410:14 Kut 34:7; Ay 7:21; 13:27Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona,

wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.

1510:15 Ay 9:13; 10:7; Isa 3:11; Za 25:18; 25:16Kama nina hatia, ole wangu!

Hata kama ningekuwa sina hatia,

siwezi kukiinua kichwa changu,

kwa kuwa nimejawa na aibu,

na kuzama katika mateso yangu.

1610:16 Yer 5:6; Hos 5:14; 1Sam 28:21; Isa 38:16; Za 7:2; 1Sam 17:38; Mao 3:10Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba,

na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.

1710:17 1Fal 21:10; Ay 16:8; Rut 1:21Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu

na kuzidisha hasira yako juu yangu;

nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.

1810:18 Ay 3:8; 3:26; Za 22:9; Mhu 4:2; 7:1“Kwa nini basi ulinitoa tumboni?

Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.

1910:19 Ay 3:3; Yer 15:10Laiti nisingekuwako kamwe,

au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja

kutoka tumboni kwenda kaburini!

2010:20 Mhu 6:12; Ay 7:16-19; 5:7; Za 39:13; Ay 9:25Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha?

Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi

2110:21 2Sam 12:23; Za 88:12; 23:4; Ay 3:13; Mhu 2:9kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena,

katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,

2210:22 Ay 3:5; 1Sam 2:9nchi ya giza kuu sana,

yenye uvuli wa giza na machafuko,

mahali ambapo hata nuru ni giza.”

Ketab El Hayat

أيوب 10:1-22

1قَدْ كَرِهْتُ حَيَاتِي، لِهَذَا أُطْلِقُ الْعَنَانَ لِشَكْوَايَ، وَأَتَحَدَّثُ عَنْ أَشْجَانِي فِي مَرَارَةِ نَفْسِي، 2قَائِلاً لِلهِ: لَا تَسْتَذْنِبْنِي. فَهِّمْنِي لِمَاذَا تُخَاصِمُنِي؟ 3أَيَحْلُو لَكَ أَنْ تَظْلِمَ وَتَنْبِذَ عَمَلَ يَدِكَ، وَتُحَبِّذَ مَشُورَةَ الأَشْرَارِ؟ 4أَلَكَ عَيْنَا بَشَرٍ، أَمْ كَنَظَرِ الإِنْسَانِ تَنْظُرُ؟ 5هَلْ أَيَّامُكَ مِثْلُ أَيَّامِ الإِنْسَانِ، أَمْ سِنُوكَ فِي قِصَرِ سِنِيِ الْبَشَرِ، 6حَتَّى تَبْحَثَ عَنْ إِثْمِي وَتُنَقِّبَ عَنْ خَطَايَايَ؟ 7فَأَنْتَ عَالِمٌ أَنِّي لَسْتُ مُذْنِباً، وَأَنَّهُ لَا مُنْقِذَ مِنْ يَدِكَ.

8قَدْ كَوَّنَتْنِي يَدَاكَ وَصَنَعَتَانِي بِجُمْلَتِي، وَالآنَ الْتَفَتَّ إِلَيَّ لِتَسْحَقَنِي! 9اذْكُرْ أَنَّكَ جَبَلْتَنِي مِنْ طِينٍ، أَتُرْجِعُنِي بَعْدُ إِلَى التُّرَابِ؟ 10أَلَمْ تَصُبَّنِي كَاللَّبَنِ وَتُخَثِّرْنِي كَالْجُبْنِ؟ 11كَسَوْتَنِي جِلْداً وَلَحْماً، فَنَسَجْتَنِي بِعِظَامٍ وَعَصَبٍ. 12مَنَحْتَنِي حَيَاةً وَرَحْمَةً، وَحَفِظَتْ عِنَايَتُكَ رُوحِي. 13كَتَمْتَ هَذِهِ الأُمُورَ فِي قَلْبِكَ، إِلّا أَنِّي عَلِمْتُ أَنَّ هَذَا قَصْدُكَ.

14إِنْ أَخْطَأْتُ فَأَنْتَ تُرَاقِبُنِي، وَلا تُبْرِئُنِي مِنْ إِثْمِي. 15إِنْ أَذْنَبْتُ فَوَيْلٌ لِي. وَإِنْ كُنْتُ بَارّاً لَا أَرْفَعُ رَأْسِي، لأَنِّي مُمْتَلِئٌ هَوَاناً وَنَاظِرٌ مَذَلَّتِي، 16وَإِنْ شَمَخْتُ بِرَأْسِي تَقْتَنِصُنِي كَالأَسَدِ، ثُمَّ تَعُودُ فَتَصُولُ عَلَيَّ. 17تُجَدِّدُ شُهُودَكَ ضِدِّي، وَتُضْرِمُ غَضَبَكَ عَلَيَّ، وَتُؤَلِّبُ جُيُوشاً تَتَنَاوَبُ ضِدِّي.

18لِمَاذَا أَخْرَجْتَنِي مِنَ الرَّحِمِ؟ أَلَمْ يَكُنْ خَيْراً لَوْ أَسْلَمْتُ الرُّوحَ وَلَمْ تَرَنِي عَيْنٌ؟ 19فَأَكُونُ كَأَنِّي لَمْ أَكُنْ فَأُنْقَلُ مِنَ الرَّحِمِ إِلَى الْقَبْرِ. 20أَلَيْسَتْ أَيَّامِي قَلِيلَةً؟ كُفَّ عَنِّي لَعَلِّي أَتَمَتَّعُ بِبَعْضِ الْبَهْجَةِ، 21قَبْلَ أَنْ أَمْضِيَ إِلَى حَيْثُ لَا أَعُودُ، إِلَى أَرْضِ الظُّلْمَةِ وَظِلِّ الْمَوْتِ، 22إِلَى أَرْضِ الظُّلْمَةِ الْمُتَكَاثِفَةِ وَالْفَوْضَى، حَيْثُ الإِشْرَاقُ فِيهَا كَاللَّيْلِ الْبَهِيمِ».