Amosi 9 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 9:1-15

Israeli Kuangamizwa

19:1 Za 68:21; Yer 11:11Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema:

“Piga vichwa vya nguzo

ili vizingiti vitikisike.

Viangushe juu ya vichwa vya watu wote;

na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga.

Hakuna awaye yote atakayekimbia,

hakuna atakayetoroka.

29:2 Za 139:8-10; Ay 20:6; 7:9; Yer 51:33; Oba 1:4; Eze 26:20Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu,

kutoka huko mkono wangu utawatoa.

Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu,

kutoka huko nitawashusha.

39:3 Yer 23:24; 6:16-17; Za 139:8-10; 68:22; Mwa 49:17; Ay 11:20Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli,

huko nitawawinda na kuwakamata.

Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu

katika vilindi vya bahari,

huko nako nitaamuru joka kuwauma.

49:4 Law 26:33; 17:10; Eze 5:12; 15:7; Kum 28:65; Yer 39:16; 21:10; 44:11Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao,

huko nako nitaamuru upanga uwaue.

Nitawakazia macho yangu kwa mabaya

wala si kwa mazuri.”

59:5 Za 46:2; Amo 8:8; Mik 1:4Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka,

na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza:

nayo nchi yote huinuka kama Naili,

kisha hushuka kama mto wa Misri;

69:6 Za 104:1-3, 5-13; Amo 5:8; Yer 43:9yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu

na kuisimika misingi yake juu ya dunia,

yeye aitaye maji ya bahari

na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:

Bwana ndilo jina lake.

79:7 2Nya 12:3; Kum 2:23; Isa 43:3; 22:6; 2Fal 16:9; Yer 47:4; Amo 1:5; Mwa 10:14“Je, Waisraeli,

ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?”

asema Bwana.

“Je, sikuleta Israeli kutoka Misri,

Wafilisti kutoka Kaftori,9:7 Yaani Krete.

na Washamu kutoka Kiri?

89:8 Yer 30:11; 44:27; Za 11:4“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi

yako juu ya ufalme wenye dhambi.

Nami nitauangamiza

kutoka kwenye uso wa dunia:

hata hivyo sitaiangamiza kabisa

nyumba ya Yakobo,”

asema Bwana.

99:9 Lk 22:31; Isa 30:28; Yer 31:36; Dan 9:7“Kwa kuwa nitatoa amri,

na nitaipepeta nyumba ya Israeli

miongoni mwa mataifa yote,

kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo,

na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.

109:10 Yer 5:12; 23:17; 49:37; Eze 20:38; Amo 6:3Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu

watauawa kwa upanga,

wale wote wasemao,

‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’

Kurejezwa Kwa Israeli

119:11 Mdo 15:16; Mik 7:8-11; Zek 12:7; Isa 7:2; 49:8; Mwa 26:22; Eze 17:24“Katika siku ile nitaisimamisha

hema ya Daudi iliyoanguka.

Nitakarabati mahali palipobomoka

na kujenga upya magofu yake,

na kuijenga kama ilivyokuwa awali,

129:12 Hes 24:18; Isa 43:7; Oba 1:19; Yer 25:29; Mdo 15:16-17ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu,

na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,”

asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.

139:13 Law 26:5; Amu 9:27; Yoe 3:18; 2:24; Yer 31:38; 33:14; Rut 2:3“Siku zinakuja,” asema Bwana,

“wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima,

naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu.

Divai mpya itadondoka kutoka milimani,

na kutiririka kutoka vilima vyote.

149:14 Isa 32:18; 49:8; 62:9; 61:4; Eze 34:13-14; Yer 29:14; 33:7; 30:18Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa;

wataijenga tena miji iliyoachwa magofu,

nao wataishi ndani mwake.

Watapanda mizabibu na kunywa divai yake;

watalima bustani na kula matunda yake.

159:15 Kut 15:17; Isa 60:21; 65:9; Yer 18:9; 23:8; 3:18; 24:6; 32:15; Eze 28:26; 34:28; Yoe 3:20Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe,

hawatangʼolewa tena

kutoka nchi ambayo nimewapa,”

asema Bwana Mungu wenu.

Ketab El Hayat

عاموس 9:1-15

دمار إسرائيل

1وَرَأَيْتُ السَّيِّدَ وَاقِفاً إِلَى جُوَارِ الْمَذْبَحِ قَائِلاً: «اضْرِبْ تِيجَانَ الأَعْمِدَةِ حَتَّى تَهْتَزَّ الْعَتَبَاتُ، وَحَطِّمْهَا عَلَى رُؤُوسِ جَمِيعِ الشَّعْبِ. وَمَنْ يَنْجُو مِنْهُمْ أُهْلِكُهُ بِالسَّيْفِ، فَلا يَهْرُبُ مِنْهُمْ أَحَدٌ وَلا يُفْلِتُ مِنْهُمْ نَاجٍ. 2وَإِنْ نَقَبُوا لأَنْفُسِهِمْ مَلْجَأً فِي أَعْمَاقِ الْهَاوِيَةِ، فَإِنَّ يَدِي تَطُولُهُمْ هُنَاكَ، وَإِنِ ارْتَقَوْا إِلَى السَّمَاوَاتِ فَمِنْ هُنَاكَ أُنْزِلُهُمْ. 3وَإِنِ اخْتَبَأُوا فِي أَعَالِي الْكَرْمَلِ فَهُنَاكَ أَبْحَثُ عَنْهُمْ وَأَعْتَقِلُهُمْ. وَإِنْ تَوَارَوْا عَنِّي فِي أَعْمَاقِ الْبَحْرِ فَإِنِّي آمُرُ هُنَاكَ الْحَيَّةَ فَتَلْدَغُهُمْ. 4وَإِنْ سِيقُوا إِلَى السَّبْيِ أَمَامَ أَعْدَائِهِمْ أُلاحِقُهُمْ بِالسَّيْفِ لأَفْنِيَهُمْ، وَأَتَعَقَّبُهُمْ لأَبْتَلِيَهُمْ بِالشَّرِّ لَا بِالْخَيْرِ».

5إِنَّ الرَّبَّ الإِلَهَ الْقَدِيرَ هُوَ الَّذِي يَلْمَسُ الأَرْضَ فَتَذُوبُ، وَيَنُوحُ كُلُّ الْمُقِيمِينَ فِيهَا، وَيَرْتَفِعُ كُلُّ مَا فِيهَا وَيَنْخَفِضُ كَنَهْرِ نِيلِ مِصْرَ. 6هُوَ الَّذِي يَبْنِي مَخَادِعَهُ الْعُلْيَا فِي السَّمَاوَاتِ وَيُؤَسِّسُ قُبَّتَهُ عَلَى الأَرْضِ، الَّذِي يَدْعُو مِيَاهَ الْبَحْرِ وَيَسْكُبُهَا عَلَى وَجْهِ الثَّرَى، الرَّبُّ اسْمُهُ.

7أَلَسْتُمْ لِي يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِثْلَ الْكُوشِيِّينَ يَقُولُ الرَّبُّ؟ أَلَمْ أُخْرِجْ إِسْرَائِيلَ مِنْ دِيَارِ مِصْرَ وَالْفِلِسْطِينِيِّينَ مِنْ كَفْتُورَ وَالأَرَامِيِّينَ مِنْ قِيرٍ. 8هَا إِنَّ عَيْنَيِ الرَّبِّ مُسَلَّطَتَانِ عَلَى الْمَمْلَكَةِ الْخَاطِئَةِ لأَمْحُوَهَا عَنْ وَجْهِ الأَرْضِ، إِلّا أَنِّي لَنْ أَسْتَأْصِلَ بَيْتَ يَعْقُوبَ قَاطِبَةً يَقُولُ الرَّبُّ. 9أُغَرْبِلُ بَيْتَ إِسْرَائِيلَ بَيْنَ جَمِيعِ الأُمَمِ كَمَا تُغَرْبَلُ الْحِنْطَةُ فِي غُرْبَالٍ، فَلا تَسْقُطُ حَبَّةٌ عَلَى الأَرْضِ. 10وَيَمُوتُ جَمِيعُ خُطَاةِ شَعْبِي بِالسَّيْفِ مِمَّنْ يَقُولُونَ: لَنْ يُدْرِكَنَا الشَّرُّ أَوْ يَلْقَانَا.

رد السبي

11فِي ذَلِكَ الْيَوْمِ أُقِيمُ مَسْكَنَ دَاوُدَ الَّذِي تَهَاوَى، وَأَسُدُّ ثُغْرَاتِهِ وَأُعَمِّرُ خَرَائِبَهُ وَأُعِيدُ بِنَاءَهُ كَالْعَهْدِ بِهِ فِي الأَيَّامِ الْغَابِرَةِ. 12لِكَيْ يَرِثَ إِسْرَائِيلُ مَا تَبَقَّى مِنْ أَدُومَ وَجَمِيعَ الأُمَمِ الَّتِي دُعِيَ اسْمِي عَلَيْهَا، يَقُولُ الرَّبُّ صَانِعُ هَذِهِ الأُمُورِ. 13هَا أَيَّامٌ تَأْتِي يَقُولُ الرَّبُّ، يُدْرِكُ فِيهَا الْحَارِثُ الْحَاصِدَ، وَدَائِسُ الْعِنَبِ بَاذِرَ الْحَبِّ، وَتَسِيلُ الْخُمورُ الطَّيِّبَةُ مِنْ كُرُومِ الْجِبَالِ وَتَفِيضُ بِها التِّلالُ كُلُّهَا. 14وَأَرُدُّ سَبْيَ شَعْبِي إِسْرَائِيلَ فَيُعِيدُونَ بِنَاءَ الْمُدُنِ الْخَرِبَةِ وَيَسْكُنُونَهَا، وَيَزْرَعُونَ كُرُوماً وَيَشْرَبُونَ مِنْ خَمْرِهَا، وَيَغْرِسُونَ جَنَّاتٍ وَيَأْكُلُونَ مِنْ ثِمَارِهَا. 15وَأَغْرِسُ شَعْبِي فِي أَرْضِهِمْ فَلا يُسْتَأْصَلُونَ ثَانِيَةً أَبَداً مِنَ الأَرْضِ الَّتِي وَهَبْتُهَا لَهُمْ، يَقُولُ الرَّبُّ إِلَهُكُمْ.