Amosi 5 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 5:1-27

Maombolezo Na Wito Wa Toba

15:1 Yer 4:8; 7:29; Eze 9:1Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:

25:2 2Fal 19:21; Yer 14:17; 50:32; Amo 8:14“Bikira Israeli ameanguka,

kamwe hatainuka tena,

ameachwa pweke katika nchi yake,

hakuna yeyote wa kumwinua.”

35:3 Amo 6:9; Isa 6:13Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli,

mia moja tu watarudi;

wakati mji utakapopeleka mia moja,

kumi tu ndio watarudi hai.”

45:4 Kum 32:46-47; 4:29; Isa 55:3; 2Nya 15:2; Yer 29:13; Eze 18:9Hili ndilo Bwana asemalo kwa nyumba ya Israeli:

“Nitafuteni mpate kuishi;

55:5 1Sam 11:14; 7:16; 8:6; Mwa 21:31; Hos 4:15; Amu 8:14msitafute Betheli,

msiende Gilgali,

msisafiri kwenda Beer-Sheba.

Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni,

na Betheli itafanywa kuwa si kitu.”5:5 Yaani Aveni kwa Kiebrania, kumaanisha Beth-Aveni, jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

65:6 Sef 2:3; Amo 3:14; Law 18:5; Za 22:26; 105:4; Kum 4:24Mtafuteni Bwana mpate kuishi,

au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto;

utawateketeza, nayo Betheli

haitakuwa na yeyote wa kuuzima.

75:7 Isa 5:20; Amo 6:12; 3:10; Hos 10:4Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu

na kuiangusha haki chini

85:8 Ay 38:31-34; Mwa 1:16; Isa 42:16; Za 104:6-9, 20; Yer 16:21; Amo 4:13(yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni,

ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko

na mchana kuwa usiku,

ambaye huyaita maji ya bahari

na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:

Bwana ndilo jina lake;

9yeye hufanya maangamizo kwenye ngome

na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),

105:10 Isa 29:21; Mwa 4:16; 1Fal 22:8; Gal 4:16mnamchukia yule akemeaye mahakamani,

na kumdharau yule ambaye husema kweli.

115:11 Mik 6:15; Amo 8:6; 3:15; 9:14; Amu 9:27; Sef 1:13Mnamgandamiza maskini

na kumlazimisha awape nafaka.

Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari,

hamtaishi ndani yake;

ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu,

hamtakunywa divai yake.

125:12 Ay 5:4; 36:18; Isa 29:21; 5:23; 1:23; Hos 5:3; Eze 22:12; Yer 5:28; Amo 2:6-7Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu

na ukubwa wa dhambi zenu.

Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa

na kuzuia haki ya maskini mahakamani.

13Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo,

kwa kuwa nyakati ni mbaya.

145:14 Za 34:12-16; Mit 7:7; 11:27; Isa 1:16, 17; Mik 3:11; 6:8; Rum 2:7-9Tafuteni mema, wala si mabaya,

ili mpate kuishi.

Ndipo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atakuwa pamoja nanyi,

kama msemavyo yupo nanyi.

155:15 Rum 12:9; Yoe 2:14; Kut 32:30; Za 52:3; 97:10; Mik 5:7-8; 7:18; Mwa 18:25Yachukieni maovu, yapendeni mema;

dumisheni haki mahakamani.

Yamkini Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote

atawahurumia mabaki ya Yosefu.

165:16 Yer 9:17; 7:34; Sef 1:10; Yoe 1:11Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo:

“Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote

na vilio vya uchungu katika njia kuu zote.

Wakulima wataitwa kuja kulia,

na waombolezaji waje kuomboleza.

175:17 Kut 12:12; Isa 16:10; Yer 48:33Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu,

kwa kuwa nitapita katikati yenu,”

asema Bwana.

Siku Ya Bwana

185:18 Isa 2:12; 5:19, 30; Yoe 1:15; Ay 20:28; Yer 30:7; 1Sam 2:9Ole wenu ninyi mnaoitamani

siku ya Bwana!

Kwa nini mnaitamani siku ya Bwana?

Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.

195:19 Mhu 10:8; Kum 32:34; Ay 20:24; Mao 3:10; Eze 12:22; Mal 3:1; 2Pet 3:4; Isa 24:17-18; Yer 15:2-3Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba

kumbe akakutana na dubu,

kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake

na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta,

kumbe akaumwa na nyoka.

205:20 Oba 1:15; Eze 7:7; 1Sam 2:9; Isa 13:10; Sef 1:15Je, siku ya Bwana haitakuwa giza, na si nuru:

giza nene, bila mwonzi wa mwanga?

215:21 Law 26:31; Hos 2:11; Yer 44:4; Isa 1:11-16; Eze 23:18“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini;

siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.

225:22 Yer 14:12; 7:21; Mik 6:6-7; Isa 1:11-16; 66:3; Za 40:6; Amo 4:4Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka,

sitazikubali.

Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani,

sitazitambua.

23Niondoleeni kelele za nyimbo zenu!

Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.

245:24 Yer 22:3; Mik 6:8; Isa 45:8Lakini acheni haki itiririke kama mto,

na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!

255:25 Isa 43:23; Mdo 7:42; Kum 32:17; Kut 16:35“Je, mliniletea dhabihu na sadaka

kwa miaka arobaini kule jangwani,

ee nyumba ya Israeli?

265:26 Eze 18:6; 20:16Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu,

Sikuthi mungu wenu mtawala,

na Kiuni mungu wenu wa nyota,

ambao mliwatengeneza wenyewe.

275:27 Yer 38:17; Amo 6:7; Mdo 7:42-43; Mik 1:16; Kum 32:17-19Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,”

asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.

Nueva Versión Internacional

Amós 5:1-27

Advertencias y lamentos

1Escuchen, israelitas, esta palabra, este canto fúnebre que por ustedes entono:

2«Ha caído la virginal Israel

y no volverá a levantarse;

abandonada en su propia tierra,

no hay quien la levante».

3Así dice el Señor y Dios al reino de Israel:

«La ciudad que salía a la guerra con mil hombres

se quedará solo con cien

y la que salía con cien

se quedará solo con diez».

4Así dice el Señor a Israel:

«¡Búsquenme y vivirán!

5Pero no busquen a Betel,

ni vayan a Guilgal,

ni pasen a Berseba;

porque Guilgal será llevada cautiva

y Betel, reducida a la nada».5:5 nada. Lit. aven, que es una posible referencia a Betel Avén, que significa casa de maldad, un nombre despectivo dado a Betel, que significa casa de Dios; véase Os 4:15.

6¡Busquen al Señor y vivirán!,

no sea que él caiga como fuego

sobre los descendientes de José,

fuego que devore a Betel

sin que haya quien lo apague.

7Ustedes convierten el derecho en amargura

y echan por tierra la justicia.

8El que hizo las Pléyades y el Orión,

convierte en aurora las densas tinieblas

y oscurece el día hasta convertirlo en noche.

Él convoca las aguas del mar

y las derrama sobre la tierra.

¡Su nombre es el Señor!

9Él trae una destrucción repentina sobre la fortaleza

y sobre la plaza fuerte, destrucción.

10Ustedes odian al que defiende la justicia en el tribunal

y detestan al que dice la verdad.

11Por eso, como oprimen a los pobres

y les exigen un impuesto sobre el grano,

no vivirán en las casas de piedra labrada que han construido

ni beberán del vino de los selectos viñedos que han plantado.

12¡Yo sé cuán numerosos son sus delitos,

cuán grandes sus pecados!

Ustedes oprimen al justo, exigen soborno

y en los tribunales atropellan al necesitado.

13Por eso en circunstancias como estas guarda silencio el prudente,

porque estos tiempos son malos.

14Busquen el bien y no el mal, y vivirán;

y así estará con ustedes el Señor Dios de los Ejércitos,

tal como ustedes lo afirman.

15¡Odien el mal y amen el bien!

Establezcan la justicia en los tribunales;

tal vez así el Señor, el Dios de los Ejércitos,

tenga compasión del remanente de José.

16Por eso, así dice el Señor y Dios, el Dios de los Ejércitos:

«En todas las plazas se escucharán lamentos

y gritos de angustia en todas las calles.

Llamarán a duelo a los agricultores

y a los llorones profesionales para hacer lamentación.

17Se escucharán lamentos en todos los viñedos

cuando yo pase en medio de ti»,

dice el Señor.

El día del Señor

18¡Ay de los que suspiran

por el día del Señor!

¿De qué les servirá ese día

si va a ser de oscuridad y no de luz?

19Será como cuando alguien huye de un león

y se le viene encima un oso,

o como cuando al llegar a su casa,

apoya la mano en la pared

y lo muerde una serpiente.

20¿No será el día del Señor de oscuridad y no de luz?

¡Será por cierto sombrío y sin resplandor!

21«Detesto y aborrezco sus fiestas religiosas;

no me agradan sus cultos solemnes.

22Aunque me traigan holocaustos y ofrendas de cereal,

no los aceptaré;

no prestaré atención

a los sacrificios de comunión de novillos cebados.

23Aleja de mí el bullicio de tus canciones;

no quiero oír la música de tus liras.

24Pero ¡que fluya el derecho como las aguas

y la justicia como arroyo inagotable!

25»Casa de Israel, ¿acaso me ofrecieron ustedes sacrificios y ofrendas

durante los cuarenta años en el desierto?

26Ustedes cargaban la imagen de Sicut, su rey,

y también la de Quiyún,

imágenes de esos dioses astrales

que ustedes mismos se han fabricado.

27Por lo tanto, los mandaré al exilio más allá de Damasco»,

dice el Señor, cuyo nombre es Dios de los Ejércitos.