Amosi 3 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 3:1-15

Mashahidi Waitwa Dhidi Ya Israeli

13:1 Amo 2:10; Sef 2:5Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:

23:2 Kut 19:6; 1Pet 4:17; Lk 12:47; Mik 2:3; Eze 9:6; Dan 9:12; Mt 11:22; Rum 2:9; Kum 7:6; Yer 14:10“Ni ninyi tu niliowachagua

kati ya jamaa zote za dunia;

kwa hiyo nitawaadhibu

kwa ajili ya dhambi zenu zote.”

3Je, watu wawili hutembea pamoja

wasipokubaliana kufanya hivyo?

43:4 Za 104:21; Hos 5:14; Isa 42:13Je, simba hunguruma katika kichaka

wakati hana mawindo?

Aweza kuvuma katika pango

wakati ambao hajakamata chochote?

5Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini

ambapo hajategewa chambo?

Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini

wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?

63:6 Isa 14:24-27; 31:2; 45:7; Hes 10:2; Eze 33:3; Ay 39:24; Yer 4:21Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari,

watu hawatetemeki?

Mji upatwapo na maafa,

je, si Bwana amesababisha?

73:7 1Sam 3:7; Mwa 6:13; 18:17; Mit 3:32; Yn 15:15; Yer 23:22; Mit 3:32; Dan 9:22-27; Ufu 1:1, 19Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote

bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.

83:8 1Kor 9:16; Yn 3:1-3; Mdo 4:20; Isa 31:4; 42:13; Yer 20:9Simba amenguruma:

je, ni nani ambaye hataogopa?

Bwana Mwenyezi ametamka:

je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?

93:9 Yos 13:3; 2Nya 26:6Tangazeni katika ngome za Ashdodi

na katika ngome za Misri:

“Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria;

angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake,

na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”

103:10 Yer 4:22; Amo 6:12; 5:7; Mik 6:10; Hab 2:8Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema,

wale ambao hujilundikia nyara

na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”

113:11 Amo 2:5; 6:14; 2Fal 17:6Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Adui ataizingira nchi;

ataangusha chini ngome zenu

na kuteka nyara maboma yenu.”

123:12 1Sam 17:34; Es 1:6; Amo 6:4Hili ndilo asemalo Bwana:

“Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba

vipande viwili tu vya mfupa wa mguu

au kipande cha sikio,

hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa,

wale wakaao Samaria

kwenye kingo za vitanda vyao,

na katika Dameski

kwenye viti vyao vya fahari.”

13“Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

143:14 Mwa 12:8; Amo 5:5-6; Kut 27:2; Law 26:18“Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake,

nitaharibu madhabahu za Betheli;

pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali

na kuanguka chini.

153:15 Yer 36:22; Amu 3:20; 1Fal 22:39; Hos 10:5-8; Isa 34:5; Amo 5:11; 6:11Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika,

pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi;

nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu

na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,”

asema Bwana.

New International Version

Amos 3:1-15

Witnesses Summoned Against Israel

1Hear this word, people of Israel, the word the Lord has spoken against you—against the whole family I brought up out of Egypt:

2“You only have I chosen

of all the families of the earth;

therefore I will punish you

for all your sins.”

3Do two walk together

unless they have agreed to do so?

4Does a lion roar in the thicket

when it has no prey?

Does it growl in its den

when it has caught nothing?

5Does a bird swoop down to a trap on the ground

when no bait is there?

Does a trap spring up from the ground

if it has not caught anything?

6When a trumpet sounds in a city,

do not the people tremble?

When disaster comes to a city,

has not the Lord caused it?

7Surely the Sovereign Lord does nothing

without revealing his plan

to his servants the prophets.

8The lion has roared—

who will not fear?

The Sovereign Lord has spoken—

who can but prophesy?

9Proclaim to the fortresses of Ashdod

and to the fortresses of Egypt:

“Assemble yourselves on the mountains of Samaria;

see the great unrest within her

and the oppression among her people.”

10“They do not know how to do right,” declares the Lord,

“who store up in their fortresses

what they have plundered and looted.”

11Therefore this is what the Sovereign Lord says:

“An enemy will overrun your land,

pull down your strongholds

and plunder your fortresses.”

12This is what the Lord says:

“As a shepherd rescues from the lion’s mouth

only two leg bones or a piece of an ear,

so will the Israelites living in Samaria be rescued,

with only the head of a bed

and a piece of fabric3:12 The meaning of the Hebrew for this phrase is uncertain. from a couch.3:12 Or Israelites be rescued, / those who sit in Samaria / on the edge of their beds / and in Damascus on their couches.

13“Hear this and testify against the descendants of Jacob,” declares the Lord, the Lord God Almighty.

14“On the day I punish Israel for her sins,

I will destroy the altars of Bethel;

the horns of the altar will be cut off

and fall to the ground.

15I will tear down the winter house

along with the summer house;

the houses adorned with ivory will be destroyed

and the mansions will be demolished,”

declares the Lord.