Amosi 3 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 3:1-15

Mashahidi Waitwa Dhidi Ya Israeli

13:1 Amo 2:10; Sef 2:5Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:

23:2 Kut 19:6; 1Pet 4:17; Lk 12:47; Mik 2:3; Eze 9:6; Dan 9:12; Mt 11:22; Rum 2:9; Kum 7:6; Yer 14:10“Ni ninyi tu niliowachagua

kati ya jamaa zote za dunia;

kwa hiyo nitawaadhibu

kwa ajili ya dhambi zenu zote.”

3Je, watu wawili hutembea pamoja

wasipokubaliana kufanya hivyo?

43:4 Za 104:21; Hos 5:14; Isa 42:13Je, simba hunguruma katika kichaka

wakati hana mawindo?

Aweza kuvuma katika pango

wakati ambao hajakamata chochote?

5Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini

ambapo hajategewa chambo?

Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini

wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?

63:6 Isa 14:24-27; 31:2; 45:7; Hes 10:2; Eze 33:3; Ay 39:24; Yer 4:21Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari,

watu hawatetemeki?

Mji upatwapo na maafa,

je, si Bwana amesababisha?

73:7 1Sam 3:7; Mwa 6:13; 18:17; Mit 3:32; Yn 15:15; Yer 23:22; Mit 3:32; Dan 9:22-27; Ufu 1:1, 19Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote

bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.

83:8 1Kor 9:16; Yn 3:1-3; Mdo 4:20; Isa 31:4; 42:13; Yer 20:9Simba amenguruma:

je, ni nani ambaye hataogopa?

Bwana Mwenyezi ametamka:

je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?

93:9 Yos 13:3; 2Nya 26:6Tangazeni katika ngome za Ashdodi

na katika ngome za Misri:

“Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria;

angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake,

na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”

103:10 Yer 4:22; Amo 6:12; 5:7; Mik 6:10; Hab 2:8Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema,

wale ambao hujilundikia nyara

na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”

113:11 Amo 2:5; 6:14; 2Fal 17:6Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Adui ataizingira nchi;

ataangusha chini ngome zenu

na kuteka nyara maboma yenu.”

123:12 1Sam 17:34; Es 1:6; Amo 6:4Hili ndilo asemalo Bwana:

“Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba

vipande viwili tu vya mfupa wa mguu

au kipande cha sikio,

hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa,

wale wakaao Samaria

kwenye kingo za vitanda vyao,

na katika Dameski

kwenye viti vyao vya fahari.”

13“Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

143:14 Mwa 12:8; Amo 5:5-6; Kut 27:2; Law 26:18“Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake,

nitaharibu madhabahu za Betheli;

pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali

na kuanguka chini.

153:15 Yer 36:22; Amu 3:20; 1Fal 22:39; Hos 10:5-8; Isa 34:5; Amo 5:11; 6:11Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika,

pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi;

nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu

na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,”

asema Bwana.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

阿摩司書 3:1-15

責備以色列人

1以色列人啊,

要聽耶和華責備你們的話,

責備我從埃及領出來的整個民族的話,

2『世上萬族之中,我只揀選了你們,

所以我要因你們的罪惡而懲罰你們。』」

3若非相約,

二人怎會同行呢?

4若非捕到獵物,

獅子怎會在林中咆哮呢?

若非獵獲食物,

猛獅怎會在洞中吼叫呢?

5若非設下誘餌,

鳥兒怎會陷入網羅呢?

若非有什麼陷進去,

網羅怎會收起來呢?

6若城中響起號角,

居民豈不恐懼顫抖?

若災禍降臨城中,

豈不是耶和華的作為?

7的確,主耶和華不向祂的僕人——眾先知顯明祂的計劃,

就不會採取任何行動。

8獅子吼叫,誰不懼怕呢?

主耶和華已發言,誰能不傳講呢?

9要向亞實突埃及的城堡宣告:

「你們要聚集到撒瑪利亞的山上,

看看城中的混亂和暴虐之事。

10他們不知正道,強取豪奪,

在他們的堡壘中積斂錢財。

這是耶和華說的。」

11所以,主耶和華說:

「敵人要圍攻此地,

攻破他們的防守,

搶掠他們的城堡。」

12耶和華說:

「牧人從獅口中救羊,

只能奪回兩條腿和一塊耳朵。

同樣,住在撒瑪利亞以色列人被救回的時候,

也僅剩一片床榻和一角臥椅。」

13主——萬軍之上帝耶和華說:

「你們要聽這話,去警告雅各家。

14我追討以色列人的罪時,

要摧毀伯特利的祭壇,

將祭壇的角砍落在地。

15我要拆毀過冬和避暑的房屋,

搗毀象牙裝飾的宮殿,

推倒許多宏偉的樓宇。

這是耶和華說的。」