2 Wathesalonike 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wathesalonike 1:1-12

11:1 Mdo 16:1; 1The 1:1Paulo, Silvano1:1 Yaani Sila. na Timotheo:

Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:

21:2 Rum 1:7; 1Kor 1:3Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.

Shukrani Na Maombi

31:3 1The 3:12; 1:2, 3; 2The 2:13Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka. 41:4 2Kor 7:14; 1The 1:3; 1:6Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.

51:5 Flp 1:28Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake. 61:6 Rum 12:19; Ufu 6:10Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi 71:7 1The 4:16; Yud 14na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu. 81:8 Gal 4:8; Rum 2:8Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu. 91:9 1The 5:3; 2Pet 3:7; 2The 2:8Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, 101:10 1Kor 3:13; Yn 17:10; 1Kor 1:6siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.

111:11 1The 1:3; 2The 1:5Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu. 121:12 Flp 2:9, 11; 1Pet 1:7; 4:14Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.

New International Reader’s Version

2 Thessalonians 1:1-12

1I, Paul, am writing this letter. Silas and Timothy join me in writing.

We are sending this letter to you, the members of the church in Thessalonica. You belong to God our Father and the Lord Jesus Christ.

2May God the Father and the Lord Jesus Christ give you grace and peace.

Paul Prays and Gives Thanks

3Brothers and sisters, we should always thank God for you. That is only right, because your faith is growing more and more. We also thank God that the love you all have for one another is increasing. 4So among God’s churches we brag about the fact that you don’t give up easily. We brag about your faith in all the suffering and testing you are going through.

5All of this proves that when God judges, he is fair. So you will be considered worthy to enter God’s kingdom. You are suffering for his kingdom. 6God is fair. He will pay back trouble to those who give you trouble. 7He will help you who are troubled. And he will also help us. All these things will happen when the Lord Jesus appears from heaven. He will come in blazing fire. He will come with his powerful angels. 8He will punish those who don’t know God. He will punish those who don’t obey the good news about our Lord Jesus. 9They will be destroyed forever. They will be shut out of heaven. They will never see the glory of the Lord’s strength. 10All these things will happen when he comes. On that day his glory will be seen in his holy people. Everyone who has believed will be amazed when they see him. This includes you, because you believed the witness we gave you.

11Keeping this in mind, we never stop praying for you. Our God has chosen you. We pray that he will make you worthy of his choice. We pray he will make every good thing you want to do come true. We pray that he will do this by his power. We pray that he will make perfect all that you have done by faith. 12We pray this so that the name of our Lord Jesus will receive glory through what you have done. We also pray that you will receive glory through what he has done. We pray all these things in keeping with the grace of our God and the Lord Jesus Christ.