2 Wakorintho 5 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wakorintho 5:1-21

Makao Yetu Ya Mbinguni

15:1 1Kor 15:47; Isa 38:12; 1Pet 1:13-14Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. 2Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni, 3kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi. 45:4 1Kor 15:33, 54; Rum 8:23; 2Kor 5:2; 1Kor 15:51Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima. 55:5 Rum 8:23; 2Kor 1:22; Efe 1:13-14Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.

65:6 Ebr 11:13Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana, 75:7 1Kor 13:12; 2Kor 4:18kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona. 85:8 Yn 12:26; Flp 1:23Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana. 95:9 Rum 14:18; Efe 5:10; Kol 1:10; 1The 4:1Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana. 105:10 Mt 16:27; Mdo 10:42; Rum 2:16; 14:10; Efe 6:8Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.

Huduma Ya Upatanisho

115:11 Ay 23:15; Ebr 10:31; 12:29; Yud 23; 2Kor 4:2Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia. 125:12 2Kor 3:1; 1:14Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni. 135:13 2Kor 11:1, 16-17; 12:11Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu. 145:14 Rum 6:6-7; Gal 2:20; Kol 3:3Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa. 155:15 Rum 14:7-9; 4:25Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.

165:16 2Kor 10:4; 11:18Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo. 175:17 Rum 16:3; Yn 1:13; Rum 6:4; Gal 6:15; Isa 65:17; Ufu 21:4-5Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya. 185:18 Rum 11:36; 5:10Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho: 19Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho. 205:20 2Kor 6:1; Efe 6:20; Isa 27:5Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu. 215:21 Ebr 4:15; 7:26; 1Pet 2:22-24; 1Yn 3:5; Rum 1:17; 1Kor 1:30Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.

King James Version

2 Corinthians 5:1-21

1For we know that if our earthly house of this tabernacle were dissolved, we have a building of God, an house not made with hands, eternal in the heavens. 2For in this we groan, earnestly desiring to be clothed upon with our house which is from heaven: 3If so be that being clothed we shall not be found naked. 4For we that are in this tabernacle do groan, being burdened: not for that we would be unclothed, but clothed upon, that mortality might be swallowed up of life. 5Now he that hath wrought us for the selfsame thing is God, who also hath given unto us the earnest of the Spirit. 6Therefore we are always confident, knowing that, whilst we are at home in the body, we are absent from the Lord: 7(For we walk by faith, not by sight:) 8We are confident, I say, and willing rather to be absent from the body, and to be present with the Lord. 9Wherefore we labour, that, whether present or absent, we may be accepted of him. 10For we must all appear before the judgment seat of Christ; that every one may receive the things done in his body, according to that he hath done, whether it be good or bad.

11Knowing therefore the terror of the Lord, we persuade men; but we are made manifest unto God; and I trust also are made manifest in your consciences. 12For we commend not ourselves again unto you, but give you occasion to glory on our behalf, that ye may have somewhat to answer them which glory in appearance, and not in heart. 13For whether we be beside ourselves, it is to God: or whether we be sober, it is for your cause. 14For the love of Christ constraineth us; because we thus judge, that if one died for all, then were all dead: 15And that he died for all, that they which live should not henceforth live unto themselves, but unto him which died for them, and rose again. 16Wherefore henceforth know we no man after the flesh: yea, though we have known Christ after the flesh, yet now henceforth know we him no more. 17Therefore if any man be in Christ, he is a new creature: old things are passed away; behold, all things are become new. 18And all things are of God, who hath reconciled us to himself by Jesus Christ, and hath given to us the ministry of reconciliation; 19To wit, that God was in Christ, reconciling the world unto himself, not imputing their trespasses unto them; and hath committed unto us the word of reconciliation. 20Now then we are ambassadors for Christ, as though God did beseech you by us: we pray you in Christ’s stead, be ye reconciled to God. 21For he hath made him to be sin for us, who knew no sin; that we might be made the righteousness of God in him.