2 Wafalme 9 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 9:1-37

Yehu Atiwa Mafuta Kuwa Mfalme

19:1 1Sam 10:5; 2Fal 8:28Nabii Elisha akamwita mtu mmoja kutoka kwa wana wa manabii na kumwambia, “Jikaze viuno, uichukue hii chupa ya mafuta, na uende Ramoth-Gileadi. 2Ukifika huko, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi. Enda kwake, umtenge na wenzake, na umpeleke katika chumba cha ndani. 39:3 1Fal 19:16Kisha chukua hii chupa na umimine mafuta juu ya kichwa chake, nawe utangaze, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’ Kisha ufungue mlango na ukimbie; usikawie!”

4Basi yule kijana nabii akaenda Ramoth-Gileadi. 5Wakati alipofika, akawakuta maafisa wa jeshi wameketi pamoja, akasema, “Nina ujumbe wako, ee jemadari.”

Yehu akauliza, “Kwa yupi miongoni mwetu?”

Akamjibu, “Kwako wewe, jemadari.”

69:6 1Fal 19:16Yehu akainuka na kuingia ndani ya nyumba. Ndipo yule nabii akamimina mafuta juu ya kichwa cha Yehu na kutangaza, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Bwana, yaani Israeli. 79:7 Mwa 4:24; Kum 32:43Inakupasa uiangamize nyumba ya bwana wako Ahabu, nami nitalipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii na damu ya watumishi wote wa Bwana iliyomwagwa na Yezebeli. 89:8 1Sam 25:22Nyumba yote ya Ahabu itaangamia. Nitamkatilia mbali kila mzaliwa wa kiume wa Ahabu katika Israeli, aliye mtumwa ama aliye huru. 99:9 1Fal 14:10Nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama ile nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama ile nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya. 109:10 1Fal 21:23Kuhusu Yezebeli, mbwa watamla kwenye kiwanja huko Yezreeli, wala hakuna mtu atakayemzika.’ ” Kisha akafungua mlango na kukimbia.

119:11 Yn 10:20; 1Sam 10:11Yehu alipotoka nje na kurudi kwenda kwa maafisa wenzake, mmoja wao akamuuliza, “Je, kila kitu ni salama? Kwa nini huyu mwenye wazimu alikuja kwako?”

Yehu akajibu, “Wewe unamfahamu huyo mtu, na aina ya mambo ambayo yeye husema.”

12Wakasema, “Hiyo siyo kweli! Tuambie.”

Yehu akasema, “Haya ndiyo aliyoniambia: ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’ ”

139:13 Mt 21:8; 2Sam 15:10Wakaharakisha kuvua mavazi yao, na kuyatandaza chini ya Yehu ili akanyage juu kwenye ngazi ya nje. Kisha wakapiga tarumbeta na kupaza sauti wakisema, “Yehu ni mfalme!”

Yehu Anamuua Yoramu Na Ahazia

149:14 Kum 4:43; 2Fal 8:28Basi Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi, akafanya shauri baya dhidi ya Yoramu. (Wakati huu, Yoramu na Israeli wote walikuwa wakiilinda Ramoth-Gileadi dhidi ya Hazaeli mfalme wa Aramu, 159:15 2Fal 8:29lakini Mfalme Yoramu alikuwa amerudishwa Yezreeli ili kujiuguza kutokana na majeraha ambayo Waaramu walimtia katika vita na Hazaeli mfalme wa Aramu.) Yehu akasema, “Kama hii ndiyo nia yenu, msimruhusu hata mmoja kutoroka nje ya mji kwenda kupeleka habari huko Yezreeli.” 169:16 2Nya 22:7Ndipo Yehu akaingia katika gari lake la vita na kuendesha kwenda Yezreeli, kwa sababu Yoramu alikuwa amepumzika huko, na Ahazia mfalme wa Yuda alikuwa ameenda kumwona.

179:17 1Sam 14:16Mlinzi aliyesimama juu ya kinara cha Yezreeli alipoona askari wa Yehu wanakuja, akaita akisema, “Naona askari wanakuja.”

Yoramu akaamuru, “Mtwae mpanda farasi umtume akakutane nao na kuuliza, ‘Je, mmekuja kwa amani?’ ”

18Mpanda farasi akaondoka kwenda kukutana na Yehu na kusema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme: ‘Je, mmekuja kwa amani?’ ”

Yehu akamjibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.”

Mlinzi akatoa habari, “Mjumbe amewafikia lakini harudi.”

19Basi mfalme akamtuma mpanda farasi wa pili. Wakati alipowafikia akasema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme, ‘Je, mmekuja kwa amani?’ ”

Yehu akajibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.”

209:20 2Sam 18:27Yule mlinzi akatoa taarifa akasema, “Mjumbe amewafikia, lakini hata yeye harudi. Uendeshaji ule ni kama wa Yehu mwana wa Nimshi, anaendesha kama mwenye wazimu!”

219:21 1Fal 21:1Yoramu akaagiza, akasema, “Weka tayari gari langu la vita.” Na baada ya gari kuwa tayari, Yoramu mfalme wa Israeli, na Ahazia mfalme wa Yuda, wakaondoka kila mmoja kwenye gari lake ili kukutana na Yehu. Walikutana naye katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli. 229:22 1Fal 18:19Yoramu alipomwona Yehu akauliza, “Je, Yehu, umekuja kwa amani?”

Yehu akajibu, “Kunawezaje kuwa na amani wakati ibada za sanamu na uchawi wa mama yako Yezebeli ungaliko?”

239:23 2Fal 11:14Yoramu akageuka nyuma na kukimbia, akimwambia Ahazia, “Huu ni uhaini, Ahazia!”

249:24 1Fal 22:34Kisha Yehu akatwaa upinde wake na kumchoma Yoramu katikati ya mabega. Mshale ukapenya kwenye moyo wake, naye akaanguka ghafula ndani ya gari lake. 259:25 1Fal 21:19-22Yehu akamwambia Bidkari, mwendeshaji wa gari lake, “Mwinue na umtupe katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli. Kumbuka jinsi mimi na wewe tulivyokuwa tukiendesha pamoja magari yetu nyuma ya Ahabu baba yake, wakati Bwana alipotoa unabii huu kumhusu: 269:26 1Fal 21:19‘Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya wanawe, nami kwa hakika nitakufanya uilipe juu ya shamba hili, asema Bwana.’ Sasa basi, mwinue na umtupe juu ya kiwanja, kulingana na neno la Bwana.”

279:27 Amu 1:27; 2Fal 23:29Wakati Ahazia mfalme wa Yuda alipoona kilichotokea, akakimbia kupitia barabara ya Beth-Hagani. Yehu akamkimbiza akipaza sauti na kusema, “Muue naye pia!” Wakamjeruhi katika gari lake kwenye njia ielekeayo Guri karibu na Ibleamu, lakini akatorokea Megido na akafia huko. 289:28 2Fal 23:30Watumishi wake wakambeba kwa gari la vita na kumpeleka Yerusalemu, wakamzika pamoja na baba zake kwenye kaburi lake katika Mji wa Daudi. 299:29 2Fal 8:25(Katika mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu, Ahazia alianza kutawala katika Yuda.)

Yezebeli Auawa

309:30 Yer 4:30; Eze 23:40Kisha Yehu akaenda Yezreeli. Yezebeli aliposikia habari hii, akayapaka macho yake rangi, akatengeneza nywele zake na kutazama nje dirishani. 319:31 1Fal 16:9-10Yehu alipokuwa akiingia langoni, Yezebeli akasema, “Je, umekuja kwa amani, Zimri, wewe muuaji wa bwana wako?”

32Yehu akaangalia juu dirishani na kuita, “Je, ni nani aliye upande wangu? Ni nani?” Matowashi wawili au watatu wakamtazama. 339:33 Za 7:5Yehu akasema, “Mtupeni huyo mwanamke chini!” Kwa hiyo wakamtupa chini, nayo baadhi ya damu yake ikatapanyika ukutani na nyingine juu ya farasi walipokuwa wakimkanyaga kwa miguu yao.

349:34 1Fal 16:31Yehu akaingia ndani, akala na akanywa. Akasema, “Mshughulikieni huyo mwanamke aliyelaaniwa. Mzikeni, kwa sababu alikuwa binti wa mfalme.” 35Lakini walipotoka kwenda kumzika, hawakukuta kitu chochote isipokuwa fuvu la kichwa, miguu yake na mikono. 369:36 Za 68:23; 1Fal 21:23Wakarudi na kumwambia Yehu, ambaye alisema, “Hili ndilo neno la Bwana alilosema kupitia kinywa cha mtumishi wake Eliya Mtishbi, kwamba: Katika kiwanja cha Yezreeli, mbwa wataikula nyama ya Yezebeli. 379:37 Za 83:10; Yer 8:2Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mavi shambani katika uwanja wa Yezreeli, kwamba hakutakuwepo mtu atakayeweza kusema, ‘Huyu ndiye Yezebeli.’ ”

La Bible du Semeur

2 Rois 9:1-37

Elisée envoie l’un de ses disciples oindre Jéhu

1Le prophète Elisée appela l’un des disciples des prophètes et lui dit : Habille-toi pour partir. Prends cette fiole d’huile et va à Ramoth en Galaad. 2Là tu iras voir Jéhu, fils de Josaphat et petit-fils de Nimshi. Tu l’aborderas et tu lui demanderas de laisser ses compagnons et de te suivre seul dans une pièce retirée. 3Tu prendras la fiole d’huile et tu en verseras le contenu sur sa tête en disant : « Voici ce que déclare l’Eternel : Je te confère l’onction pour t’établir roi d’Israël ! » Puis tu te précipiteras vers la porte et tu t’enfuiras sans attendre.

4Le jeune prophète partit donc pour Ramoth en Galaad. 5Quand il arriva, il trouva les chefs de l’armée d’Israël siégeant ensemble. Il dit : Chef, j’ai un message pour toi.

Jéhu demanda : Pour lequel d’entre nous ?

Il répondit : Pour toi, chef !

6Jéhu se leva et entra dans la maison. Le prophète lui répandit l’huile sur la tête et lui dit : Voici ce que déclare l’Eternel, le Dieu d’Israël : « Je te confère l’onction pour t’établir roi d’Israël, le peuple de l’Eternel9.6 Voir 1 R 19.6.. 7Tu frapperas la maison d’Achab, ton seigneur. Ainsi, je vengerai le meurtre de mes serviteurs les prophètes et celui de tous les serviteurs de l’Eternel assassinés par Jézabel. 8Oui, toute la famille d’Achab périra. J’en exterminerai tous les hommes, esclaves et libres, en Israël. 9Je traiterai cette maison comme j’ai traité celle de Jéroboam, fils de Nebath, et celle de Baésha, fils d’Ahiya9.9 Voir 1 R 15.29 ; 16.11-12.. 10Quant à Jézabel, elle sera dévorée par les chiens dans le domaine de Jizréel, sans qu’il y ait personne pour l’enterrer9.10 Voir 1 R 21.23.. »

Après avoir dit cela, le prophète ouvrit la porte et s’enfuit.

11Lorsque Jéhu revint auprès des autres officiers du roi, ils lui demandèrent : Est-ce que ça va ? Pourquoi cet exalté est-il venu te voir ?

Jéhu leur répondit : Vous connaissez bien ce genre de personnes et leurs divagations.

12Mais ils répliquèrent : Tu mens ! Raconte-nous donc ce qui s’est passé.

– Eh bien, dit-il, voici comment il m’a parlé. Il m’a dit : « Voici ce que déclare l’Eternel : Je te confère l’onction pour t’établir roi d’Israël. »

13A ces mots, les officiers s’empressèrent d’étendre leurs manteaux devant lui sur les marches de l’escalier, puis ils sonnèrent du cor et se mirent à crier : Vive le roi Jéhu !

Jéhu assassine Yoram et Ahazia

14C’est ainsi que Jéhu, fils de Josaphat, petit-fils de Nimshi, forma une conspiration contre Yoram à l’époque où celui-ci défendait, avec tout Israël, Ramoth en Galaad contre Hazaël, roi de Syrie. 15Le roi Yoram était retourné à Jizréel pour se faire soigner des blessures que lui avaient infligées les Syriens pendant le combat contre Hazaël, roi de Syrie. Jéhu dit à ses compagnons : Si vous êtes décidés à vous rallier à moi, il faut que personne ne s’échappe de la ville pour aller annoncer la chose à Jizréel.

16Puis Jéhu monta sur son char et partit pour Jizréel où Yoram était alité et recevait la visite d’Ahazia, le roi de Juda.

17La sentinelle, postée sur la tour de Jizréel, vit venir la troupe de Jéhu et fit dire au roi : J’aperçois une troupe.

Yoram ordonna : Qu’on désigne un cavalier et qu’on l’envoie à leur rencontre pour leur demander s’ils viennent pour la paix.

18Le cavalier se rendit à la rencontre de Jéhu et lui dit : Ainsi parle le roi : « Viens-tu pour la paix ? »

Jéhu répondit : Que t’importe la paix ? Fais demi-tour et passe derrière moi.

La sentinelle fit son rapport en disant : Le messager est arrivé jusqu’à eux, mais il ne revient pas.

19On envoya un deuxième cavalier qui arriva auprès d’eux et dit : Ainsi parle le roi : « Viens-tu pour la paix ? »

Jéhu répondit : Que t’importe la paix ? Fais demi-tour et passe derrière moi.

20La sentinelle fit son rapport en disant : Il est arrivé jusqu’à eux, mais il ne revient pas. Le chef de la troupe conduit son char à la manière de Jéhu, petit-fils de Nimshi : il conduit comme un fou.

(2 Ch 22.7-9)

21Alors Yoram ordonna : Qu’on attelle mon char !

Et l’on attela son char. Yoram, roi d’Israël et Ahazia, roi de Juda, sortirent chacun sur son char pour aller au-devant de Jéhu, ils le rejoignirent dans le champ de Naboth de Jizréel9.21 Voir 1 R 21.1.. 22Dès que Yoram fut à portée de voix de Jéhu, il lui demanda : Viens-tu pour la paix, Jéhu ?

Jéhu répondit : Comment peut-il être question de paix tant que durent les prostitutions de ta mère Jézabel et ses innombrables pratiques de sorcellerie ?

23Alors Yoram fit demi-tour et s’enfuit, en criant à Ahazia : Attention, Ahazia ! c’est une trahison !

24Mais Jéhu saisit son arc et tira. La flèche frappa Yoram entre les deux épaules, lui transperça le cœur et ressortit par la poitrine. Yoram s’effondra mort dans son char. 25Jéhu dit à son écuyer Bidqar : Prends son cadavre et jette-le dans le champ de Naboth de Jizréel ! Te rappelles-tu ? Lorsque nous étions ensemble sur un char derrière son père Achab, l’Eternel a prononcé contre lui cette sentence : 26« Voici ce que déclare l’Eternel : Puisque j’ai vu couler le sang de Naboth et celui de ses enfants, je te le ferai payer dans ce champ même – l’Eternel le déclare9.26 Voir 1 R 21.19. ! » Maintenant donc, emporte-le et jette-le dans ce champ, comme l’Eternel l’a annoncé.

27Quand Ahazia, roi de Juda, vit ce qui se passait, il s’enfuit en direction de Beth-Hagân. Mais Jéhu se lança à sa poursuite et ordonna à ses hommes : Lui aussi, frappez-le sur son char !

Il fut blessé à la montée de Gour près de Yibleam et réussit à fuir jusqu’à Meguiddo où il mourut. 28Ses serviteurs le ramenèrent sur un char à Jérusalem, et l’ensevelirent dans son tombeau à côté de ses ancêtres dans la Cité de David. 29Ahazia était devenu roi de Juda la onzième année du règne de Yoram, fils d’Achab.

La fin de Jézabel

30Jéhu était sur le point d’entrer à Jizréel. A cette nouvelle, Jézabel se farda les yeux, arrangea sa chevelure et se pencha à sa fenêtre pour regarder. 31Lorsque Jéhu eut franchi la porte de la ville, elle lui cria : Viens-tu pour la paix, nouveau Zimri9.31 Allusion à Zimri, qui tua le roi Ela d’Israël 45 ans plus tôt, assassina toute la famille de Baésha, mais ne régna que sept jours (1 R 16.8-20)., assassin de ton seigneur ?

32Il leva les yeux vers la fenêtre et s’écria : Qui de vous est pour moi ? Qui donc ?

Alors deux ou trois chambellans se penchèrent vers lui aux fenêtres. 33Il leur ordonna : Jetez-la en bas !

Ils la précipitèrent dans le vide, et son sang éclaboussa le mur et les chevaux. Jéhu passa sur elle avec son char, 34puis il entra dans le palais pour manger et pour boire. Ensuite, il ordonna à ses compagnons : Occupez-vous de cette femme maudite et enterrez-la. Après tout, c’est une fille de roi9.34 Du roi des Sidoniens (1 R 16.31).. 35Ses hommes allèrent pour la mettre au tombeau, mais ils ne trouvèrent d’elle que son crâne, ses pieds et ses mains. 36Ils retournèrent l’annoncer à Jéhu qui s’écria : C’est bien ce que l’Eternel avait annoncé par son serviteur Elie de Tishbé, lorsqu’il a déclaré : « Les chiens dévoreront le corps de Jézabel dans le champ de Jizréel9.36 Voir 1 R 21.23.. 37Les restes du cadavre de Jézabel seront dispersés comme du fumier épandu sur le sol du champ de Jizréel, de sorte que personne ne pourra dire : C’est Jézabel. »