2 Wafalme 8 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 8:1-29

Ardhi Ya Mshunami Yarudishwa

18:1 2Fal 4:8-37; Kum 28:22Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.” 2Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.

3Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. 4Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.” 58:5 2Fal 4:35Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.

Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.” 6Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza.

Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”

Hazaeli Anamuua Ben-Hadadi

78:7 2Sam 8:5; 2Fal 6:27Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,” 88:8 1Fal 19:15; 1Sam 9:7mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’ ”

9Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’ ”

10Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.” 118:11 Lk 19:41; Amu 3:25Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.

128:12 1Fal 19:17; 2Fal 15:16Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?”

Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”

138:13 1Sam 17:43; 1Fal 19:15Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?”

Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”

14Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.” 158:15 2Fal 1:17Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.

Yehoramu Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 21:1-20)

168:16 2Fal 1:17; 2Nya 21:1-4Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda. 17Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane. 18Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana. 198:19 2Sam 21:17Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.

208:20 1Fal 22:47Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe. 21Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao. 228:22 Mwa 27:40; Yos 21:13Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.

23Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 24Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

Ahazia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 22:1-6)

258:25 2Fal 9:29Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala. 268:26 2Fal 8:18; 1Fal 16:23Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli. 278:27 1Fal 16:30; 15:26Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.

288:28 Kum 4:43; 2Fal 9:1, 14Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu. 298:29 1Fal 21:29; 2Fal 10:13Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi8:29 Yaani Rama kwa Kiebrania. alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu.

Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.

Swedish Contemporary Bible

2 Kungaboken 8:1-29

En kvinna får tillbaka sin mark

1Elisha hade sagt till kvinnan, vars son han hade uppväckt från de döda: ”Ta din familj och flytta till ett annat land, för Herren ska låta en hungersnöd drabba landet, och den kommer att vara i sju år.”

2Kvinnan lydde gudsmannens uppmaning och bosatte sig med sin familj i filistéernas land under sju år. 3När de sju åren hade gått, återvände hon till Israel, där hon sökte upp kungen för att få tillbaka sitt hus och sin mark. 4Just som hon kom in, höll kungen på att tala med Gechasi, gudsmannens tjänare. ”Berätta för mig om de under Elisha har gjort”, bad kungen honom. 5Gechasi berättade då för kungen hur Elisha hade uppväckt en död, och just i det ögonblicket kom kvinnan in, vars son Elisha hade väckt till liv. Hon kom för att be kungen om att få tillbaka sitt hus och sin mark. ”Min herre och kung”, sa Gechasi. ”Här är ju kvinnan och pojken, som Elisha förde tillbaka till livet!”

6Då frågade kungen ut henne, och hon berättade allt för honom. Sedan gav kungen en av sina tjänstemän i uppdrag att se till att hon fick tillbaka allt det hon hade ägt och dessutom ersättning för den inkomst hon förlorat under hela den tid hon varit borta från landet.

Hasael mördar kung Ben-Hadad

7Elisha begav sig till Damaskus i Aram, där kung Ben-Hadad låg sjuk. När han fick veta att gudsmannen var där, 8sa han till Hasael: ”Ta med dig en gåva och gå till gudsmannen och fråga Herren genom honom om jag kommer att bli frisk igen!”

9Hasael gick då för att träffa Elisha och tog med sig det bästa Damaskus hade att erbjuda, så mycket som fyrtio kameler kunde bära. ”Din son Ben-Hadad, kungen i Aram, har sänt mig hit för att fråga om han kommer att bli frisk”, sa han till Elisha.

10”Säg till honom att han ska bli frisk8:10 till honom i denna sats kan möjligen också tolkas som en negation, och i så fall blir översättningen: Säg att han inte kommer att bli frisk.”, svarade Elisha. ”Men Herren har visat mig att han ändå snart kommer att dö.”

11Elisha stirrade så länge på Hasael att denne blev besvärad, och sedan började gudsmannen gråta. 12”Varför gråter du, min herre?” frågade Hasael. ”Därför att jag vet vilka fruktansvärda saker du kommer att göra mot israeliterna”, svarade Elisha. ”Du kommer att bränna ner deras fästningar, döda de unga männen med svärd, krossa de små barnen mot marken och skära upp magen på havande kvinnor.”

13”Hur skulle jag, din tjänare, som bara är en hund, kunna göra något sådant?” sa Hasael. ”Herren har uppenbarat för mig att du kommer att bli kung över Aram”, svarade Elisha.

14När Hasael gick från Elisha och återvände till sin herre, frågade kungen: ”Vad sa han till dig?” ”Han talade om för mig att du skulle bli frisk”, svarade Hasael. 15Men följande dag tog Hasael en filt, doppade den i vatten och höll den över kungens ansikte tills han dog.

Sedan blev Hasael kung.

Joram regerar i Juda

(2 Krön 21:5-10; 21:20)

16Under Jorams, Achavs sons, femte regeringsår i Israel, medan Joshafat var kung i Juda, blev Joram, Joshafats son, kung i Juda. 17Han var trettiotvå år gammal när han blev kung, och han regerade i åtta år i Jerusalem. 18Men han följde kungarna i Israel i spåren, som Achavs familj hade gjort. Han gifte sig med en dotter till Achav. Han gjorde det som var ont i Herrens ögon. 19Men eftersom Herren hade lovat sin tjänare David att han alltid skulle låta en lampa brinna för honom och hans ättlingar, utplånade han inte Juda.

20Under Jorams regering gjorde Edom uppror mot Juda och tog sig en egen kung. 21Joram drog till Sair med alla sina vagnar. På natten bröt han upp och slog edoméerna som hade omringat honom och hans vagnsbefälhavare, men folket flydde hem. 22Sedan Edom gjorde uppror har det inte mer stått under Judas makt. Livna gjorde också uppror vid samma tid.

23Kung Jorams historia i övrigt och vad han gjorde finns nedtecknat i Juda kungars krönika. 24Joram dog och gick till vila hos sina förfäder. Han blev begraven bland dem i Davids stad.

Achasja regerar i Juda

(2 Krön 22:1-6)

Achasja, Jorams son, blev kung efter honom. 25Under det tolfte året av Israels kung Jorams, Achavs sons regering, började Achasja, Jorams son, regera i Juda. 26Achasja var tjugotvå år gammal när han blev kung, och han regerade i ett år i Jerusalem. Hans mor hette Atalja och var sondotter till Israels kung Omri. 27Han vandrade på samma vägar som Achavs familj och gjorde det som var ont i Herrens ögon, så som Achavs familj hade gjort, och han var ingift i Achavs släkt.

28Achasja och kung Joram i Israel, Achavs son, gick till krig mot den arameiske kungen Hasael vid Ramot i Gilead. Joram blev sårad av araméerna 29och vände tillbaka till Jisreel för att få sina sår läkta som tillfogats honom vid Rama i striden mot Arams kung Hasael. Medan han låg sjuk i Jisreel, kom kung Achasja av Juda, Jorams son, på besök till honom.