2 Wafalme 8 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 8:1-29

Ardhi Ya Mshunami Yarudishwa

18:1 2Fal 4:8-37; Kum 28:22Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.” 2Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.

3Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. 4Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.” 58:5 2Fal 4:35Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.

Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.” 6Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza.

Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”

Hazaeli Anamuua Ben-Hadadi

78:7 2Sam 8:5; 2Fal 6:27Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,” 88:8 1Fal 19:15; 1Sam 9:7mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’ ”

9Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’ ”

10Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.” 118:11 Lk 19:41; Amu 3:25Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.

128:12 1Fal 19:17; 2Fal 15:16Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?”

Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”

138:13 1Sam 17:43; 1Fal 19:15Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?”

Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”

14Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.” 158:15 2Fal 1:17Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.

Yehoramu Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 21:1-20)

168:16 2Fal 1:17; 2Nya 21:1-4Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda. 17Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane. 18Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana. 198:19 2Sam 21:17Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.

208:20 1Fal 22:47Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe. 21Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao. 228:22 Mwa 27:40; Yos 21:13Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.

23Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 24Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

Ahazia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 22:1-6)

258:25 2Fal 9:29Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala. 268:26 2Fal 8:18; 1Fal 16:23Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli. 278:27 1Fal 16:30; 15:26Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.

288:28 Kum 4:43; 2Fal 9:1, 14Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu. 298:29 1Fal 21:29; 2Fal 10:13Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi8:29 Yaani Rama kwa Kiebrania. alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu.

Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪下 8:1-29

书念妇人得回产业

1以利沙曾经救活了一位书念妇人的儿子。他对那妇人说:“你和家人要离开这里去别处寄居,因为耶和华已决定使这里遭受七年饥荒。” 2那妇人遵照上帝仆人的话,举家迁往非利士,在那里寄居了七年。 3七年后,她从非利士返回,去向王请求收回自己的房屋和田地。 4那时,王正与上帝仆人的侍者基哈西谈话,让基哈西以利沙所做的一切大事讲给他听。 5基哈西正在向王讲述以利沙如何使死人复活的时候,那位书念妇人刚好进宫求见王,基哈西便说:“我主我王,这就是那妇人,这是她那个被以利沙救活的儿子。” 6王问那妇人,她便原原本本地将那件事禀告王。王委派一位臣仆处理她的事情,并吩咐说:“凡属于这妇人的东西,包括从她离开本地直到今天她田地的所有出产,要全部还给她。”

以利沙对哈薛的预言

7一天,以利沙到了大马士革。当时亚兰便·哈达正在生病,他得知上帝的仆人来了, 8便对哈薛说:“你带着礼物去见上帝的仆人,请他求问耶和华,看看我这病能否痊愈。” 9哈薛用四十头骆驼驮着大马士革的各种美物前去拜见以利沙。到了那里,他站在以利沙面前说:“你儿子亚兰便·哈达派我来问你,他的病能否痊愈?”

10以利沙哈薛说:“你去告诉他,他一定会痊愈。不过,耶和华告诉我他会死。” 11他目不转睛地盯着哈薛,盯得他很不安。然后,上帝的仆人哭了。 12哈薛问:“我主为什么哭呢?”以利沙说:“因为我知道你会加害以色列人。你会放火烧他们的堡垒,用刀杀戮他们的壮丁,摔死他们的孩童,剖开他们的孕妇。” 13哈薛说:“你仆人算什么,不过是一条狗,怎能做这样的大事呢?”以利沙说:“耶和华告诉我,你要做亚兰王。” 14哈薛辞别以利沙回去了。王问他:“以利沙对你说什么?”他答道:“以利沙告诉我,你一定会痊愈。” 15第二天,哈薛拿了一床浸透水的被子,蒙在王的脸上,王窒息而死。于是哈薛篡位。

约兰做犹大王

16以色列亚哈的儿子约兰执政第五年,犹大约沙法让位给儿子约兰17约兰三十二岁登基,在耶路撒冷执政八年。 18他与亚哈家一样步以色列诸王的后尘,因为他娶了亚哈的女儿为妻,做耶和华视为恶的事。 19但耶和华因祂仆人大卫的缘故而不愿毁灭犹大,因为祂曾应许让大卫的子孙永远做王。 20约兰执政期间,以东人反叛犹大,自己立王。 21约兰率领所有战车前往撒益,他和战车长们被以东人包围。他们乘夜出击,突出重围,各自逃回家去。 22以东人至今仍脱离犹大的统治。立拿人也在那个时候叛变了。

23约兰其他的事及其一切所作所为都记在犹大列王史上。 24约兰与祖先同眠后,葬在大卫城他的祖坟里。他儿子亚哈谢继位。

亚哈谢做犹大王

25以色列亚哈的儿子约兰执政第十二年,犹大约兰的儿子亚哈谢登基。 26他二十二岁登基,在耶路撒冷执政一年。他母亲叫亚她利雅,是以色列暗利的孙女。 27亚哈谢亚哈家的女婿,他步亚哈家的后尘,做耶和华视为恶的事。

28他联合亚哈的儿子约兰基列拉末亚兰哈薛交战。约兰受了伤, 29便回到耶斯列疗伤。犹大亚哈谢前去探望。