2 Wafalme 5 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 5:1-27

Naamani Aponywa Ukoma

15:1 Mwa 10:22; Lk 4:27Wakati huu, Naamani alikuwa jemadari wa jeshi la mfalme wa Aramu. Alikuwa mtu mkuu mbele ya bwana wake na aliyeheshimiwa sana, kwa sababu kupitia kwake, Bwana alikuwa amewapa Aramu ushindi. Alikuwa askari shujaa, lakini alikuwa na ukoma.5:1 Ukoma ni neno lililotumika kwa Kiebrania kueleza magonjwa mbalimbali ya ngozi ambayo si lazima yawe ni ukoma halisi.

25:2 2Fal 6:23Siku hizo vikosi kutoka Aramu vilikuwa vimekwenda na vikawa vimemteka msichana kutoka Israeli, naye akamtumikia mkewe Naamani. 35:3 Mwa 20:7Akamwambia bibi yake, “Kama bwana wangu angelimwona nabii aliyeko Samaria! Angemponya ukoma wake.”

4Naamani akaenda kwa bwana wake na kumwambia alichosema yule msichana kutoka Israeli. 55:5 Mwa 24:53; 1Sam 9:7Mfalme wa Aramu5:5 Yaani mfalme wa Shamu. akamjibu, “Hakika, nenda. Nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaondoka, akiwa amechukua talanta kumi5:5 Talanta 10 za fedha ni sawa na kilo 340. za fedha, shekeli 6,000 za dhahabu,5:5 Shekeli 6,000 za dhahabu ni sawa na kilo 70. na mivao kumi ya mavazi. 6Barua aliyopelekea mfalme wa Israeli iliandikwa hivi: “Pamoja na barua hii ninamtuma mtumishi wangu, Naamani, kwako ili uweze kumponya ukoma wake.”

75:7 Mwa 30:2; Kum 32:39; 1Fal 20:7Mara mfalme wa Israeli alipomaliza kuisoma ile barua, akararua mavazi yake na kusema, “Je, mimi ni Mungu? Je, mimi naweza kuua na kufufua tena? Kwa nini huyu mtu anamtuma mtu ili mimi nipate kumponya ukoma wake? Tazama jinsi anavyotafuta kuanzisha ugomvi nami!”

85:8 1Fal 22:7Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alikuwa amerarua mavazi yake, akamtumia ujumbe huu: “Kwa nini umerarua mavazi yako? Mwamuru mtu huyo aje kwangu, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.” 9Kwa hiyo Naamani akaenda, akiwa na farasi zake na magari yake, na kusimama mlangoni mwa nyumba ya Elisha. 105:10 Yn 9:7; Law 14:7Elisha akamtuma mjumbe kumwambia, “Nenda uoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itapona, nawe utatakasika.”

115:11 Kut 7:19Lakini Naamani akaondoka akiwa amekasirika, akasema, “Hakika nilidhani kwamba angetoka nje, asimame na kuliitia jina la Bwana Mungu wake, na kuweka mkono wake juu ya mahali pagonjwa, aniponye ukoma wangu. 125:12 Mit 14:17, 29Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora zaidi kuliko mito yoyote ya Israeli? Je, nisingeweza kuoga ndani ya hiyo mito na kutakasika?” Basi akageuka na kuondoka kwa hasira kuu.

135:13 2Fal 6:21Watumishi wa Naamani wakamwendea na kumwambia, “Baba yangu, kama huyo nabii angekuambia kufanya jambo lililo kubwa, je, usingelifanya? Je, si zaidi sana basi, anapokuambia, ‘Oga na utakasike!’ ” 145:14 Law 14:7; Ay 33:25Hivyo akashuka na kujizamisha ndani ya Yordani mara saba, kama vile huyo mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia, nayo nyama ya mwili wake ikapona na kutakasika kama ya mwili wa mvulana mdogo.

155:15 Yos 4:24; 1Sam 17:46Kisha Naamani na wahudumu wake wote wakarudi kwa yule mtu wa Mungu. Akasimama mbele yake na kusema, “Sasa najua kwamba hakuna Mungu katika ulimwengu wote isipokuwa katika Israeli. Tafadhali sasa upokee zawadi kutoka kwa mtumishi wako.”

165:16 Mwa 14:23; Dan 5:17Nabii akajibu, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ninamtumikia, sitapokea kitu hata kimoja.” Ingawa Naamani alimsihi sana, yeye alikataa.

175:17 Kut 20:24Naamani akasema, “Ikiwa hutapokea, tafadhali mtumishi wako na apewe udongo kiasi cha mzigo wa kuweza kubebwa na punda wawili, kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa na dhabihu kwa mungu mwingine isipokuwa Bwana. 185:18 2Fal 7:2Lakini Bwana na amsamehe mtumishi wake kwa kitu hiki kimoja: Wakati bwana wangu atakapoingia kwenye hekalu la Rimoni ili kusujudu, naye akiwa anauegemea mkono wangu, nami nikasujudu huko pia, wakati nitakaposujudu ndani ya hekalu la Rimoni, Bwana na amsamehe mtumishi wako kwa ajili ya jambo hili.”

195:19 1Sam 1:17; Mdo 15:33Elisha akamwambia, “Nenda kwa amani.”

Baada ya Naamani kusafiri umbali fulani, 205:20 Kut 20:7Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akajiambia mwenyewe, “Bwana wangu amemwachia kirahisi sana Naamani, huyu Mwaramu, kwa kutokupokea kutoka kwake vile alivyovileta. Hakika kama Bwana aishivyo, nitamkimbilia na kupata kitu kutoka kwake.”

21Hivyo Gehazi akaharakisha kumfuatilia Naamani. Naamani alipomwona akikimbia kumwelekea, akashuka chini kutoka kwenye gari lake na kwenda kumlaki. Akauliza, “Je, mambo yote ni sawa?”

225:22 2Fal 5:5; Mwa 45:22Gehazi akajibu, “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma nikuambie, ‘Vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamenijia kutoka nchi ya vilima ya Efraimu. Tafadhali wape talanta ya fedha5:22 Talanta ya fedha ni sawa na kilo 34. na mivao miwili ya mavazi.’ ”

23Naamani akasema, “Hakika, chukua talanta mbili za fedha.” Akamsihi Gehazi azipokee, kisha akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili pamoja na mivao miwili ya mavazi. Akawapa watumishi wake wawili mizigo hiyo, nao wakaibeba wakitangulia mbele ya Gehazi. 24Gehazi alipofika kwenye kilima, akavichukua vile vitu kutoka kwa wale watumishi na kuvificha ndani ya nyumba. Akawaaga wale watu, nao wakaondoka. 25Kisha akaingia ndani na kusimama mbele ya Elisha bwana wake.

Elisha akamuuliza, “Gehazi, ulikuwa wapi?”

Gehazi akajibu, “Mtumishi wako hakwenda popote.”

265:26 2Fal 5:16; Yer 45:5Lakini Elisha akamwambia, “Je, roho yangu haikuwa pamoja nawe wakati yule mtu aliposhuka kutoka kwenye gari lake ili kukulaki? Je, huu ni wakati wa kupokea fedha au kupokea nguo, mashamba ya mizeituni, mashamba ya mizabibu, makundi ya kondoo na mbuzi, makundi ya ngʼombe, au watumishi wa kiume na wa kike? 275:27 Hes 12:10; Kut 4:6Ukoma wa Naamani utakushika wewe na wazao wako milele.” Kisha Gehazi akaondoka mbele ya Elisha, mwenye ukoma, mweupe kama theluji.

Священное Писание

4 Царств 5:1-27

Исцеление Наамана от проказы

1Нааман был военачальником царя Сирии. Он был великим и уважаемым человеком в глазах своего господина, потому что через него Вечный даровал Сирии победу. Он был доблестным воином, но болел проказой5:1 На языке оригинала здесь и далее в этой книге стоит слово, которое обозначает несколько разных кожных болезней, а не только проказу.. 2А отряды сирийцев во время одного из набегов взяли в Исраиле в плен маленькую девочку, и она служила жене Наамана. 3Она сказала госпоже:

– Если бы только моему господину повидать пророка, который в Самарии! Он исцелил бы его от болезни.

4Нааман пошёл к господину и передал ему то, что сказала девочка из Исраила.

5– Конечно иди, – ответил царь Сирии. – Я напишу письмо царю Исраила.

И Нааман пошёл, взяв с собой триста шестьдесят килограммов серебра, семьдесят два килограмма5:5 Букв.: «десять талантов… шесть тысяч шекелей». золота и десять смен одежды. 6В письме, которое он принёс царю Исраила, говорилось: «Когда ты получишь это письмо, знай, что я послал к тебе моего слугу Наамана, чтобы ты вылечил его от проказы».

7Когда царь Исраила прочитал это письмо, он разорвал на себе одежду и сказал:

– Разве я Всевышний, чтобы умерщвлять и оживлять? Почему он посылает ко мне, чтобы я исцелил от проказы? Смотрите, он пытается затеять со мной ссору!

8Когда пророк Елисей услышал о том, что царь Исраила разорвал на себе одежду, он послал сказать ему:

– Почему ты разорвал на себе одежду? Пошли этого человека ко мне, и он узнает, что есть пророк в Исраиле.

9Нааман пришёл с конями и колесницами и остановился у двери дома Елисея. 10Елисей отправил посланца сказать ему:

– Пойди, омойся семь раз в Иордане, твоё тело исцелится, и ты станешь чист.

11Но Нааман разгневался и ушёл, говоря:

– Я думал, что он непременно выйдет ко мне, встанет, призовёт имя Вечного, своего Бога, поводит рукой над больным местом и исцелит меня от проказы. 12Разве Авана и Фарфар, реки Дамаска, не лучше всех вод Исраила? Разве я не мог омыться в них, чтобы очиститься?

Он повернулся и в гневе ушёл. 13Слуги Наамана подошли к нему и сказали:

– Отец, если бы пророк сказал тебе сделать нечто великое, разве бы ты этого не сделал? А он лишь сказал тебе: «Омойся и будешь чист».

14Тогда он пошёл и семь раз окунулся в Иордане, как сказал ему пророк, – и его тело исцелилось и стало чистым, как у младенца. 15Нааман со слугами вернулся к пророку. Он встал перед ним и сказал:

– Теперь я знаю, что во всём мире нет Бога, кроме как в Исраиле. А теперь, прошу, прими от твоего раба подарок.

16Пророк ответил:

– Верно, как и то, что жив Вечный, Которому я служу, – я ничего не приму.

И хотя Нааман уговаривал его, он отказался.

17– Если ты не желаешь, – сказал Нааман, – то прошу тебя, пусть твоему рабу дадут столько земли5:17 Большинство неисраильтян верило, что божеству можно поклоняться только на земле, принадлежащей этому божеству, или же соорудив ему жертвенник из этой земли., сколько сможет увезти пара мулов, потому что твой раб никогда больше не будет приносить всесожжения и жертвы никакому богу, кроме Вечного. 18Пусть только Вечный простит твоего раба за одно: когда мой господин входит в храм Риммона5:18 Риммон – сирийский бог-громовержец., чтобы поклониться там, и опирается на мою руку, я кланяюсь тоже. Когда я буду кланяться в храме Риммона, пусть Вечный простит за это твоего раба.

19– Иди с миром, – сказал Елисей.

Гехази наказан проказой

Когда Нааман уже отошёл на некоторое расстояние, 20Гехази, слуга пророка Елисея, сказал себе: «Мой господин отпустил этого сирийца Наамана слишком легко, не взяв у него никаких даров. Верно, как и то, что жив Вечный, – я побегу за ним и возьму у него что-нибудь». 21И Гехази помчался за Нааманом. Когда Нааман увидел, как он бежит к нему, он слез с колесницы, чтобы встретить его.

– Всё ли благополучно? – спросил он.

22– Всё благополучно, – ответил Гехази. – Просто мой господин послал меня сказать: «Два молодых ученика пророков пришли ко мне из нагорий Ефраима. Прошу тебя, дай им тридцать шесть килограммов5:22 Букв.: «один талант». серебра и две смены одежды».

23– Конечно! Бери семьдесят два килограмма5:23 Букв.: «два таланта»., – сказал Нааман.

Он уговорил Гехази взять семьдесят два килограмма серебра в двух мешках, вместе с двумя сменами одежды. Он отдал их двум слугам, и они понесли их перед Гехази. 24Когда Гехази пришёл на холм, он взял это у слуг и положил у себя дома. Он отпустил людей, и они ушли. 25После этого он вошёл и встал перед своим господином Елисеем.

– Где ты был, Гехази? – спросил Елисей.

– Твой раб никуда не ходил, – ответил Гехази.

26Но Елисей сказал ему:

– Разве не был с тобой мой дух, когда Нааман слез с колесницы, чтобы встретить тебя? Время ли брать деньги или принимать одежды, масличные рощи, виноградники, отары, стада, слуг или служанок? 27Так пусть проказа Наамана пристанет к тебе и твоим потомкам навеки.

И когда Гехази вышел от Елисея, он был бел от проказы, как снег.